Kwa wasiotumia akili wataona umenena lkn ukweli ni kwamba wanawezaje kuliangamiza taifa wakati sio chama tawala? Chama tawala kinafanya nini mpaka taifa linaangalia wenyewe wanaangalia tuu?, CCM ndio wanaoongoza sasa iweje wengine CDM waangamize wao waangalie na kushangilia? mpaka hapo umejichanganya mwenyewe WANAO ANGAMIZA NI CCM:
Kwa jinsi CDM wanavyobambikiwa kesi ni wazi kabisa wakifanya makosa ndio kaburi lao. hiyo tu inaonyesha kuwa wako makini. kama wangekuwa wanauza unga wangeshafia jela siku nyingi maana wasingehangaika na kesi za kubambikia.
Ukiona mtu ambaye wewe unamdharau halafu anahesimiwa na kupendwa na watu zaidi yako basi ujue wewe Thamani yako ni ndogo kuliko ya huyo unayemdharau. WACHENI CDM ipendwe, iheshimiwe na kuthaminiwa na watu hata kama nyie CCM hamuipenda kinawauma nini?
MEA MTWARO! Hongera sana kwa kuisemea haki, Tuache ushabiki wa kinazi bali uzalendo utawale
Mkuu Bakari, hapo kuna kitu usichokielewa juu ya hoja zitolewazona maProCHADEMA! Kama ingekuwa huwa wanapinga kila kitu kama unavyojadiri, hebu angalia kwenye thread ya mama Ana Tibaijuka! Tatizo si dini, kabila, kanda au chochote ulichoandika kwenye uzi wako, tatizo ni je huyo mtu anaishi kama anavyo hubiri? Ungewauliza why critisise him na siyo, Mwakyembe, Tibaijuka, Kagasheki! Ungepata jibu, watu wana data za kila mtu hapa! Ukianza kusema tuvae nguo wakati wewe uko uchi watakuhoji accordingly! Umekosa upeo wa kina katika kujenga hoja yako!Kwa kawaida watu makini hawaongozwi na Ubinafsi katika kujadili masuala mbalimbali muhimu ya kitaifa. Hawasukumwi na Umimi, ukabila, ukanda na Udini katika kutoa michango na maoni katika ujenzi wa Taifa, hali ipo tofauti kwa Waumini wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambao wanajitambulisha kwa Udini,ukabila,ukanda,Umimi na Ubinafsi katika kujadili mambo nyeti ya Kitaifa.
Aidha Watu wanaojipofisha jicho la kulia na kuacha la kushoto kuangalia mambo mabaya tu hawawezi kuitwa 'Great Thinkers' kama wanavyojidanganya Wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Mitandao ya Kijamii.
Naam! Ndugu wapendwa, kabla ya kusogeza Mguu mbele, naomba kusema kuwa, ni Ibara ya 18(a)ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiyo inayonipa haki ya kuandika Makala hii kwani Ibara hiyo inatoa Uhuru wa Mtu kutoa Mawazo na Fikra zake kuhusu Nchi yake
Ndiyo! nimeamua kuandika Makala hii kutokana na maoni na michango mbalimbali iliyotolewa na Waumini wa CHADEMA katika Mtandao wa Jamiiforums ambapo walikuwa wakichangia Makala iliyoandikwa na Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),Dk. Khamisi Kigwangalla. Michango na maoni hayo ni Ushahidi tosha kwamba CHADEMA inawahujumu Watanzania na Taifa kwa Ujumla.
Siku ya Alhamisi ya tarehe 30,May 2013, Mbunge wa Jimbo la Nzega,Mkoani Tabora, Dk. Kigwangwalla aliandika Makala katika Mtandao wa Jamiiforums. Katika Makala hiyo Dk. Kigwangalla alieleza Matatizo mbalimbali yanayolikabili Taifa letu huku akipendekeza njia mbadala kuyakabili Matatizo hayo.Kubwa zaidi Dk. Kigwangalla aliwataka Watanzania kubadilika Kifikra huku akisema kuwa,"Uoga wa kubalika ni sumu kwa Wapenda Maendeleo". Ngoja niendelee kumnukuu Mbunge huyo ili kwayo Maoni yake yaweze kulinganishwa na kile kilichochangiwa na 'Wanamagwanda'.
