CHADEMA inaamini nini kwa sasa?

CHADEMA inaamini nini kwa sasa?

CHADEMA kwa sasa haina dira wala mwelekeo wowote ipo tu inaishi kwa kuokoteza habari za magazetini na mitandaoni na matukio.NI kijiwe tu cha umbeya siku hizi

CCM ipo ipo tu kwa kuamini kuwa mtu mmoja ndiyo mihimili yote na anayemkosoa adhabu yake ni kupigwa risasi 32
 
Jibu maswali haya

1. Umasikini umepungua kwa kiwango gani sasa?

2. Ajira zimepungua kivipi? Tangu 2016 wahitimu wa Elimu ya Sanaa hawajaajiriwa hadi sasa

3. Mumenunua madiwani Arusha, mkapewa uthibitisho juu hiyo Rushwa baadae mkakiri kuhusika na hiyo Rushwa lakini kwa sababu ninyi ndio mnapambana na Rushwa hiyo mkaona sio Rushwa na muhusika mkamzawadia Cheo kingine zaidi alichokuwanacho, Sasa mnapambana na Rushwa ipi?

4. Utekaji, utesaji, uuaji, kutishia viongozi silaha mchana kweupe, kushambulia watu na Risasi mchana kweupe, uokotwaji wa maiti pembezoni wa fukwe ya bahari hiyo ndio Amani mnailinda kwa wananchi?
 
CCM ipo ipo tu kwa kuamini kuwa mtu mmoja ndiyo mihimili yote na anayemkosoa adhabu yake ni kupigwa risasi 32
Thibitisha madai hayo kwa ushahidi usio na shaka. Siyo neno unatumia haki yako ya kikatiba hata kuandika utumbo
 
Soma majibu yenye maandishi mekundu

Jibu maswali haya

1. Umasikini umepungua kwa kiwango gani sasa?
Usiwe mvivu wa kusoma majarida na machapisho ya BOT, TRA na TBS pamoja na majarida ya nje km The Economist, IFM, WB, nk

2. Ajira zimepungua kivipi? Tangu 2016 wahitimu wa Elimu ya Sanaa hawajaajiriwa hadi sasa
Rejea jibu langu hapo juu na kuhusu ajira ya hao wahitimu, kama wewe ni mmoja wa hao ambao hajaajiriwa, jiajiri mwenyewe kwa kuwa mtunzi wa riwaya za filamu au maigizo au jiunge na vikundi vilivyopo vya sanaa. Tumia kichwa chako.

3. Mumenunua madiwani Arusha, mkapewa uthibitisho juu hiyo Rushwa baadae mkakiri kuhusika na hiyo Rushwa lakini kwa sababu ninyi ndio mnapambana na Rushwa hiyo mkaona sio Rushwa na muhusika mkamzawadia Cheo kingine zaidi alichokuwanacho, Sasa mnapambana na Rushwa ipi?
Kama viongozi wa upinzani wanaweza kununulika basi upinzani haufai kuongoza nchi hii!

4. Utekaji, utesaji, uuaji, kutishia viongozi silaha mchana kweupe, kushambulia watu na Risasi mchana kweupe, uokotwaji wa maiti pembezoni wa fukwe ya bahari hiyo ndio Amani mnailinda kwa wananchi?
Weka ushahidi usio na shaka, ueleweke
 
Soma majibu yenye maandishi mekundu
1. Unataka tujibizane kwa hoja, lakini hoja zako zipo kabatini, zilete hapa tuzione, unafikiri wakati wa kuomba kura utaenda kumwambia mwananchi nenda kasome jarida ili upate jibu la swali lako? Sishangai kwa sababu mtaji wenu ni hao ambao hawawezi kusoma hivyo vitu.

2. Mlituambia mtatupa ajiri hamkutuambia tukiwapa kura tutajiajiri.

3. Haujajibu swali
Narudia.

Mnapambana na Rushwa ipi? Ambayo ya akina Mnyeti sio Rushwa

4. Roma mkatoliki, Nape Nnauye, Tundu Lissu, Maiti 7 coco beach
 
1. Unataka tujibizane kwa hoja, lakini hoja zako zipo kabatini, zilete hapa tuzione, unafikiri wakati wa kuomba kura utaenda kumwambia mwananchi nenda kasome jarida ili upate jibu la swali lako? Sishangai kwa sababu mtaji wenu ni hao ambao hawawezi kusoma hivyo vitu.

2. Mlituambia mtatupa ajiri hamkutuambia tukiwapa kura tutajiajiri.

3. Haujajibu swali
Narudia.

Mnapambana na Rushwa ipi? Ambayo ya akina Mnyeti sio Rushwa

4. Roma mkatoliki, Nape Nnauye, Tundu Lissu, Maiti 7 coco beach

Mtaishia kutupa lawama za hisia, uwongo, uzushi na kukata tamaa, ati Mlituambia mtatupa ajiri hamkutuambia tukiwapa kura tutajiajiri.

Kama ubongo wako unaishi kiutegemezi huwezi kuyaona mabadiliko ya kijamii, kisiasa, kiuchumi na kimaendeleo yakiendelea kufanyika.

Upinzani utakapo zinduka ni mwaka 2025 wa Tanzania mpya. Kwa sasa hivi endeleeni na hizo siasa majitaka za mitandaoni nyuma ya 'keyboard' na 'ID' feki. Unaonesha kwamba hujui kinachoendelea katika nchi yako. Kwa kuwa hujui kama hujui, nikusamehe tu.
 
inaamini kwa miaka kumi tutakuwa tunavaa viraka kama enzi za mwalimu na nchi haina kichwa kwa sasa
Walizoea kuishi ki pedeshee sasa mirija imekatwa wanataka uhiru ili waiunge tena waendelee na maisha ya ukwasi
 
Mtaishia kutupa lawama za hisia, uwongo, uzushi na kukata tamaa, ati Mlituambia mtatupa ajiri hamkutuambia tukiwapa kura tutajiajiri.

Kama ubongo wako unaishi kiutegemezi huwezi kuyaona mabadiliko ya kijamii, kisiasa, kiuchumi na kimaendeleo yakiendelea kufanyika.

Upinzani utakapo zinduka ni mwaka 2025 wa Tanzania mpya. Kwa sasa hivi endeleeni na hizo siasa majitaka za mitandaoni nyuma ya 'keyboard' na 'ID' feki. Unaonesha kwamba hujui kinachoendelea katika nchi yako. Kwa kuwa hujui kama hujui, nikusamehe tu.
Naomba ufafanue namba 1, 3 na 4 kwenye post uliyo qoute kama ulivyofafanua namba 2.

Naam sisi tunafanya siasa mitandaoni maana wewe na mada yako sio siasa.

Sijawahi kuona serikali inayoongozwa na watu waoga kama awamu hii.

Mliona mkiacha Siasa za majukwaani ziendelee tena ambapo ni halali kikatiba Viwanda visingejengwa. Mkaona kurusha matangazo ya Bunge moja kwa moja ni kikwazo cha kujenga Viwanda.

Mnaamini tunafanya siasa za Majitaka lakini tukiwakosoa na hizo hizo hoja za majitaka mnakosa usingizi utadhani mna homa ya Ini na mnaishia kutumia vyombo vya dola kujibu hoja za Majitaka badala ya hoja kwa hoja.

Lakini kumbuka kwamba sasa watu wanajitambu sio kama kipindi cha nyuma.
 
Back
Top Bottom