CHADEMA isitishe maandamano

CHADEMA isitishe maandamano

Heshima sana wanajamvi wote.

Kwanza napenda kuwajulisha wanajamvi wote Ngongo si mwanachama wa chama chochote cha siasa Tanzania ila ni mpenzi wa siasa.Ninaposema ni mpenzi wa siasa nina maana ninapenda kushiriki,kusikiliza na kushauriana masuala yote yahusuyo siasa bila kuwa mwanachama wa chama cha siasa.Kwahiyo unapochangia mjadala huu ni vyema ukijikita zaidi katika hoja.

Ni jambo lililo wazi Tanzania inapita katika kipindi kigumu sana tangu kuhasisiwa kwa taifa hili.Vikao vya bunge maalamu la kutunga katiba mpya vinaendelea mjini Dodoma huku baadhi ya wajumbe (UKAWA) wa bunge hilo wakisusia vikao hivyo kwasababu ambazo kwa kiasi fulani hata mimi nakubaliana nazo.Sina haja ya kueleza kwanini tumefikia hapa kwakuwa najua wengi wenu tunazijua sababu hizo ingawa kumekuwa na juhudi kubwa za kimkakati/propaganda za kupotosha kwa maksudi sababu zilizopelekea UKAWA kususia bunge la katiba.

Vyombo vya habari hasa vile vinavyomilikiwa na serekali na chama tawala vimekuwa vikipotosha ukweli kwa makusudi ya kupandikiza taswira mbaya ya UKAWA mbele ya macho ya jamii ya kitanzania hasa wale wasiopenda kuchambua mambo kwa undani.

CHADEMA sijui kama UKAWA wamo katika hii hoja ya maandamano wamekuwa wakipaza sauti za malalamiko na sasa wanataka kuanzisha maandamano nchi nzima kama sehemu ya kuonyesha kutorizishwa na jinsi mchakato wa kuandika katiba mpya unavyopaswa kwenda.Ni kweli bunge la Bwana Sitta limekosa viwango,limekosa ushirikishwa wa mawazo ya wananchi,limejivika kazi za tume ya kukusanya maoni,limekosa mjumuiko wa makundi yote (wanaCCM wametamalaki),limekataa mawazo ya wananchi,limekumbatia mawazo ya watawala.halina maana kabisaaaaa.

Ukweli ni kwamba sababu za kuandamana zipo nyingi sana lakini Ngongo wa JF anakataa maandamano kwasababu ambazo nitazieleza.

Maandamano hayajawahi kuleta mabadiliko chanya Tanzania badala yake yameacha makovu makubwa ambayo hatujawahi kuona matunda yake hata kidogo. Mji wa Arusha ni mfano mzuri wananchi waliandamana kudai uchaguzi wa haki wa meya wa Jiji la Arusha mpaka leo bado meya ni yuleyule na ikumbukwe kuna wananchi walipoteza maisha yao kwaajili ya kuhakikisha haki inapatikana.

Kwanini nakataa maandamano sasa.Nakataa maandamano kwasababu wananchi waliopoteza maisha yao kwaajili ya kuitikia wito wa maandamano mpaka leo hawajatendewa haki.Kuna wanawake leo hii ni wajane wana watoto wanashindwa kupata elimu,afya,lishe stahiki kwakuwa hawana Baba wa kuwatunza.CDM kama chama mpaka leo hawajachukua hatua za kisheria kuhakikisha walioshiriki kutoa uhai wa raia wasiokuwa na silaha wanafikishwa mahakamani,sijasikia wanasheria wa CDM wakisubutu kuanzisha mchakato wa kuishitaki serekali ICC kwa mauaji ya raia.

CDM ilidai ina mkanda wa watu walioshiriki kurusha bomu uwanja wa Soweto Arusha,tena walidai polisi walishiriki kuhakikisha mrusha bomu hakamatwi na raia kwa kurusha risasi ili kumkinga asikamatwe.Siju huo mkanda umewekwa kwaajili gani wakati inajulikana kuna wananchi walipoteza maisha yao pasipo sababu za maana.Ikiwa CDM kweli ina mkanda ni kwanini mpaka leo bado imeukali inasubiri nini kwaajili ya manufaa ya nani au ndio mtaji wake mwaka 2015 ?.Vipi waliopoteza maisha au baada ya kuzikwa na kupiga mapicha za mazishi ndio basi.

CDM iache kucheza na maisha ya watanzania kama kweli inataka maandamano lazima watueleze wananchi walipoteza maisha wamefanyiwa nini ?.Tunajua upande wa serekali imefanya nini kwa makamanda wa mikoa yote yalipofanyika mauaji wengi wamepandishwa vyeo kwa kazi nzuri na njema ya kusimamia mauaji ya wananchi upande wa CDM watuambie familia za waanga wa maandamano na mikutano yake wamewafanyia nini ?.

