PreGE2025 Chadema imeshakufa, ilifia hapa

PreGE2025 Chadema imeshakufa, ilifia hapa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

mtechnical

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
356
Reaction score
877
Kwa huzuni kubwa niseme kuwa chama cha CHADEMA ni kama kimeshajifia.

CHADEMA imebaki hasa hasa kwa wanaharakati wa demokrasia tu ila imepoteza kwa kiasi kikubwa uungwaja mkono wa wananchi, huu ni ukweli mchungu.

CHADEMA ILIFIA WAPI?

Kifo cha CHADEMA kilianza kwenye uchaguzi wa 2015 pale walipo mpokea Lowasa kuwa mgombea wao, lile lilikuwa kosa kubwa la kutosha kabisa kuwaua, na bahati mbaya wakaendelea kujipiga risasi wenyewe kipindi cha Magufuli na Magufuli wa udikteta wake akawachimbia kaburi kabisa.

CHADEMA ilipata uungwaji mkono mkubwa wa wananchi kwa vita yake dhidi ya ufisadi na wizi wa rasilimali za nchi, iliwaaminisha waTanzania kuwa hii nchi haitakuwa masikini kama ufisadi ukikomeshwa muda huo huo ikiwatuhumu viongozi kadhaa kuwa ni mafisadi papa na namba moja akiwa Lowasa.

CHADEMA walipo mkubali Lowasa wakalazimika kuachana na ajenda iliyo wapa uungwaji mkono ya ufisadi wakabaki kumsafisha Lowasa. Baada ya uchaguzi kuisha na Lowasa kurudi CCM wakakosa ujasiri wa kuendelea na hoja ya ufisadi.

Bahati mbaya Magufuli akawa dikteta akawapa hoja mpya ya demokrasia ambayo ndio wanaendelea nayo hadi hivi leo. Bahati mbaya kwao ni kuwa hoja ya demokrasia haina mvuto kwa asilimia kubwa ya watanzania isipokuwa wanasiasa na wanaharakati tu.

Mtanzania ambaye hana hata mpango wa kupiga kula ukija na hoja ya NO REFORM NO ELECTION yani unamshawishije? Kwanza nakuona kama unawaza kushika madaraka tu.

CHADEMA ndio ilikuwa tumaini pekee la kuiondoa CCM ila kwa sasa watanzania wameshakata tamaa. Ili CHADEMA ifufuke basi irudi kwenye misingi yake ambayo ni vita dhidi ya ufisadi na ubadhilifu wa mali ya uma.
 
Kwa huzuni kubwa niseme kuwa chama cha CHADEMA ni kama kimeshajifia.
CHADEMA imebaki hasa hasa kwa wanaharakati wa demokrasia tu ila imepoteza kwa kiasi kikubwa uungwaja mkono wa wananchi, huu ni ukweli mchungu.
CHADEMA ILIFIA WAPI?
Kifo cha CHADEMA kilianza kwenye uchaguzi wa 2015 pale walipo mpokea Lowasa kuwa mgombea wao, lile lilikuwa kosa kubwa la kutosha kabisa kuwaua, na bahati mbaya wakaendelea kujipiga risasi wenyewe kipindi cha Magufuli na Magufuli wa udikteta wake akawachimbia kaburi kabisa.
CHADEMA ilipata uungwaji mkono mkubwa wa wananchi kwa vita yake dhidi ya ufisadi na wizi wa rasilimali za nchi ,
iliwaaminisha waTanzania kuwa hii nchi haitakuwa masikini kama ufisadi ukikomeshwa muda huo huo ikiwatuhumu viongozi kadhaa kuwa ni mafisadi papa na namba moja akiwa Lowasa.
CHADEMA walipo mkubali Lowasa wakalazimika kuachana na ajenda iliyo wapa uungwaji mkono ya ufisadi wakabaki kumsafisha Lowasa.
Baada ya uchaguzi kuisha na Lowasa kurudi CCM wakakosa ujasiri wa kuendelea na hoja ya ufisadi.
Bahati mbaya Magufuli akawa dikteta akawapa hoja mpya ya demokrasia ambayo ndio wanaendelea nayo hadi hivi leo. Bahati mbaya kwao ni kuwa hoja ya demokrasia haina mvuto kwa asilimia kubwa ya watanzania isipokuwa wanasiasa na wanaharakati tu. Mtanzania ambaye hana hata mpango wa kupiga kula ukija na hoja ya NO REFORM NO ELECTION yani unamshawishije? Kwanza nakuona kama unawaza kushika madaraka tu.
CHADEMA ndio ilikuwa tumaini pekee la kuiondoa CCM ila kwa sasa watanzania wameshakata tamaa.
Ili CHADEMA ifufuke basi irudi kwenye misingi yake ambayo ni vita dhidi ya ufisadi na ubadhilifu wa mali ya uma.
Weka aya/paragraphs
 