"Napenda kuona Watanzania, Sote kwa pamoja tukibadilika kifikra. Tuanze kuwa Wabunifu zaidi, wenye Uthubutu,Wachapa kazi, Waaminifu, kuweka mbele Uzalendo kwa faida ya wote badala ya Umimi zaidi kwa faida yangu. Napenda kuona Watanzania Wenzangu tukizaliwa Upya leo na kuanza nguvu mpya leo ya kuleta mabadiliko ya kifikra na Kiutendaji. Tuondoke kwenye Umbumbumbu wa kuamini kuwa,kila kitu kitaletwa na Serikali. Tuanze kuamini kuwa, tunaweza kubadilisha maisha yetu kwa kuchukua hatua sahihi katika maisha yetu binafsi na katika jamii yetu. Tuanze kuamini vingine kuwa, tunaweza kuamua kuibalisha Nchi yetu sisi wenyewe na kutoka hapa tulipo leo na kuingia Dunia nyingine kabisa kiuchumi na kijamii".
Bila shaka Mawazo yaliyoandikwa katika Makala hiyo ni ya kupongezwa,kuungwa mkono,kuhamasishwa na kufanfanyiwa kazi kwa Watu wenye Ujenzi wa Fikra kwani Mwandishi wa Makala hiyo ameonekana kuandika kwa hisia kali na hivyo kudhihirisha kuwa, ameguswa na kukerwa na matatizo yanayolikabili Taifa letu. Hongera sana Kigwangalla.
Lakini tazama! hali inakuwa tofauti kwa Wafuasi wa CHADEMA,baada ya kuunga mkono,kuhamasisha na kufanyia kazi mawazo hayo, wametumia Wino wao kubeza na kutweza mawazo hayo kwa kuwa tu yamesemwa na Mtu wa CCM. Yangesemwa na Kiongozi wa CHADEMA yangekuwa lulu. Huu ni Uzandiki wa Fikra unaoweza kuliangamiza Taifa letu kwa Misingi ya Uchama, Ubinafsi na Umimi na kwamba vitendo hivi vya hovyo hufanywa na Wasomi Uchwara na Wanasiasa Makapi wasiolitakia Taifa mema na haya ni matokeo ya kushindwa kujenga hoja na kutumia hoja za nguvu kuyafanya mambo yao yakubalike.
Aidha, ni bora kuwasilisha kwenu baadhi ya michango na maoni ya baadhi ya Wanamtandao huo wa Jamiiforums ambao mara nyingi wanajitambulisha na kujigamba kwa Uchama badala ya Utaifa kama ifuatavyo:
Mchangiaji aliyejitambulisha kwa jina la Steven Robert Masatu amesema "Huwezi kuhubiri Fikra mbadala ilihali wewe upo kwenye fikra mgando. Mkuu toka kwanza huko uliko( CCM)". Evi ni kweli kwa mfano si sahihi kwa mnyonge kuwatetea wanyoge wenzake kwa kuwa tu naye ni Mnyoge? kama hivyo ndivyo basi Mwalimu Nyerere asingeliwatetea Watanzania maana alikuwa Mnyonge, kama si upotoshaji nini?.Ingawa hata hivyo Kigwanga haonekani kuwa na Fikra mgando maana aliyoyanena hapo hunenwa na wachache tu.
Nderingosha kama anavyojitambulisha katika Mtandao huo amesema "Hizi Makala ungekuwa unawaandikia Wabunge wenzako wa CCM maana wao ndio wanatakiwa kubadilika kifikra na siyo Wananchi". Huu ni ukweli au kuwahujumu Watanzania?
Vilevi Meningits amesema kuwa "Badiliko la kwanza ni kuitoa CCM mwaka 2015" huku akifuatiwa na mwenzake anayejitambulisha kwa jina la Verified na kusema kuwa, "Tatizo ni CCM" hawa ndio wasomi wetu wanaoyaangalia mambo kwa jicho moja tena la kushoto. Ewe Mwenyezi epusha janga hili katika Taifa letu.
Hivyo,Wachangiaji hawa wanne ni wachache kati ya Wengi wanaojitambulisha kwa Uchadema katika mtandao huo wa kijamii ambao wanaonekana kukifia chama kuliko Taifa, kupinga 'Constructive Ideas' kwa sababu tu yamesemwa na Mtu wa CCM na kuyaangalia mambo kwa jicho la kushoto huku wakiziba la kulia wasione mazuri. Huku ni kulitafuna Taifa kwa Misingi ya Uchama, Umimi na Ubinafsi.