Naomba kuwasilisha.
Mkuu Ngongo, asante kwa hii!, kuna watu humu tumekuwa tunakutana kwenye threads mbali mbali na kupitia michango yao humu, unajikuta unawafahamu wamesimamia wapi!, kwa jinsi nilivyokufahamu Mkuu Ngongo, nilidhani nakufahamu, kumbumbe nilikuwa sikufahamu, ila kwa uzi huu, leo ndio nimekufahamu!, hili kundi la tusio na vyama humu jukwaani ni kundi dogo lenye wachache ila ndio ndio wawakilishi wa Watanzania walio wengi ambao hawana vyama ambao mwisho wa siku wao ndio wahanga wakuu wa matokeo ya hizi harakati za vyama!.

Hongera sana Mkuu Ngongo kwa kusimama na kuhesabiwa!.

Asante.

Pasco
 
Acha waandamane siku nyingi zimepita bila kusikia vurugu na vifo; vurugu ndio mtaji wa Chadema
 
..askari aliyemlipua Mwangosi amefikishwa mahakamani na kesi yake inaendelea.

..suala la familia ya Mwangosi kudai fidia linategemea hukumu itakayotolewa kwenye kesi hiyo.

..pia kuna hatari kwamba ikiwa CDM watakuwa mstari wa mbele kudai fidia kwa niaba ya familia ya Mwangosi, basi CCM na serikali wataamua kesi hiyo kisiasa.

..mwisho, hivi kwanini tunawalaumu CDM ktk suala hili na siyo Raisi, serikali, na CCM? Raisi Kikwete amempandisha cheo kamanda aliyekuwa incharge siku Mwangosi ameuawa. What does that tell you?


Freeland, Pasco, Manyerere Jackton

Mkuu JokaKuu Umegusia jambo la msingi sana,kwamba wa kulaumiwa ni watawala...lakini inajulikana kuwa watawala wameyafanya haya yote kwa makusudi kabisa ndio maana katika kesi zote hizo hakuna aliyewajibishwa....Hakuna polisi aliyechukuliwa hatua kwa mauaji...wala hakuna mtuhumiwa yeyote walau amedhibitiwa....

Lakini Ngongo wote tukiwa "well wishers" hasa kwa maisha ya watu waliopotea tunatakiwa tufikiri namna bora zaidi hata ya kuwashauri CHADEMA namna ya ku deal na hizo cases....Kwenda mahakamani kwangu mimi inaweza isiwe very good option...Mahakama haziko huru....maamuzi ya kesi yanaweza kufanywa kisiasa zaidi......

Umetumia ishu ya kunywa chai ikulu kama kitu ambacho chadema wasingefanya.....walau naweza kukubaliana na wewe ukiwa na maana kwamba hawa wawe adui kabisa na wasisalimiane....lakini je...hiyo ndio justice kwa waliofiwa?

Mimi nadhani CHADEMA wangeenda mahakamani kudai rulling au ufafanuzi wa kisheria kuhusu mamlaka ya Jeshi la Polisi katika ishu ya maandamano.........je ni kutoa kibali au ni kupewa taarifa tu?
 
Last edited by a moderator:
..sasa hebu nikuulize: mkakati wa Raisi, na CCM, unaelewa? Je, umeridhika nao?

..halafu wakati mwingine ni wa-Tz wenyewe tunaowashinikiza Ukawa wakazungumze Ikulu, halafu Raisi asipotekeleza yale waliyokubaliana tunawalaumu Ukawa.

..hivi kwa akili za kawaida, bunge la katiba lilipaswa kuendelea baada ya makubaliano yaliyofikiwa kati ya vyama vya upinzani na Raisi? Kwanini hatumlaumu Samuel Sitta kwa kiburi anachokionyesha kwa Raisi? Kwanini hatumlaumu Raisi kwa kumdekeza Samuel Sitta? Badala yake kwanini tunawalaumu Ukawa?

cc MTAZAMO

Mkuu hilo swala la Bunge la katiba ni ishu ambayo hutakiwi kujidanganya kuwa analofanya Sitta hana maelekezo ya Kikwete....Analofanya sitta ndiolo maelekezo ya kikwete na ccm na serikali yao...Kile kikao cha kikwete na Ukawa ni kwamba kikwete amewapiga chenga ya Mwili UKAWA....Kikao kile hakina mamlaka ya kutoa maamuzi "enforceable" kisheria.....Ni sawa na kigenge cha kahawa tu
 
CCM isitishe bunge la katiba. Vurugu zote chanzo ni matumizi mabaya ya madaraka na.fedha za walipa kodi. Kwa nini watu wafungiwe biashara kwa kutokulipa kodi halafu wengine watumbue hela kidogo inayopatikana kwa starehe zao? Kwa kuwa walioko bungeni ni wanachama wa CCM ni kwa nini hawalipwi na chama chao?
 
Heshima sana wanajamvi wote.

