Mimi ni mgeni humu, sipendi siasa na wala ushabiki, mimi ni victim of several circumtances wa mambo kibao katika nchi hii, nimekuwa nafuatilia maswala mengi ya nchi hii zikiwemo siasa, kuna vitu vingi nimejifunza, sasa hebu niwape kisa kimoja, nilikuwa pale Uganda , yupo mtu mmoja anaitwa ELIAS LUKWAAGO, huyu bwana aligombea umeya wa jiji la Kampala kupitia chama pinzani akashinda kwa kishindo, baada ya hapo serikali ya Museveni haikumpa ushirikiano kabisa na kwa taarifa nilizo pata ni kwamba badala yake aliajiriwa mama mmoja aitwaye JENIFER MUSISI,, akapewa cheo cha DIRECTOR OF KAMPALA CITY COUNCIL AUTHORITY , Akawa anafanya kazi zote za jiji ikiwemo tenda na ukusanyaji wa kodi na ukarabati wa mji wote wa kampala, meya akitaka kufanya kitu ilibidi apate kibali toka kwa huyu mama, mambo yalienda hivyo mpaka Meya akafukuzwa kwenye ofisi, akawa kila mara anafanya maandamano mpaka mda wake umeisha. Wananchi wamemchagua tena ila wamesusia uchaguzi wa madiwani upande wa upinzani hawakujitokeza baada ya Besigye kufanyiwa kitu mbaya, hivo akajikuta anashinda peke yake kuwa meya na madiwani wote wa chama tawala, kule uganda meya anachaguliwa na watu wa mitaa ya jiji husika si madiwani wenzake, so hali itaendelea kuwa tete. Nirudi hapa Tanzania, Rais magufuli nyote mnajua sio mtu wa siasa, ni mtu wa action, hapendi mizaha na ni mwepesi sana wa kufanya maamuzi magumu sana, kukata tawi alilo kalia hata kama atahatarisha mgongo wake potelea mbali. Yaliyompata LUKWAGO yanaweza kuwapata UKAWA kama hawakuwa smart kwenye masuala nyeti, kutukana kukejeli kubeza, na kukaidi mambo yanayo fanywa na serikali ya Magufuli hakutakuwa na impact kwa siasa za sasa, hasa pale ambapo watu wengine tena hata wa upinzani wanadiriki kumtaja magu kama ndo raisi waliyemtaka hata kama hawakumchagua, uongo na usannii wa watu wa ukawa watu hawaukubali tena, nilikuwa Bukoba juzi mtu mmoja akansikizisha crp moja jinsi watu wanavyo mkubali rais na wanajuta kumchagua RWAKATARE nilishangaa. So ukawa be very technical, work slowly with Jpm ili awe fair kwa minajili kwamba hata maamuzi na matakwa yenu yapate kibali, vinginevyo wananchi wa Tanzania ni wwpesi wa kubadilika mnaweza kupoteza uchaguzi ujao na msije mkashangaa, Nawapenda na kuwaombea .