Sangarara
JF-Expert Member
- Sep 29, 2011
- 13,100
- 5,649
Mtanisamehe kwa kukosa maneno fasaha ya Kiswahili kutuma ujumbe uliobebeka katika kichwa cha habari, Lakini nadhani tafsiri ya kuungaunga ni kwamba CHADEMA sio MALAIKA ila ni afadhali kuliko CCM. Mtanisamehe kwa upungufu nilionao katika Lugha ya Taifa, nadhani ujumbe umewafikia.
Nijielekeze kwenye hoja ya msingi, Ghafla, katika namna ambayo mfuatiliaji yeyote wa maswala ya siasa angeitegemea kumetokea Watanzania wenzetu wengi waliojikita hasa hapa JF katika kukipaka matope Chama cha Democrasia na Maendeleo bila shaka lengo kuu likiwa ni ama kuonyesha kwamba hata chenyewe ni chama kichafu kama chao ama Viongozi wake nao ni wachafu kama wao.
Japokuwa hii hoja ni pana sana, naomba niifupishe kwa kuweka wazi kwamba, Watanzania tuna options mbili tu, ama kuichagua CCM ama kuichagua CHADEMA, na katika hili niseme wazi kabisa kwamba vyama vingine vyote ni hovyo hovyo kama tulivyozoa kumsikia MR BEN a.k.a undertaker majukwaani siku za karibuni.
Viongozi wa CCM na CHADEMA na mfumo mzima wa uendeshaji wa vyama hivi viwili sio PERFECT, wao kama binaadamu wanamapungufu yao na vyama hivi viwili kama matokeo ya Fikra za Mwanaadamu sio PERFECT. kuna mapungufu mengi tu na ukichukulia mfumo mzima unaoitwa wa kidemocrasia ulivyokuwa mfumo wenye misingi mibovu kuliko mifumo mingine haishangazi kabisa matokeo ya mfumo huo kuwa mabovu kwa maana ya vyote viwili, vyama shiriki vya democrasia na wanasiasa wenyewe.
Kwa hapa tulipofikia watanzania, hakuna namna tunaweza tukasema tuutupilie mbali mfumo wa kidemocrasia ili tuachane na vyama hivi wala wanasiasa hawa, bahati nzuri Jamii kubwa ya Watanzania imeonyesha kuwa na imani na mfumo huu, hivyo bila shaka tutafaidika na labda tunafaidika nao.
Misingi ya mfumo huu ni kuchagua mwanasiasa huyu na kuachana na mwanasiasa huyu au kuchagua chama hiki na kuachana na chama hiki, Watanzania tuko kwenye mchakato wa kuchagua na ni lazima tuchague, HATA VYAMA HIVI VIKIENDELEA NA MIKAKATI YA KUCHAFUANA NI NGUMU SANA KUICHAGUA CCM. ZAIDI WANACHOKIFANYA CCM NI KAMA VILE KUFURUGA HALI YA HEWA ILI WATU WASHINDWE KUCHAGUA. HAIWEZEKANI.
LAZIMA TUCHAGUE
Nijielekeze kwenye hoja ya msingi, Ghafla, katika namna ambayo mfuatiliaji yeyote wa maswala ya siasa angeitegemea kumetokea Watanzania wenzetu wengi waliojikita hasa hapa JF katika kukipaka matope Chama cha Democrasia na Maendeleo bila shaka lengo kuu likiwa ni ama kuonyesha kwamba hata chenyewe ni chama kichafu kama chao ama Viongozi wake nao ni wachafu kama wao.
Japokuwa hii hoja ni pana sana, naomba niifupishe kwa kuweka wazi kwamba, Watanzania tuna options mbili tu, ama kuichagua CCM ama kuichagua CHADEMA, na katika hili niseme wazi kabisa kwamba vyama vingine vyote ni hovyo hovyo kama tulivyozoa kumsikia MR BEN a.k.a undertaker majukwaani siku za karibuni.
Viongozi wa CCM na CHADEMA na mfumo mzima wa uendeshaji wa vyama hivi viwili sio PERFECT, wao kama binaadamu wanamapungufu yao na vyama hivi viwili kama matokeo ya Fikra za Mwanaadamu sio PERFECT. kuna mapungufu mengi tu na ukichukulia mfumo mzima unaoitwa wa kidemocrasia ulivyokuwa mfumo wenye misingi mibovu kuliko mifumo mingine haishangazi kabisa matokeo ya mfumo huo kuwa mabovu kwa maana ya vyote viwili, vyama shiriki vya democrasia na wanasiasa wenyewe.
Kwa hapa tulipofikia watanzania, hakuna namna tunaweza tukasema tuutupilie mbali mfumo wa kidemocrasia ili tuachane na vyama hivi wala wanasiasa hawa, bahati nzuri Jamii kubwa ya Watanzania imeonyesha kuwa na imani na mfumo huu, hivyo bila shaka tutafaidika na labda tunafaidika nao.
Misingi ya mfumo huu ni kuchagua mwanasiasa huyu na kuachana na mwanasiasa huyu au kuchagua chama hiki na kuachana na chama hiki, Watanzania tuko kwenye mchakato wa kuchagua na ni lazima tuchague, HATA VYAMA HIVI VIKIENDELEA NA MIKAKATI YA KUCHAFUANA NI NGUMU SANA KUICHAGUA CCM. ZAIDI WANACHOKIFANYA CCM NI KAMA VILE KUFURUGA HALI YA HEWA ILI WATU WASHINDWE KUCHAGUA. HAIWEZEKANI.
LAZIMA TUCHAGUE