Kwanza napenda kuwajulisha wanajamvi wote Ngongo si mwanachama wa chama chochote cha siasa Tanzania ila ni mpenzi wa siasa.Ninaposema ni mpenzi wa siasa nina maana ninapenda kushiriki,kusikiliza na kushauriana masuala yote yahusuyo siasa bila kuwa mwanachama wa chama cha siasa.Kwahiyo unapochangia mjadala huu ni vyema ukijikita zaidi katika hoja.

Ni jambo lililo wazi Tanzania inapita katika kipindi kigumu sana tangu kuhasisiwa kwa taifa hili.Vikao vya bunge maalamu la kutunga katiba mpya vinaendelea mjini Dodoma huku baadhi ya wajumbe (UKAWA) wa bunge hilo wakisusia vikao hivyo kwasababu ambazo kwa kiasi fulani hata mimi nakubaliana nazo.Sina haja ya kueleza kwanini tumefikia hapa kwakuwa najua wengi wenu tunazijua sababu hizo ingawa kumekuwa na juhudi kubwa za kimkakati/propaganda za kupotosha kwa maksudi sababu zilizopelekea UKAWA kususia bunge la katiba.

Vyombo vya habari hasa vile vinavyomilikiwa na serekali na chama tawala vimekuwa vikipotosha ukweli kwa makusudi ya kupandikiza taswira mbaya ya UKAWA mbele ya macho ya jamii ya kitanzania hasa wale wasiopenda kuchambua mambo kwa undani.

CHADEMA sijui kama UKAWA wamo katika hii hoja ya maandamano wamekuwa wakipaza sauti za malalamiko na sasa wanataka kuanzisha maandamano nchi nzima kama sehemu ya kuonyesha kutorizishwa na jinsi mchakato wa kuandika katiba mpya unavyopaswa kwenda.Ni kweli bunge la Bwana Sitta limekosa viwango,limekosa ushirikishwa wa mawazo ya wananchi,limejivika kazi za tume ya kukusanya maoni,limekosa mjumuiko wa makundi yote (wanaCCM wametamalaki),limekataa mawazo ya wananchi,limekumbatia mawazo ya watawala.halina maana kabisaaaaa.

Ukweli ni kwamba sababu za kuandamana zipo nyingi sana lakini Ngongo wa JF anakataa maandamano kwasababu ambazo nitazieleza.

Maandamano hayajawahi kuleta mabadiliko chanya Tanzania badala yake yameacha makovu makubwa ambayo hatujawahi kuona matunda yake hata kidogo. Mji wa Arusha ni mfano mzuri wananchi waliandamana kudai uchaguzi wa haki wa meya wa Jiji la Arusha mpaka leo bado meya ni yuleyule na ikumbukwe kuna wananchi walipoteza maisha yao kwaajili ya kuhakikisha haki inapatikana.

Kwanini nakataa maandamano sasa.Nakataa maandamano kwasababu wananchi waliopoteza maisha yao kwaajili ya kuitikia wito wa maandamano mpaka leo hawajatendewa haki.Kuna wanawake leo hii ni wajane wana watoto wanashindwa kupata elimu,afya,lishe stahiki kwakuwa hawana Baba wa kuwatunza.CDM kama chama mpaka leo hawajachukua hatua za kisheria kuhakikisha walioshiriki kutoa uhai wa raia wasiokuwa na silaha wanafikishwa mahakamani,sijasikia wanasheria wa CDM wakisubutu kuanzisha mchakato wa kuishitaki serekali ICC kwa mauaji ya raia.

CDM ilidai ina mkanda wa watu walioshiriki kurusha bomu uwanja wa Soweto Arusha,tena walidai polisi walishiriki kuhakikisha mrusha bomu hakamatwi na raia kwa kurusha risasi ili kumkinga asikamatwe.Siju huo mkanda umewekwa kwaajili gani wakati inajulikana kuna wananchi walipoteza maisha yao pasipo sababu za maana.Ikiwa CDM kweli ina mkanda ni kwanini mpaka leo bado imeukali inasubiri nini kwaajili ya manufaa ya nani au ndio mtaji wake mwaka 2015 ?.Vipi waliopoteza maisha au baada ya kuzikwa na kupiga mapicha za mazishi ndio basi.

CDM iache kucheza na maisha ya watanzania kama kweli inataka maandamano lazima watueleze wananchi walipoteza maisha wamefanyiwa nini ?.Tunajua upande wa serekali imefanya nini kwa makamanda wa mikoa yote yalipofanyika mauaji wengi wamepandishwa vyeo kwa kazi nzuri na njema ya kusimamia mauaji ya wananchi upande wa CDM watuambie familia za waanga wa maandamano na mikutano yake wamewafanyia nini ?.

Naomba kuwasilisha.

Kila roho itaonja mauti, sasa kama unaogopa kufa ili ubaki ukinyanyaswa, hiyo ni habari nyingine. Watu wanaona bora wafe ghafla kuliko manyanyaso wanayoyapata hapa duniani dhidi ya Chama tawala. hakuna dhambi kubwa kama Uoga.
 
