Nakuunga mkono sana, hao vijana wa CHADEMA walitoa pendekezo la kijinga la kutaka maandamano na mwenyekiti wao bila kuangalia athari za maandamano kuwa hazitajenga chama bali kukibomoa akatangaza maandamano, ni bora wangecchukua ile ya Halimma Mdee kutoka BAWACHA ingekisaidia sana chama, maandamano yanaleta taswira mbaya.CDM bado ndio mkombozi tatizo hawajapata mwanya wa kutokea maana CCM piga ua wamebana kila kona na wakiishiwa wanajua pa kukwapua. Kueneza sera na itikadi ya chama nchi nzima kunahitaji mtaji mkubwa sana ambao CDM hawana. Wananchi wengi sana wana hamu ya kukisikia chama hiki lakini hawapati fursa kwa sababu hakuna ofisi sehemu nyingi tu ziwe za kata, tawi au jimbo.
CDM ingetumia mikutano ya hadhara zaidi kuliko maandamano kufikisha ujumbe kwa wananchi. CCM wameshahakikisha CDM haitafanya maandamano kwa kuagiza polisi iwadhibiti vilivyo.
Tujikite kwenye hoja tuache kupayuka. Hoja ni hizi:
1. Je ccm ni chama cha wez na mafisadi?
2. Je kuna mafisadi waccm walioiba bila kunawasasa wanataka na urais?
3 je ccm imeshindwa kuwaendeea vijana?.
4. Je kuna uwezekano wowote ata asilimia 5 tu kw chadema kuchukuanchi
5. Je chadema imetuangusha watanzaniia?
6. Je independentcandidates watakuwa mbadala wa chadema?
Tuache ukutoa pumba tujikite kwenye hizi hoja mujarabu tujenge nchi yetu
rekebisha hapo hayo maneno mkuu, CHADEMA kinapigania maslahi ya watu wa kaskazini tu ndiyo maana bila hata haya viongozi wote wa safari hii wanatoka north.
CHADEMA imekwisha imebaki ya matusi na maandamano. Wanahubiri amani huku wameficha mapanga. Kinajiita chama cha Demokrasia na Maendeleo lakini demokrasia yake lazima ukubaliane na Mbowe na Slaa, ukitofautiana nao unaitwa msaliti na kufukuzwa. Rejea waraka wa Marehemu Chacha Wangwe!
Wanahubiri kupinga ufisadi huku Mwenyekiti wake ituhumiwa kutumia hela za walipa kodi kula bata na kimada Dubai.
Wanahubiri kupinga ufisadi huku Mweyekiti wake akituhumiwa kuchukua hela kwa Nimrod Mkono ili asipige kampeni
jimboni kwake apite bila kupigwa.
Hiyo ndio CDM, demokrasia kwao ni kutoka vyama vingine na kuhamia CHADEMA, lakini ukitoka CDM kwenda chama kingine wanasema ni msaliti na -----------! Walisema CUF ni CCM B, wanafuata sera ya ushoga lakini leo CUF imekuwa CCM A na imeacha sera ya ushoga wako pamoja kwenye UKAWA
Hiyo ndio CDM, walimfukuza David Kafulila na kumwita maneno yote ya kejeli lakini leo tena Mbowe amemteua huyohuyo Kafulila waliyemwona hafai kuwa Waziri kivuli.