mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,286
- 6,727
Kumekuwa na shutuma nyingi, kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kuhusu utendaji kazi wa Rais Magufuli na Serikali ya CCM, hadi Rais kupachikwa majina kadhaa na kutuhumiwa kuwa ni mkurupukaji.
Naomba nijielekeze kwenye dira inayo mwongoza Rais Magufuli katika utendaji kazi wake, na kumalizia na swali la msingi linalobeba kichwa cha mada yangu.
Katiba ya CCM (2005), Sehemu ya Kwanza: Jina, Imani na Madhumuni, Ibara ya 4(3) - Ujamaa na Kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru. Imani hii inaendana na moja ya misingi ya Katiba ya JMT (1977) kwamba KWA KUWA SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeaamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuri, haki, udugu na amani:
Imani hiyo inatekelezwa kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ya CCM ya Uchaguzi (2015) ili kuleta maendeleo ya kweli nchini kwa maana ya:
1) Afya na ustawi wa jamii ya watu.
2) Elimu.
3) Mishahara inayofaa.
4) Kuinuka kwa hali ya maisha na upatikanaji rahisi wa mahitaji ya lazima.
Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 inabainisha kwamba Katika miaka mitano ijayo (2015-2020), CCM ikiwa madarakani, itazielekeza Serikali zake kutumia nguvu zake zote kuendelea kupambana na changamoto kubwa nne:- 1) kuondoa umasikini; 2) kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira hasa kwa vijana; 3) kuendeleza vita dhidi ya adui rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma; na 4) kuendelea kudumisha amani, ulinzi na usalama wa maisha ya wananchi na mali zao.
Je, hayo yametimizwa na kwa kiwangi gani? Hakuna shaka kuwa kuna nuru kubwa tu kwenye tanuru la giza, ikizingatiwa vita anazoziendesha Rais dhidi ya uzembe, urasimu, uhujumu uchumi, na madawa ya kulevya, ikiwa ni pamoja na ujenzi na uboreshaji wa miundo mbinu ya usafirishaji, uchukuzi, afya, elimu na sekta ya viwanda kuongeza ajira na pato la taifa.
Swali langu la msingi: Je, imani ya CHADEMA iliyojengwa ndani ya falsafa yake ya Nguvu na Mamlaka ya Umma (The People's Power) katika kumiliki, kuendesha, kubuni, na kuendeleza maamuzi, mawazo, rasmali, uchumi na siasa ya nchi yao, inatekelezwa vipi, ili kuendana na Itikadi yake ya MRENGO WA KATI (center party)?
FIKIRI KABLA HUJAJIBU
Naomba nijielekeze kwenye dira inayo mwongoza Rais Magufuli katika utendaji kazi wake, na kumalizia na swali la msingi linalobeba kichwa cha mada yangu.
Katiba ya CCM (2005), Sehemu ya Kwanza: Jina, Imani na Madhumuni, Ibara ya 4(3) - Ujamaa na Kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru. Imani hii inaendana na moja ya misingi ya Katiba ya JMT (1977) kwamba KWA KUWA SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeaamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuri, haki, udugu na amani:
Imani hiyo inatekelezwa kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ya CCM ya Uchaguzi (2015) ili kuleta maendeleo ya kweli nchini kwa maana ya:
1) Afya na ustawi wa jamii ya watu.
2) Elimu.
3) Mishahara inayofaa.
4) Kuinuka kwa hali ya maisha na upatikanaji rahisi wa mahitaji ya lazima.
Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 inabainisha kwamba Katika miaka mitano ijayo (2015-2020), CCM ikiwa madarakani, itazielekeza Serikali zake kutumia nguvu zake zote kuendelea kupambana na changamoto kubwa nne:- 1) kuondoa umasikini; 2) kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira hasa kwa vijana; 3) kuendeleza vita dhidi ya adui rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma; na 4) kuendelea kudumisha amani, ulinzi na usalama wa maisha ya wananchi na mali zao.
Je, hayo yametimizwa na kwa kiwangi gani? Hakuna shaka kuwa kuna nuru kubwa tu kwenye tanuru la giza, ikizingatiwa vita anazoziendesha Rais dhidi ya uzembe, urasimu, uhujumu uchumi, na madawa ya kulevya, ikiwa ni pamoja na ujenzi na uboreshaji wa miundo mbinu ya usafirishaji, uchukuzi, afya, elimu na sekta ya viwanda kuongeza ajira na pato la taifa.
Swali langu la msingi: Je, imani ya CHADEMA iliyojengwa ndani ya falsafa yake ya Nguvu na Mamlaka ya Umma (The People's Power) katika kumiliki, kuendesha, kubuni, na kuendeleza maamuzi, mawazo, rasmali, uchumi na siasa ya nchi yao, inatekelezwa vipi, ili kuendana na Itikadi yake ya MRENGO WA KATI (center party)?
FIKIRI KABLA HUJAJIBU