Ni kweli hoja zako zinaweza kuwa na mantiki lakini zimekosa ujasiri, je ni kweli hujaona watoto ambao wazazi wao wapo lakini bado wanakosa hayo yote??? Usiwe wa kukata tamaa kwani hata wale waliouwawa maumau ndio kwanza sasa wanalipwa nina hakika chini ya chadema wafu hawa wataheshimika kam mashujaa na nina imani hata mbinguni pia. Maisha yalipofika ni ya kujitolea na kujitoa tukiwa wachoyo kwa kuipeleka ubinafsi mbele hatuisaidii hii nchi na kama ndivyo basi mtu wa kwanza kufanya hivyo angekuwa Mbowe ambae ana kila haki ya kutumbua utajiri wake na kutia timu na mafisadi la kini leo kwa zaidi ya miaka 20 anavaa kombati akiacha suti zake za ghali zikiharibika na kufubaa kabatini,. Ukweli ni kwamba wewe utakuwa mbinafsi kwa kuona tu afueni ya maisha yako, lakini maisha kwa watu wengi sana sasa hakuna tufauti na kifo, wakati kifo na maisha havina tofauti watu wanatakiwa kuchukua hatua, ndio maana wengine badala ya kusubiri kifo nyumbani wanaona ni bora kufanya hata wizi ili pengine atatoka!!!!! Chukua Hatua Mkuu!! Nchi hii sasa imeshaharibika mtu anauwawa kwa kuiba simu pengine akamlipie ada mwanae ambae amefukuzwa shule lakini wale wa EPA na fedha za Uswiss wanatandikiwa mazuria mekundu kwa heshima kubwa. Hebu ndugu yangu fuatilia kwa makini magazeti kila siku ipo ripoti mpya ya wizi wa fedha za umma, lakini magereza yamejaa wezi wa kuku na simu. Wizi wa sasa hivi ni wa hand to mouth...... hii inadhihirisha ukata na ukali wa maisha. Unakuta jamaa wamekuja iba lakini kabla wanaanza na kutafuta chakula wale ndio waibe.........???????????!!!!!!!!! Thinka about this, think twice

Heshima sana wanajamvi wote.

Kwanza napenda kuwajulisha wanajamvi wote Ngongo si mwanachama wa chama chochote cha siasa Tanzania ila ni mpenzi wa siasa.Ninaposema ni mpenzi wa siasa nina maana ninapenda kushiriki,kusikiliza na kushauriana masuala yote yahusuyo siasa bila kuwa mwanachama wa chama cha siasa.Kwahiyo unapochangia mjadala huu ni vyema ukijikita zaidi katika hoja.

Ni jambo lililo wazi Tanzania inapita katika kipindi kigumu sana tangu kuhasisiwa kwa taifa hili.Vikao vya bunge maalamu la kutunga katiba mpya vinaendelea mjini Dodoma huku baadhi ya wajumbe (UKAWA) wa bunge hilo wakisusia vikao hivyo kwasababu ambazo kwa kiasi fulani hata mimi nakubaliana nazo.Sina haja ya kueleza kwanini tumefikia hapa kwakuwa najua wengi wenu tunazijua sababu hizo ingawa kumekuwa na juhudi kubwa za kimkakati/propaganda za kupotosha kwa maksudi sababu zilizopelekea UKAWA kususia bunge la katiba.

Vyombo vya habari hasa vile vinavyomilikiwa na serekali na chama tawala vimekuwa vikipotosha ukweli kwa makusudi ya kupandikiza taswira mbaya ya UKAWA mbele ya macho ya jamii ya kitanzania hasa wale wasiopenda kuchambua mambo kwa undani.

CHADEMA sijui kama UKAWA wamo katika hii hoja ya maandamano wamekuwa wakipaza sauti za malalamiko na sasa wanataka kuanzisha maandamano nchi nzima kama sehemu ya kuonyesha kutorizishwa na jinsi mchakato wa kuandika katiba mpya unavyopaswa kwenda.Ni kweli bunge la Bwana Sitta limekosa viwango,limekosa ushirikishwa wa mawazo ya wananchi,limejivika kazi za tume ya kukusanya maoni,limekosa mjumuiko wa makundi yote (wanaCCM wametamalaki),limekataa mawazo ya wananchi,limekumbatia mawazo ya watawala.halina maana kabisaaaaa.

Ukweli ni kwamba sababu za kuandamana zipo nyingi sana lakini Ngongo wa JF anakataa maandamano kwasababu ambazo nitazieleza.

Maandamano hayajawahi kuleta mabadiliko chanya Tanzania badala yake yameacha makovu makubwa ambayo hatujawahi kuona matunda yake hata kidogo. Mji wa Arusha ni mfano mzuri wananchi waliandamana kudai uchaguzi wa haki wa meya wa Jiji la Arusha mpaka leo bado meya ni yuleyule na ikumbukwe kuna wananchi walipoteza maisha yao kwaajili ya kuhakikisha haki inapatikana.

