Mkuu Ngongo mbona hukuwaambia BMK waache kuchezea pesa za walala hoi??
Ngongo uko sahihi lakini pia hawa CHADEMA wanapata upinzani mkubwa sana...Unakumbuka Operatioy ya M4C ilisitishwa baada ya Serikali na jeshi la polisi kuwa na mkakati maalum wa kuua katika mikutano ya CHADEMA...Usidhani kuwa hawajui...ila wanajitahidi kuwa kwenye defensive side mara nyingi na Offensive mara chache...mkuu....Katika mapambano haya najua maumivu ni makubwa sana...But muda huu sio wa kukata tamaa........One day yes mkuu...Ila kitu kimoja nakuhakikishia kama kuna mmoja kati yao viongozi wa CHADEMA hana nia ya dhati katika struggle hii...Daima damu ya waliofariki itamlilia...CDM ina damu za watu mkuu
Mkuu Freeland wanahabari wameanzisha tunzo ya kumbukumbu ya Daud Mwangosi hata hili limekuwa jambo gumu kufanywa na CDM ?.CDM ina wanasheria wengi ambao wako tayari kwenda mahakamani kutetea wabunge wa CDM lakini wanasheria hao hao wameshindwa kutumia taaluma yao kupigania haki za familia za marehemu waliouwawa katika mikutano na maandamano yao.Nakumbuka familia ya marehemu Lt Gen Kombe ilidai fidia serekali ni kwanini jambo hili halifanyiki kwa wanafamilia wote waliopoteza ndugu zao katika mikutano na maandamano au tukisha weka bendera katika majeneza ndio basi ?.
![]()
Ngongo,
..hawa wanapimana misuli.
..sasa upande ule utakaovunjika moyo ndiyo utashindwa.
..kama CDM wanataka mabadiliko basi wanatakiwa waandamane mpaka polisi/ccm wakate tamaa na kuamua kukubali yaishe.
..bila hilo kutokea basi usitegemee mabadiliko yoyote yale ya maana nchi hii.
NB:
..kwasababu wahanga wa utawala mbovu na wakikatili wa CCM ni wananchi hohe-hahe basi tabaka hilohilo ndilo linalopaswa kuwa mstari wa mbele and sometimes even pay the ultimate price ktk mapambano dhidi ya dhuluma.
Chadema wanakera sana wanapoamua kurudi kwenye mazungumzo na watu wasioaminika .....bora yatangazwe maandamano ambayo hayajapata kushuhudiwa ili tuone matunda ya mabadiliko na si kusitisha kwa ahadi za peremende .....
Isitishe maandamano kwa faida ya nani? Mbona kila mmoja kaingia upepo? Fedha inayoliwa Dodoma ni nyingi sana .....haivumiliki......
..askari aliyemlipua Mwangosi amefikishwa mahakamani na kesi yake inaendelea.
..suala la familia ya Mwangosi kudai fidia linategemea hukumu itakayotolewa kwenye kesi hiyo.
..pia kuna hatari kwamba ikiwa CDM watakuwa mstari wa mbele kudai fidia kwa niaba ya familia ya Mwangosi, basi CCM na serikali wataamua kesi hiyo kisiasa.
..mwisho, hivi kwanini tunawalaumu CDM ktk suala hili na siyo Raisi, serikali, na CCM? Raisi Kikwete amempandisha cheo kamanda aliyekuwa incharge siku Mwangosi ameuawa. What does that tell you?
Freeland, Pasco, Manyerere Jackton
Every revolution has sacrifices; hakuna mapinduzi yasiyokuwa na wahanga! mapinduzi yoyote dunia yamefanikishwa na watu jasiri wenye maonu mapana na mioyo mikubwa sio wenye roho biskuti kama wewe! siasa za hisia za kusikilizia kwa mbali unazofanya wewe hazitufai; kaa pembeni wanaume watende kazi utadandia bogi huko twendako. Bs.
Mkuu JokaKuu kitendo cha viongozi wa upinzani kwenda Ikulu kunywa juisi na mtu wanayejua dhahiri ndiye aliyetoa amri ya askari kutupa mabomu hovyo,kupiga risasi wananchi wasiokuwa na silaha ndio kimenifanya nianze kuwatilia shaka hawa viongozi wetu wa upinzani wanaodai kwenda kunywa juisi Ikulu. Mimi siwaelewi kabisa hawa mikakati madhubuti,hawana lolote.Hoja ya mauaji ya wananchi ingesimamiwa vizuri hakika leo hii hakuna polisi angekubali kutumiwa hata kidogo.Tazama mifano ya maRPC waliosimamia zoezi la mauaji leo wako wapi wengine kidogo wangeukwaa uIGP.
..sasa hebu nikuulize: mkakati wa Raisi, na CCM, unaelewa? Je, umeridhika nao?
..halafu wakati mwingine ni wa-Tz wenyewe tunaowashinikiza Ukawa wakazungumze Ikulu, halafu Raisi asipotekeleza yale waliyokubaliana tunawalaumu Ukawa.
..hivi kwa akili za kawaida, bunge la katiba lilipaswa kuendelea baada ya makubaliano yaliyofikiwa kati ya vyama vya upinzani na Raisi? Kwanini hatumlaumu Samuel Sitta kwa kiburi anachokionyesha kwa Raisi? Kwanini hatumlaumu Raisi kwa kumdekeza Samuel Sitta? Badala yake kwanini tunawalaumu Ukawa?
cc MTAZAMO