Mafyangula
JF-Expert Member
- Jan 16, 2025
- 505
- 887
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinalaani vikali wimbi la ukamataji, utekaji na vitisho vinavyoendelea dhidi ya viongozi na wanachama wake katika Kanda ya Victoria, hususani mkoani Kagera.
Tarehe 16 Oktoba 2025, viongozi na wanachama zaidi ya saba wamekamatwa na vyombo vya dola mkoani Kagera katika mazingira yenye utata bila maelezo yoyote rasmi kutoka kwenye vyombo vya ulinzi na usalama wa raia.
Matukio haya yanajiri wakati ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiendelea na kampeni zake za Urais kwenye kanda hiyo inayojumuisha mikoa ya Mwanza, Geita na Kagera.
Miongoni mwa waliokamatwa ni:
Aidha, Khalid Swarehe (Makamu Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Victoria), bado anashikiliwa gerezani baada ya kupwepeshwa kesi ya wizi wa kutumia silaha tofauti na kosa analoshitakiwa nalo.
Tarehe 16 Oktoba 2025, viongozi na wanachama zaidi ya saba wamekamatwa na vyombo vya dola mkoani Kagera katika mazingira yenye utata bila maelezo yoyote rasmi kutoka kwenye vyombo vya ulinzi na usalama wa raia.
Matukio haya yanajiri wakati ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiendelea na kampeni zake za Urais kwenye kanda hiyo inayojumuisha mikoa ya Mwanza, Geita na Kagera.
Miongoni mwa waliokamatwa ni:
- Chief Adronicus Kalumuna (Mwenyekiti wa Chadema jimbo la Bukoba Mjini na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Kanda ya Victoria)
- Paulo Shijason Musisi (Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa)
- Daniel Damian Lwebugisa (Katibu wa Chadema Mkoa wa Kagera)
- Egbert Aloyce Kikulega (Mwanachama)
- Ramadhan Fadhiri (Mwanachama)
- Levocatus Willison (Mwanachama)
- Baziri Waziri (Katibu wa Jimbo la Kyerwa)
Aidha, Khalid Swarehe (Makamu Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Victoria), bado anashikiliwa gerezani baada ya kupwepeshwa kesi ya wizi wa kutumia silaha tofauti na kosa analoshitakiwa nalo.