Kwanini nakataa maandamano sasa.Nakataa maandamano kwasababu wananchi waliopoteza maisha yao kwaajili ya kuitikia wito wa maandamano mpaka leo hawajatendewa haki.Kuna wanawake leo hii ni wajane wana watoto wanashindwa kupata elimu,afya,lishe stahiki kwakuwa hawana Baba wa kuwatunza.CDM kama chama mpaka leo hawajachukua hatua za kisheria kuhakikisha walioshiriki kutoa uhai wa raia wasiokuwa na silaha wanafikishwa mahakamani,sijasikia wanasheria wa CDM wakisubutu kuanzisha mchakato wa kuishitaki serekali ICC kwa mauaji ya raia.

CDM ilidai ina mkanda wa watu walioshiriki kurusha bomu uwanja wa Soweto Arusha,tena walidai polisi walishiriki kuhakikisha mrusha bomu hakamatwi na raia kwa kurusha risasi ili kumkinga asikamatwe.Siju huo mkanda umewekwa kwaajili gani wakati inajulikana kuna wananchi walipoteza maisha yao pasipo sababu za maana.Ikiwa CDM kweli ina mkanda ni kwanini mpaka leo bado imeukali inasubiri nini kwaajili ya manufaa ya nani au ndio mtaji wake mwaka 2015 ?.Vipi waliopoteza maisha au baada ya kuzikwa na kupiga mapicha za mazishi ndio basi.

CDM iache kucheza na maisha ya watanzania kama kweli inataka maandamano lazima watueleze wananchi walipoteza maisha wamefanyiwa nini ?.Tunajua upande wa serekali imefanya nini kwa makamanda wa mikoa yote yalipofanyika mauaji wengi wamepandishwa vyeo kwa kazi nzuri na njema ya kusimamia mauaji ya wananchi upande wa CDM watuambie familia za waanga wa maandamano na mikutano yake wamewafanyia nini ?.

Naomba kuwasilisha.
 
Mkuu Bulldog nisome vizuri bandiko # 1 nimesema wazi vikao vya Dodoma limekosa uhalali wa kuwepo kwake,limejivika kazi za tume ya kukusanya maoni na mwisho nikasema halina maana kabisa.Ikiwa halina maana kabisa maana yake fedha wanazotumia zingepaswa kupelekwa maeneo mengine,pengine ni lugha tu tunapishana.

Laiti CDM wangeonyesha kuwajali wale wote waliopoteza maisha,waliopata ulemavu kwa maana ya kuhakikisha wanawapatia msaada wa kisheria,kuhakikisha ajenda ya waliokufa katika mikutano ya siasa inapewa umuhimu wa juu siku zote hakika leo hii ningekuwa mtu wa mwanzo kabisa kuunga mkono maandamano yao.

Kwanini mnadhani maandamano ni ya kuleta fujo tu?/
 
Mimi nakubaliana kwamba iko haja ya kuwa na mikakati endelevu katika mapambano ya kudai haki. napendekeza yafuatayo:
1. CHADEMA wafanyie kazi maoni hayo ya kwamba lazima kuwe na mkakati unaohakikisha kwamba wale ambao wanakuwa wahanga wa moja kwa moja wa operesheni za kudai haki, wanaenziwa.
2. kwa kuwa wanachodai CHADEMA ni kwa maslahi mapana ya taifa, na kwa kuwa CHADEMA peke yao hawatafaulu kufikia azma hiyo, ni vema wakaungwa mkono na vyama vingine na wananchi kwa ujumla. siyo vibaya watu binafsi kujitolea kutoa misaada ya hali na mali, kuanzisha mijadala kuchambua mambo haya, kuhusiana na wanafamilia wa wahanga wa operesheni, na kutoa ushauri pia.

3. CHADEMA wasiudharau muungano wa UKAWA. wasilewe na kubweteka na kusonga mbele peke yao. ushirikiano na vyama vingine katika operesheni hii ni wa muhimu sana

Ni wakati muafaka wa kufanya mambo kisayansi zaidi na kwa matokeo bora zaidi
 
Mkuu Bulldog sijawahi kuona fujo katika maadamano yoyote,fujo utokea pale polisi wanapokataa maandamano yasifanyike.Sijawahi kusikia raia wametoa uhai wa mtu kwasababu ya maandamano ila nimewahi kusikia na kushuhudia polisi wakirusha mabomu hovyo pasipo sababu za msingi na wakati mwingine unaweza kufikiri labda mabomu yalikuwa karibu ku expire ndio maana wanayavurumisha hovyo tena wakati mwingine katika sehemu ambazo hakuna viashiria vya maandamano.

Mkuu wangu nakataa maandamano kwasababu waanga wa maandamano na mikutano ya CDM wanasahaulika baada ya muda mfupi sana.


Kwanini mnadhani maandamano ni ya kuleta fujo tu?/
 
Last edited by a moderator:
Mkuu JokaKuu Umegusia jambo la msingi sana,kwamba wa kulaumiwa ni watawala...lakini inajulikana kuwa watawala wameyafanya haya yote kwa makusudi kabisa ndio maana katika kesi zote hizo hakuna aliyewajibishwa....Hakuna polisi aliyechukuliwa hatua kwa mauaji...wala hakuna mtuhumiwa yeyote walau amedhibitiwa....