Nisingependa kumaliza makala hii pasi na kuwashauri viongozi wa CHADEMA na Wafuasi wake kuwa, wawe tayari kulifia Taifa kuliko Chama, Wawaunge mkono viongozi wetu pale wanapokuja na mikakati ya kuljenga Taifa,kuwapa moyo viongozi wetu kwa mawazo yao pale yanapoonekana ni ya tija kuliko kuwabeza, tweza na kuwakatisha tamaa kwani kufanya hivyo kwaweza kupelekea viongozi wetu kujihusisha na malumbano badala ya kusisimamia shughuli za kimaendeleo na hatimaye kulipeleka Taifa kwenye Mdomo wa Mamba. Kwa faida ya nani?
Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
Ninaitwa BAKARI MADAYA (Mwanatunduru).
Ninapatikana simu: 0789357823 au barua pepe madayabakar@hotmail.com
hahaha... nae anataka ubunge?
Kama CHADEMA ikiendelea na utaratibu wa kupokea tu watu wa aina hiyo na kuwafanya makamanda wao, basi nadiriki kusema bado CHADEMA haipo serious.
Kwani huku CCM kuna utaratibu maalumu wa kupata wanachama, ni ndio maana tuna 'wafia' chama wengi kwa taratibu tulizo jiwekea.
CHADEMA jifunzeni kutoka kwa baba.
Kwa kawaida watu makini hawaongozwi na Ubinafsi katika kujadili masuala mbalimbali muhimu ya kitaifa. Hawasukumwi na Umimi, ukabila, ukanda na Udini katika kutoa michango na maoni katika ujenzi wa Taifa, hali ipo tofauti kwa Waumini wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambao wanajitambulisha kwa Udini,ukabila,ukanda,Umimi na Ubinafsi katika kujadili mambo nyeti ya Kitaifa.
Aidha Watu wanaojipofisha jicho la kulia na kuacha la kushoto kuangalia mambo mabaya tu hawawezi kuitwa 'Great Thinkers' kama wanavyojidanganya Wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Mitandao ya Kijamii.
Naam! Ndugu wapendwa, kabla ya kusogeza Mguu mbele, naomba kusema kuwa, ni Ibara ya 18(a)ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiyo inayonipa haki ya kuandika Makala hii kwani Ibara hiyo inatoa Uhuru wa Mtu kutoa Mawazo na Fikra zake kuhusu Nchi yake
Ndiyo! nimeamua kuandika Makala hii kutokana na maoni na michango mbalimbali iliyotolewa na Waumini wa CHADEMA katika Mtandao wa Jamiiforums ambapo walikuwa wakichangia Makala iliyoandikwa na Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),Dk. Khamisi Kigwangalla. Michango na maoni hayo ni Ushahidi tosha kwamba CHADEMA inawahujumu Watanzania na Taifa kwa Ujumla.
Siku ya Alhamisi ya tarehe 30,May 2013, Mbunge wa Jimbo la Nzega,Mkoani Tabora, Dk. Kigwangwalla aliandika Makala katika Mtandao wa Jamiiforums. Katika Makala hiyo Dk. Kigwangalla alieleza Matatizo mbalimbali yanayolikabili Taifa letu huku akipendekeza njia mbadala kuyakabili Matatizo hayo.Kubwa zaidi Dk. Kigwangalla aliwataka Watanzania kubadilika Kifikra huku akisema kuwa,"Uoga wa kubalika ni sumu kwa Wapenda Maendeleo". Ngoja niendelee kumnukuu Mbunge huyo ili kwayo Maoni yake yaweze kulinganishwa na kile kilichochangiwa na 'Wanamagwanda'.
"Napenda kuona Watanzania, Sote kwa pamoja tukibadilika kifikra. Tuanze kuwa Wabunifu zaidi, wenye Uthubutu,Wachapa kazi, Waaminifu, kuweka mbele Uzalendo kwa faida ya wote badala ya Umimi zaidi kwa faida yangu. Napenda kuona Watanzania Wenzangu tukizaliwa Upya leo na kuanza nguvu mpya leo ya kuleta mabadiliko ya kifikra na Kiutendaji. Tuondoke kwenye Umbumbumbu wa kuamini kuwa,kila kitu kitaletwa na Serikali. Tuanze kuamini kuwa, tunaweza kubadilisha maisha yetu kwa kuchukua hatua sahihi katika maisha yetu binafsi na katika jamii yetu. Tuanze kuamini vingine kuwa, tunaweza kuamua kuibalisha Nchi yetu sisi wenyewe na kutoka hapa tulipo leo na kuingia Dunia nyingine kabisa kiuchumi na kijamii".
