Amavubi
JF-Expert Member
- Dec 9, 2010
- 30,156
- 13,267
Niko hapa Kilombero kwa muda kwani ni msimu wa kilimo;
Nimefanya kaudadisi kadogo baada ya kuona kwa asilimia kubwa toka Mikumi hadi Chita (huko mbele sikuendelea) kuna bendera nyingi pembezoni mwa Barabara ambazo ni za CHADEMA na kugundua kwamba hiki chama kinakubalika sana huku (mm sio mfuasi wake) na kwamba zaidi ya yote idadi kubwa ya madiwani wanatoka chama hiki, hapa Chita nilizungumza na wadau kadhaa wakaniambia moja ya sababu za kuchagua CHADEMA ni kwamba wanakasirika sana umeme unatoka jirani na kwao (Kihasi) halafu unakwenda viunga vingine vya mbali ilihali wao wanawasha vibatari.......sababu nyingine ni kwamba wanaisi wamewekwa pembezoni na rasilimali muhimu za nchi na hasa ubovu wa barabara ambao hata hakuna dalili ya kutengewa fungu japokuwa wao ni wazalishaji wakubwa wa mchele
Watu wa Mngeta na Mbingu wanahasira ya umeme kwenda kwa mwekezaji wa Kilombero Plantation Limited (KPL) ilihali wao wakiambulia jenereta la mhisani mwanakijiji mwenzao
Nimewauliza vipi kuhusu sakata la Zitto linawagusaje na mustakabali wao chamani wakanijibu Zitto atapita na mambo yake lakn CHADEMA itaendelea kuwepo hIvyo wanakaza buti na Chama chao hicho.
Yeyote aliyebahatika/atakayebahatika kutembelea maeneo haya anaweza kuthibitisha haya
Besides; Simba inakubalika sana huku sababu wanachukia rangi ya kijani na njano na ninafanya mpango wa kufungua TAWI
cc: Makoye Matale, Ulimakafu, Mandieta ..................
Nimefanya kaudadisi kadogo baada ya kuona kwa asilimia kubwa toka Mikumi hadi Chita (huko mbele sikuendelea) kuna bendera nyingi pembezoni mwa Barabara ambazo ni za CHADEMA na kugundua kwamba hiki chama kinakubalika sana huku (mm sio mfuasi wake) na kwamba zaidi ya yote idadi kubwa ya madiwani wanatoka chama hiki, hapa Chita nilizungumza na wadau kadhaa wakaniambia moja ya sababu za kuchagua CHADEMA ni kwamba wanakasirika sana umeme unatoka jirani na kwao (Kihasi) halafu unakwenda viunga vingine vya mbali ilihali wao wanawasha vibatari.......sababu nyingine ni kwamba wanaisi wamewekwa pembezoni na rasilimali muhimu za nchi na hasa ubovu wa barabara ambao hata hakuna dalili ya kutengewa fungu japokuwa wao ni wazalishaji wakubwa wa mchele
Watu wa Mngeta na Mbingu wanahasira ya umeme kwenda kwa mwekezaji wa Kilombero Plantation Limited (KPL) ilihali wao wakiambulia jenereta la mhisani mwanakijiji mwenzao
Nimewauliza vipi kuhusu sakata la Zitto linawagusaje na mustakabali wao chamani wakanijibu Zitto atapita na mambo yake lakn CHADEMA itaendelea kuwepo hIvyo wanakaza buti na Chama chao hicho.
Yeyote aliyebahatika/atakayebahatika kutembelea maeneo haya anaweza kuthibitisha haya
Besides; Simba inakubalika sana huku sababu wanachukia rangi ya kijani na njano na ninafanya mpango wa kufungua TAWI
cc: Makoye Matale, Ulimakafu, Mandieta ..................