Lakini Ngongo wote tukiwa "well wishers" hasa kwa maisha ya watu waliopotea tunatakiwa tufikiri namna bora zaidi hata ya kuwashauri CHADEMA namna ya ku deal na hizo cases....Kwenda mahakamani kwangu mimi inaweza isiwe very good option...Mahakama haziko huru....maamuzi ya kesi yanaweza kufanywa kisiasa zaidi......

Umetumia ishu ya kunywa chai ikulu kama kitu ambacho chadema wasingefanya.....walau naweza kukubaliana na wewe ukiwa na maana kwamba hawa wawe adui kabisa na wasisalimiane....lakini je...hiyo ndio justice kwa waliofiwa?

Mimi nadhani CHADEMA wangeenda mahakamani kudai rulling au ufafanuzi wa kisheria kuhusu mamlaka ya Jeshi la Polisi katika ishu ya maandamano.........je ni kutoa kibali au ni kupewa taarifa tu?

..ndugu yangu tatizo lingine ni kwamba we are so used to being abused.

..tumefika mahali mpaka tunatafuta justification ya ukatili tunaofanyiwa na CCM na serikali yake.

..mfano mzuri wa hoja yangu hapo juu ni haya malalamiko na lawama kwa CDM kwamba maandamano yao yanasababisha wananchi kumwaga damu.

..binafsi sikumbuki kusikia waandamanaji wa CDM wamejeruhi polisi au raia mwingine yeyote. badala yake ni wao ndiyo wanaojeruhiwa au hata kuuwawa na polisi. katika mazingira hayo kwanini tuwalaumu CDM badala ya Polisi?

..kule Arusha kuna watoto wameuawa kutokana na harakati za Polisi kuwafanyia vurugu waandamanaji. Pamoja na hayo hakuna anayepaza sauti kulaani ukatili huo, badala yake lawama zinaelekezwa kwa victims.
 
Mkuu hilo swala la Bunge la katiba ni ishu ambayo hutakiwi kujidanganya kuwa analofanya Sitta hana maelekezo ya Kikwete....Analofanya sitta ndiolo maelekezo ya kikwete na ccm na serikali yao...Kile kikao cha kikwete na Ukawa ni kwamba kikwete amewapiga chenga ya Mwili UKAWA....Kikao kile hakina mamlaka ya kutoa maamuzi "enforceable" kisheria.....Ni sawa na kigenge cha kahawa tu

..YES, maamuzi ya kikao cha Raisi na Ukawa siyo "enforceable" kisheria.

..lakini kwa uelewa wangu maamuzi yale yalitakiwa yafanyiwe kazi kisheria na Samuel Sitta na Mwanasheria Mkuu.

..tatizo letu ni kwamba tunaleta mizaha kwa mambo ambayo hatutakiwi kufanya mizaha nayo.

..kama Raisi alifanya mazungumzo yale akiwa ameazimia "kuwapiga chenga" Ukawa basi naye atakuwa ni mtu anayefanya mizaha kwenye mambo yasiyostahili mizaha.

..tatizo ni kwamba wananchi tumezoea mizaha na ubabaishaji kiasi kwamba tunafikia hata kusifia mambo kama hayo.

cc Ngongo
 
Last edited by a moderator:
Mkuu JokaKuu ukisoma mababandiko ya Mkuu Nguruvi3 utatambua vikao vya Ikulu havina tija yoyote zaidi ya kuwapoteze muda na kumbisha mikakati ya UKAWA.Sidhani kama kiburi cha Sitta ni chake yeye kama yeye hapana nijuavyo mimi tayari kulikuwa na mikakati ya CCM kuhakikisha wanapitisha katiba bila kufuata rasimu ya Mzee Warioba.Rejea vikao vya kamati kuu ya CCM na matamko ya Kinana na Nape Nnauye.So kama UKAWA walijua Kikwete asingeweza kwenda kinyume cha kamati kuu ya chama chake ni kwanini UKAWA walikuwa nawalilia kwenda Ikulu ?.Kikwete huyu wa sasa hasa ubavu wa kukataa matakwa ya chama chake hasa ukizingatia muda wake unazidi kuyoyoma.

..CDM lazima waende kwenye hivyo vikao.

..hiyo itawawezesha kujenga hoja huku kwa wananchi kwamba walikwenda mpaka kwa Raisi lakini hoja zao zimepuuzwa.
 
Wanazi wa CDM nakumbuka nilitoa ushauri huu mapema kama angalizo lakini kwa bahati mbaya hakuna kiongozi aliyekuwa tayari kufuata au kusikiliza matokeo yake kila mmoja wetu anajua.Haya endeleeni kutia pamba masikioni mwenu iko siku mtajajikuta mnaangukia pua kwa kukataa ushauri wa maana.

