Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoa wa Arusha kimeeleza kusikitishwa na taarifa ya kuzuiwa kufanya mkutano wao wa hadhara uliopangwa kufanyika kesho Mei 28, 2025, katika viwanja vya Kilombero Jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Arusha, Elisa Stephano Mungure ameeleza kuwa Chama hicho kilikuwa tayari kimewasilisha barua kwa Jeshi la Polisi Mei 22, 2025, kuwajulisha kuhusu mkutano huo, ambao unatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi wa kitaifa wa chama hicho wakiongozwa na John Heche, Hata hivyo, leo wamejulishwa na Jeshi la Polisi kuwa mkutano huo hauwezi kufanyika katika viwanja hivyo kutokana na ujenzi unaoendelea.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Chadema wamedai kuwa maelezo ya Jeshi la Polisi si ya kweli na kwamba hakuna ujenzi wowote unaoendelea katika eneo hilo. Aidha, Jeshi la Polisi limewashauri waandae mkutano huo katika kiwanja kingine.
Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Arusha, Elisa Stephano Mungure ameeleza kuwa Chama hicho kilikuwa tayari kimewasilisha barua kwa Jeshi la Polisi Mei 22, 2025, kuwajulisha kuhusu mkutano huo, ambao unatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi wa kitaifa wa chama hicho wakiongozwa na John Heche, Hata hivyo, leo wamejulishwa na Jeshi la Polisi kuwa mkutano huo hauwezi kufanyika katika viwanja hivyo kutokana na ujenzi unaoendelea.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Chadema wamedai kuwa maelezo ya Jeshi la Polisi si ya kweli na kwamba hakuna ujenzi wowote unaoendelea katika eneo hilo. Aidha, Jeshi la Polisi limewashauri waandae mkutano huo katika kiwanja kingine.