CHADEMA kugeuka dampo la wanasiasa rejected

CHADEMA kugeuka dampo la wanasiasa rejected

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
38,638
Reaction score
49,048
Hakuna tofauti na recycle bin, Kule ambako kila material ambayo haihitajiki hupelekwa,

Chama kinapokea rejects, watu waliokua disappointed na kuona kwamba hawatapata nafasi tena huko walipokua, wanageuka mashujaa.

Kwa minajili hiyo CHADEMA will always second CCM katika kila hali, maana waliokwenda huko hawana nia ya dhati ya ukombozi bali kulinda tu heshima na maslahii binafsi.

Mtu anapiga hesabu anaona hakubaliki, au hatapata nafasi anasema CCM ni mafisadi anakimbilia CHADEMA, na huko anakokwenda wanampokea kwa mikono miwili bila kuuliza muda wote ule uliokua unanafasi kwanini hukuwahi kuja huku, leo wakati umekataliwa ndio ujione mtetezi wa haki??

Sidhani kama uongozi wa Chadema unawatendea haki wanachama wamda mrefu waliopoteza muda wao, na kuwapokea watu ili waje kugombea tu, ni jambo la wazi kabisa kua ni personal gains na si kwa benefit of all.

Sasa kwa siasa hizi za kupokea makapi, Chadema inakua kama recycle bin, kila reject inkua stored pale, inaleta picha kua, Chadema kipo kwa ajili ya kutimiza malengo ya watu binafsi.
 
kachek vizr ubongo wako huenda umeshaliwa na funyo.

UKAWA tumeanza mavuno ya viongozi na wanachama wa ccm hata kabla hatujaanza kampeni, ulipaswa kutupongeza we vipi
 
Nadhani CCM Nao wanachukua Wanachama toka Upinzani na Siyo Reject Kama Unavyotaka Kutuaminisha. Ndg yangu Kanuni za Kipolitics zinatuambia ''Kumpoteza Mwanachama mmoja Mwaminifu gharama yake ni Kubwa Kuliko Kumtafuta Mwanachama Mpya".

Sababu kubwa ikiwa ya Kwamba,Mwanachama Mzoefu na Mwaminifu akienda Upande wa pili anachofanya ni Kumwaga Sumu Kwa kuelezea Mabaya tu, na Hata Mbinu zitumiwaozo Kuhalalisha Gori la Mkono.

Pili Kumpata Mwanachama Mpya hasa Kipindi Hiki Credibility yake inakuwa Kwenye Question mark (???), Pia Mbinu za Kusaidia Kuwezesha Gori la Mkono Hazijui Vizur.
 
sasa CHADEMA ikiwa Recycle Bin inakuuma nini wewe?
 
stroke

Duh!! kweli mmeishiwa hoja yaani leo hii mnawaita Reject hivi inawezekana chama kikawa na Madiwani 20 kutoka jimbo moja na wengine 19 kutoka jimbo moja wote wakawa Reject? hiyo Reject unayoiandika wewe sijui umejitafakari kwa kina, ila watakapopata ridhaa ya kugombea tena kupitia CHADEMA(UKAWA) na wakapata nafasi hizo sijui utaiweka wapi sura yako maana hao unaowaita Reject wananchi wao wanawathamini na kuwaona ni watu muhimu kwa maendeleo yao.
 
Last edited by a moderator:
Chadema wamejenga chama ila wakipokea makapi kitaisha taratibu huwezi kupokea makapi halafu ubaki salama.
 
Hata wewe mwenyewe mleta post unaweza kuwa wa uzazi wa rejects.Yaani Baba na ...... wote walikuwa ni rejects za relations zao
 
stroke

........Inaonekana MAFURIKO yamekupa msongo wa mawazo kwa kimombo wanaita (stress). SAA YA UKOMBOZI NI SASA. OOOOOOOH!!!
 
Last edited by a moderator:
Kama ulikuwa haujui haki zako ni kuwa kila mtu anayo haki ya kuamia Chama chochote ata dr slah au mbowe wanayo haki Kwenda ccm siku yoyote
 
Chadema wamejenga chama ila wakipokea makapi kitaisha taratibu huwezi kupokea makapi halafu ubaki salama.

Maana halisi ya makapi ni kile kitu kilichoachwa baada ya kuonekana hakifai, je kwa hawa Madiwani wa CCM wanaoondoka CCM na kuingia CHADEMA wameachwa na CCM au wamefukuzwa uanachama? kama jibu litakuwa hapana sidhani kama hiki ulichokiandika kitakuwa na maana halisi unayokusudia
 
Kama madiwani 40 na wapiga kura wao zaidi ya laki 5 mnawaita reject basi UKAWA wanawahitaji sana hao reject, kama wapo na wengine waambie mlango uko wazi.
 
Maana halisi ya makapi ni kile kitu kilichoachwa baada ya kuonekana hakifai, je kwa hawa Madiwani wa CCM wanaoondoka CCM na kuingia CHADEMA wameachwa na CCM au wamefukuzwa uanachama? kama jibu litakuwa hapana sidhani kama hiki ulichokiandika kitakuwa na maana halisi unayokusudia

Tumia CS (common sense ) huwezi kuuliza swali ukajijibu.
 
Kama madiwani 40 na wapiga kura wao zaidi ya laki 5 mnawaita reject basi UKAWA wanawahitaji sana hao reject, kama wapo na wengine waambie mlango uko wazi.

Ccm wanatapatapa Madiwani 40+ hawawezi kuwa rejected
 
Back
Top Bottom