Mrema alikuwa hivi hivi kila anachoambiwa hakutaka kusikia, masikio yakazidi kichwaa leo hii amekuwa kichekesho mbele ya jamii.


Heshima sana wanajamvi wote.

Kwanza napenda kuwajulisha wanajamvi wote Ngongo si mwanachama wa chama chochote cha siasa Tanzania ila ni mpenzi wa siasa.Ninaposema ni mpenzi wa siasa nina maana ninapenda kushiriki,kusikiliza na kushauriana masuala yote yahusuyo siasa bila kuwa mwanachama wa chama cha siasa.Kwahiyo unapochangia mjadala huu ni vyema ukijikita zaidi katika hoja.

Ni jambo lililo wazi Tanzania inapita katika kipindi kigumu sana tangu kuhasisiwa kwa taifa hili.Vikao vya bunge maalamu la kutunga katiba mpya vinaendelea mjini Dodoma huku baadhi ya wajumbe (UKAWA) wa bunge hilo wakisusia vikao hivyo kwasababu ambazo kwa kiasi fulani hata mimi nakubaliana nazo.Sina haja ya kueleza kwanini tumefikia hapa kwakuwa najua wengi wenu tunazijua sababu hizo ingawa kumekuwa na juhudi kubwa za kimkakati/propaganda za kupotosha kwa maksudi sababu zilizopelekea UKAWA kususia bunge la katiba.

Vyombo vya habari hasa vile vinavyomilikiwa na serekali na chama tawala vimekuwa vikipotosha ukweli kwa makusudi ya kupandikiza taswira mbaya ya UKAWA mbele ya macho ya jamii ya kitanzania hasa wale wasiopenda kuchambua mambo kwa undani.

CHADEMA sijui kama UKAWA wamo katika hii hoja ya maandamano wamekuwa wakipaza sauti za malalamiko na sasa wanataka kuanzisha maandamano nchi nzima kama sehemu ya kuonyesha kutorizishwa na jinsi mchakato wa kuandika katiba mpya unavyopaswa kwenda.Ni kweli bunge la Bwana Sitta limekosa viwango,limekosa ushirikishwa wa mawazo ya wananchi,limejivika kazi za tume ya kukusanya maoni,limekosa mjumuiko wa makundi yote (wanaCCM wametamalaki),limekataa mawazo ya wananchi,limekumbatia mawazo ya watawala.halina maana kabisaaaaa.

Ukweli ni kwamba sababu za kuandamana zipo nyingi sana lakini Ngongo wa JF anakataa maandamano kwasababu ambazo nitazieleza.

Maandamano hayajawahi kuleta mabadiliko chanya Tanzania badala yake yameacha makovu makubwa ambayo hatujawahi kuona matunda yake hata kidogo. Mji wa Arusha ni mfano mzuri wananchi waliandamana kudai uchaguzi wa haki wa meya wa Jiji la Arusha mpaka leo bado meya ni yuleyule na ikumbukwe kuna wananchi walipoteza maisha yao kwaajili ya kuhakikisha haki inapatikana.

Kwanini nakataa maandamano sasa.Nakataa maandamano kwasababu wananchi waliopoteza maisha yao kwaajili ya kuitikia wito wa maandamano mpaka leo hawajatendewa haki.Kuna wanawake leo hii ni wajane wana watoto wanashindwa kupata elimu,afya,lishe stahiki kwakuwa hawana Baba wa kuwatunza.CDM kama chama mpaka leo hawajachukua hatua za kisheria kuhakikisha walioshiriki kutoa uhai wa raia wasiokuwa na silaha wanafikishwa mahakamani,sijasikia wanasheria wa CDM wakisubutu kuanzisha mchakato wa kuishitaki serekali ICC kwa mauaji ya raia.

CDM ilidai ina mkanda wa watu walioshiriki kurusha bomu uwanja wa Soweto Arusha,tena walidai polisi walishiriki kuhakikisha mrusha bomu hakamatwi na raia kwa kurusha risasi ili kumkinga asikamatwe.Siju huo mkanda umewekwa kwaajili gani wakati inajulikana kuna wananchi walipoteza maisha yao pasipo sababu za maana.Ikiwa CDM kweli ina mkanda ni kwanini mpaka leo bado imeukali inasubiri nini kwaajili ya manufaa ya nani au ndio mtaji wake mwaka 2015 ?.Vipi waliopoteza maisha au baada ya kuzikwa na kupiga mapicha za mazishi ndio basi.

CDM iache kucheza na maisha ya watanzania kama kweli inataka maandamano lazima watueleze wananchi walipoteza maisha wamefanyiwa nini ?.Tunajua upande wa serekali imefanya nini kwa makamanda wa mikoa yote yalipofanyika mauaji wengi wamepandishwa vyeo kwa kazi nzuri na njema ya kusimamia mauaji ya wananchi upande wa CDM watuambie familia za waanga wa maandamano na mikutano yake wamewafanyia nini ?.