Bila shaka Mawazo yaliyoandikwa katika Makala hiyo ni ya kupongezwa,kuungwa mkono,kuhamasishwa na kufanfanyiwa kazi kwa Watu wenye Ujenzi wa Fikra kwani Mwandishi wa Makala hiyo ameonekana kuandika kwa hisia kali na hivyo kudhihirisha kuwa, ameguswa na kukerwa na matatizo yanayolikabili Taifa letu. Hongera sana Kigwangalla.
Lakini tazama! hali inakuwa tofauti kwa Wafuasi wa CHADEMA,baada ya kuunga mkono,kuhamasisha na kufanyia kazi mawazo hayo, wametumia Wino wao kubeza na kutweza mawazo hayo kwa kuwa tu yamesemwa na Mtu wa CCM. Yangesemwa na Kiongozi wa CHADEMA yangekuwa lulu. Huu ni Uzandiki wa Fikra unaoweza kuliangamiza Taifa letu kwa Misingi ya Uchama, Ubinafsi na Umimi na kwamba vitendo hivi vya hovyo hufanywa na Wasomi Uchwara na Wanasiasa Makapi wasiolitakia Taifa mema na haya ni matokeo ya kushindwa kujenga hoja na kutumia hoja za nguvu kuyafanya mambo yao yakubalike.
Aidha, ni bora kuwasilisha kwenu baadhi ya michango na maoni ya baadhi ya Wanamtandao huo wa Jamiiforums ambao mara nyingi wanajitambulisha na kujigamba kwa Uchama badala ya Utaifa kama ifuatavyo:
Mchangiaji aliyejitambulisha kwa jina la Steven Robert Masatu amesema "Huwezi kuhubiri Fikra mbadala ilihali wewe upo kwenye fikra mgando. Mkuu toka kwanza huko uliko( CCM)". Evi ni kweli kwa mfano si sahihi kwa mnyonge kuwatetea wanyoge wenzake kwa kuwa tu naye ni Mnyoge? kama hivyo ndivyo basi Mwalimu Nyerere asingeliwatetea Watanzania maana alikuwa Mnyonge, kama si upotoshaji nini?.Ingawa hata hivyo Kigwanga haonekani kuwa na Fikra mgando maana aliyoyanena hapo hunenwa na wachache tu.
Nderingosha kama anavyojitambulisha katika Mtandao huo amesema "Hizi Makala ungekuwa unawaandikia Wabunge wenzako wa CCM maana wao ndio wanatakiwa kubadilika kifikra na siyo Wananchi". Huu ni ukweli au kuwahujumu Watanzania?
Vilevi Meningits amesema kuwa "Badiliko la kwanza ni kuitoa CCM mwaka 2015" huku akifuatiwa na mwenzake anayejitambulisha kwa jina la Verified na kusema kuwa, "Tatizo ni CCM" hawa ndio wasomi wetu wanaoyaangalia mambo kwa jicho moja tena la kushoto. Ewe Mwenyezi epusha janga hili katika Taifa letu.
Hivyo,Wachangiaji hawa wanne ni wachache kati ya Wengi wanaojitambulisha kwa Uchadema katika mtandao huo wa kijamii ambao wanaonekana kukifia chama kuliko Taifa, kupinga 'Constructive Ideas' kwa sababu tu yamesemwa na Mtu wa CCM na kuyaangalia mambo kwa jicho la kushoto huku wakiziba la kulia wasione mazuri. Huku ni kulitafuna Taifa kwa Misingi ya Uchama, Umimi na Ubinafsi.
Nisingependa kumaliza makala hii pasi na kuwashauri viongozi wa CHADEMA na Wafuasi wake kuwa, wawe tayari kulifia Taifa kuliko Chama, Wawaunge mkono viongozi wetu pale wanapokuja na mikakati ya kuljenga Taifa,kuwapa moyo viongozi wetu kwa mawazo yao pale yanapoonekana ni ya tija kuliko kuwabeza, tweza na kuwakatisha tamaa kwani kufanya hivyo kwaweza kupelekea viongozi wetu kujihusisha na malumbano badala ya kusisimamia shughuli za kimaendeleo na hatimaye kulipeleka Taifa kwenye Mdomo wa Mamba. Kwa faida ya nani?
Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
Ninaitwa BAKARI MADAYA (Mwanatunduru).
Ninapatikana simu: 0789357823 au barua pepe madayabakar@hotmail.com
Kila mnapozungumzia udini,ukabila na ukanda mnanikumbusha ile video ya Lipumba(CUF) akikiri kumsaidia Kikwete(CCM)kuupata uraisi!Kweli Chadema imewashika pabaya!
Makala murua na yenye tija humu jamvini!
Ongera mkuu kwa kufunguka.