CHADEMA Kimetuangusha Watanzania

galiya

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2012
Posts
302
Reaction score
133
Chama cha mainduzi ni chama au genge la wezi wanaokula bila kunawa na mafisadi waliokithiri. Hili ni genge la mijitu iliyo very selfish ambayo haitaipeleka nchi yetu popote ndo maana mwalimu nyerere alisema ni sawa na dodoki. CCM haina nia njema na wananchi wa nchi hii na hasa vijana.

Nccr ikaja na vijana wengi tukajiunga chini ya A.Mrema tulipiga nginjanginja nchi nzima but baadae tukagundua Mrema ni boya tukajiunga na chadema .

Tulitegmea mengi kutoka hiki chama lakini nacho ni kama NCCR tu, hamna jipya. kila muda unavyoenda ndivo kinavyozidi kupungua nguvu. Wote tunajua kua wabunge chadema 2015 watakuwa wachache mno. Independentcandidates ndo watakaochukua nafasi za wabunge wa chadema. Chadema kimetuangusha kama ilivokuwa kwa nccr.

Kwa mtazamo wangu chadema imebugi, mambo yote ni independent candidates . Mnaonaje?
 

ndiyo chama cha nchi gani hicho?
 
mtoa post huna akili wewe.jaribu kutumia akili.hakuna chama makini jama chadema
 
Nimeshindwa kukuelewa apa mkuu……
sasa ni kipi unakiamini kama kitatea maslai ya wananchi? Nikiangalia kwenye uzi wako ni dhahiri chadema umeipaka matope kuliko vyama vyote ulivyo vitaja apo juu, je ni chadema pekee ambayo inafanya mabaya na yakupotiliza ktk taifa letu?… mimi ni mwanachama wa chadema na ndio tumaini langu naomba unishawishi kwa hoja mzto ili nisikae kuamin kama chadema ndio mkombozi wa 2 katka taifa letu…

Nitafurai nikipata majibu yaliyonyoka

Thanks
 

rekebisha hapo hayo maneno mkuu, CHADEMA kinapigania maslahi ya watu wa kaskazini tu ndiyo maana bila hata haya viongozi wote wa safari hii wanatoka north.
 
Wewe mwenyewe mleta mada umeanza kufoka kabla ya kujadili.
 
CDM bado ndio mkombozi tatizo hawajapata mwanya wa kutokea maana CCM piga ua wamebana kila kona na wakiishiwa wanajua pa kukwapua. Kueneza sera na itikadi ya chama nchi nzima kunahitaji mtaji mkubwa sana ambao CDM hawana. Wananchi wengi sana wana hamu ya kukisikia chama hiki lakini hawapati fursa kwa sababu hakuna ofisi sehemu nyingi tu ziwe za kata, tawi au jimbo.

CDM ingetumia mikutano ya hadhara zaidi kuliko maandamano kufikisha ujumbe kwa wananchi. CCM wameshahakikisha CDM haitafanya maandamano kwa kuagiza polisi iwadhibiti vilivyo.
 
Mapambano sio kitu rahisi,ndio maana yakaitwa mapambano.
 
Mi naona kama umechanginyikiwa totally!
 
We unalijua hilo leo? Wenzako tushalitambua hilo kitaaaamboo! Cdm kwasasa inatafuta kiki kupitia maandamano pia kutaka kutoa watu kafara kwa maslahi yao binafsi!

Wasiojitambua watakuwa ni wahanga wa kafara hii!
 
CHADEMA imekwisha imebaki ya matusi na maandamano. Wanahubiri amani huku wameficha mapanga. Kinajiita chama cha Demokrasia na Maendeleo lakini demokrasia yake lazima ukubaliane na Mbowe na Slaa, ukitofautiana nao unaitwa msaliti na kufukuzwa. Rejea waraka wa Marehemu Chacha Wangwe!

Wanahubiri kupinga ufisadi huku Mwenyekiti wake ituhumiwa kutumia hela za walipa kodi kula bata na kimada Dubai.
Wanahubiri kupinga ufisadi huku Mweyekiti wake akituhumiwa kuchukua hela kwa Nimrod Mkono ili asipige kampeni
jimboni kwake apite bila kupigwa.

Hiyo ndio CDM, demokrasia kwao ni kutoka vyama vingine na kuhamia CHADEMA, lakini ukitoka CDM kwenda chama kingine wanasema ni msaliti na -----------! Walisema CUF ni CCM B, wanafuata sera ya ushoga lakini leo CUF imekuwa CCM A na imeacha sera ya ushoga wako pamoja kwenye UKAWA

Hiyo ndio CDM, walimfukuza David Kafulila na kumwita maneno yote ya kejeli lakini leo tena Mbowe amemteua huyohuyo Kafulila waliyemwona hafai kuwa Waziri kivuli.
 
Acheni kutoa mapovu jengeni hoja. Acheni kufikiri kwa kutumia masaburi
 
matusi na mandamano havitawapeleka ikulu wala kutatua matatizo ya watanzania
 

Unatumia kipimo gani kuonesha kupungua kwa nguvu ya chadema?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…