Naomba kuwasilisha.
 
Heshima sana wanajamvi wote.

Kwanza napenda kuwajulisha wanajamvi wote Ngongo si mwanachama wa chama chochote cha siasa Tanzania ila ni mpenzi wa siasa.Ninaposema ni mpenzi wa siasa nina maana ninapenda kushiriki,kusikiliza na kushauriana masuala yote yahusuyo siasa bila kuwa mwanachama wa chama cha siasa.Kwahiyo unapochangia mjadala huu ni vyema ukijikita zaidi katika hoja.

Ni jambo lililo wazi Tanzania inapita katika kipindi kigumu sana tangu kuhasisiwa kwa taifa hili.Vikao vya bunge maalamu la kutunga katiba mpya vinaendelea mjini Dodoma huku baadhi ya wajumbe (UKAWA) wa bunge hilo wakisusia vikao hivyo kwasababu ambazo kwa kiasi fulani hata mimi nakubaliana nazo.Sina haja ya kueleza kwanini tumefikia hapa kwakuwa najua wengi wenu tunazijua sababu hizo ingawa kumekuwa na juhudi kubwa za kimkakati/propaganda za kupotosha kwa maksudi sababu zilizopelekea UKAWA kususia bunge la katiba.

Vyombo vya habari hasa vile vinavyomilikiwa na serekali na chama tawala vimekuwa vikipotosha ukweli kwa makusudi ya kupandikiza taswira mbaya ya UKAWA mbele ya macho ya jamii ya kitanzania hasa wale wasiopenda kuchambua mambo kwa undani.

CHADEMA sijui kama UKAWA wamo katika hii hoja ya maandamano wamekuwa wakipaza sauti za malalamiko na sasa wanataka kuanzisha maandamano nchi nzima kama sehemu ya kuonyesha kutorizishwa na jinsi mchakato wa kuandika katiba mpya unavyopaswa kwenda.Ni kweli bunge la Bwana Sitta limekosa viwango,limekosa ushirikishwa wa mawazo ya wananchi,limejivika kazi za tume ya kukusanya maoni,limekosa mjumuiko wa makundi yote (wanaCCM wametamalaki),limekataa mawazo ya wananchi,limekumbatia mawazo ya watawala.halina maana kabisaaaaa.

Ukweli ni kwamba sababu za kuandamana zipo nyingi sana lakini Ngongo wa JF anakataa maandamano kwasababu ambazo nitazieleza.

Maandamano hayajawahi kuleta mabadiliko chanya Tanzania badala yake yameacha makovu makubwa ambayo hatujawahi kuona matunda yake hata kidogo. Mji wa Arusha ni mfano mzuri wananchi waliandamana kudai uchaguzi wa haki wa meya wa Jiji la Arusha mpaka leo bado meya ni yuleyule na ikumbukwe kuna wananchi walipoteza maisha yao kwaajili ya kuhakikisha haki inapatikana.

Kwanini nakataa maandamano sasa.Nakataa maandamano kwasababu wananchi waliopoteza maisha yao kwaajili ya kuitikia wito wa maandamano mpaka leo hawajatendewa haki.Kuna wanawake leo hii ni wajane wana watoto wanashindwa kupata elimu,afya,lishe stahiki kwakuwa hawana Baba wa kuwatunza.CDM kama chama mpaka leo hawajachukua hatua za kisheria kuhakikisha walioshiriki kutoa uhai wa raia wasiokuwa na silaha wanafikishwa mahakamani,sijasikia wanasheria wa CDM wakisubutu kuanzisha mchakato wa kuishitaki serekali ICC kwa mauaji ya raia.

CDM ilidai ina mkanda wa watu walioshiriki kurusha bomu uwanja wa Soweto Arusha,tena walidai polisi walishiriki kuhakikisha mrusha bomu hakamatwi na raia kwa kurusha risasi ili kumkinga asikamatwe.Siju huo mkanda umewekwa kwaajili gani wakati inajulikana kuna wananchi walipoteza maisha yao pasipo sababu za maana.Ikiwa CDM kweli ina mkanda ni kwanini mpaka leo bado imeukali inasubiri nini kwaajili ya manufaa ya nani au ndio mtaji wake mwaka 2015 ?.Vipi waliopoteza maisha au baada ya kuzikwa na kupiga mapicha za mazishi ndio basi.

CDM iache kucheza na maisha ya watanzania kama kweli inataka maandamano lazima watueleze wananchi walipoteza maisha wamefanyiwa nini ?.Tunajua upande wa serekali imefanya nini kwa makamanda wa mikoa yote yalipofanyika mauaji wengi wamepandishwa vyeo kwa kazi nzuri na njema ya kusimamia mauaji ya wananchi upande wa CDM watuambie familia za waanga wa maandamano na mikutano yake wamewafanyia nini ?.

Naomba kuwasilisha.


Mwenye busara na utashi amekuelewa sana ila mpumbavu hajakuelewa mkuu
 
Back
Top Bottom