Kwa huzuni kubwa niseme kuwa chama cha CHADEMA ni kama kimeshajifia.
CHADEMA imebaki hasa hasa kwa wanaharakati wa demokrasia tu ila imepoteza kwa kiasi kikubwa uungwaja mkono wa wananchi, huu ni ukweli mchungu.
CHADEMA ILIFIA WAPI?
Kifo cha CHADEMA kilianza kwenye uchaguzi wa 2015 pale walipo mpokea Lowasa kuwa mgombea wao, lile lilikuwa kosa kubwa la kutosha kabisa kuwaua, na bahati mbaya wakaendelea kujipiga risasi wenyewe kipindi cha Magufuli na Magufuli wa udikteta wake akawachimbia kaburi kabisa.
CHADEMA ilipata uungwaji mkono mkubwa wa wananchi kwa vita yake dhidi ya ufisadi na wizi wa rasilimali za nchi ,
iliwaaminisha waTanzania kuwa hii nchi haitakuwa masikini kama ufisadi ukikomeshwa muda huo huo ikiwatuhumu viongozi kadhaa kuwa ni mafisadi papa na namba moja akiwa Lowasa.
CHADEMA walipo mkubali Lowasa wakalazimika kuachana na ajenda iliyo wapa uungwaji mkono ya ufisadi wakabaki kumsafisha Lowasa.
Baada ya uchaguzi kuisha na Lowasa kurudi CCM wakakosa ujasiri wa kuendelea na hoja ya ufisadi.
Bahati mbaya Magufuli akawa dikteta akawapa hoja mpya ya demokrasia ambayo ndio wanaendelea nayo hadi hivi leo. Bahati mbaya kwao ni kuwa hoja ya demokrasia haina mvuto kwa asilimia kubwa ya watanzania isipokuwa wanasiasa na wanaharakati tu. Mtanzania ambaye hana hata mpango wa kupiga kula ukija na hoja ya NO REFORM NO ELECTION yani unamshawishije? Kwanza nakuona kama unawaza kushika madaraka tu.
CHADEMA ndio ilikuwa tumaini pekee la kuiondoa CCM ila kwa sasa watanzania wameshakata tamaa.
Ili CHADEMA ifufuke basi irudi kwenye misingi yake ambayo ni vita dhidi ya ufisadi na ubadhilifu wa mali ya uma.

Gombe:

Screenshot_20250306-183123_1.jpg
 
Kwa huzuni kubwa niseme kuwa chama cha CHADEMA ni kama kimeshajifia.
CHADEMA imebaki hasa hasa kwa wanaharakati wa demokrasia tu ila imepoteza kwa kiasi kikubwa uungwaja mkono wa wananchi, huu ni ukweli mchungu.
CHADEMA ILIFIA WAPI?
Kifo cha CHADEMA kilianza kwenye uchaguzi wa 2015 pale walipo mpokea Lowasa kuwa mgombea wao, lile lilikuwa kosa kubwa la kutosha kabisa kuwaua, na bahati mbaya wakaendelea kujipiga risasi wenyewe kipindi cha Magufuli na Magufuli wa udikteta wake akawachimbia kaburi kabisa.
CHADEMA ilipata uungwaji mkono mkubwa wa wananchi kwa vita yake dhidi ya ufisadi na wizi wa rasilimali za nchi ,
iliwaaminisha waTanzania kuwa hii nchi haitakuwa masikini kama ufisadi ukikomeshwa muda huo huo ikiwatuhumu viongozi kadhaa kuwa ni mafisadi papa na namba moja akiwa Lowasa.
CHADEMA walipo mkubali Lowasa wakalazimika kuachana na ajenda iliyo wapa uungwaji mkono ya ufisadi wakabaki kumsafisha Lowasa.
Baada ya uchaguzi kuisha na Lowasa kurudi CCM wakakosa ujasiri wa kuendelea na hoja ya ufisadi.
Bahati mbaya Magufuli akawa dikteta akawapa hoja mpya ya demokrasia ambayo ndio wanaendelea nayo hadi hivi leo. Bahati mbaya kwao ni kuwa hoja ya demokrasia haina mvuto kwa asilimia kubwa ya watanzania isipokuwa wanasiasa na wanaharakati tu. Mtanzania ambaye hana hata mpango wa kupiga kula ukija na hoja ya NO REFORM NO ELECTION yani unamshawishije? Kwanza nakuona kama unawaza kushika madaraka tu.
CHADEMA ndio ilikuwa tumaini pekee la kuiondoa CCM ila kwa sasa watanzania wameshakata tamaa.
Ili CHADEMA ifufuke basi irudi kwenye misingi yake ambayo ni vita dhidi ya ufisadi na ubadhilifu wa mali ya uma.
Vita dhidi ya ufisadi na ubadhilifu wa Mali za umma eti eeh!??

Fisadi nani ? atakaye mkamata fisadi nani ?? atakaye muhukumu fisadi nani ??

Nchi hii mwizi, mkamataji na anayehukumu wote ni ukoo mmoja labla kama wewe sio mtanzania.

Wanachokifanya chadema Cha no reform no election ndio sahihi kabisa kuliko kupambana na ufisadi ambao mwisho wa siku fisadi linapelekwa mahakamani ambako jaji ni baba au mama yake.

Nchi hii ni vile tu wananchi ni mazezeta ila

NO REFORM NO ELECTION.....

Kwa hali ya sasa hivi ndio vita sahihi.
 
Ndio kipindi niliwadharau na kukaa pembeni...
 

Attachments

  • 20240213_065335.jpg
    20240213_065335.jpg
    62.1 KB · Views: 16
Kwa huzuni kubwa niseme kuwa chama cha CHADEMA ni kama kimeshajifia.

CHADEMA imebaki hasa hasa kwa wanaharakati wa demokrasia tu ila imepoteza kwa kiasi kikubwa uungwaja mkono wa wananchi, huu ni ukweli mchungu.

CHADEMA ILIFIA WAPI?

Kifo cha CHADEMA kilianza kwenye uchaguzi wa 2015 pale walipo mpokea Lowasa kuwa mgombea wao, lile lilikuwa kosa kubwa la kutosha kabisa kuwaua, na bahati mbaya wakaendelea kujipiga risasi wenyewe kipindi cha Magufuli na Magufuli wa udikteta wake akawachimbia kaburi kabisa.

CHADEMA ilipata uungwaji mkono mkubwa wa wananchi kwa vita yake dhidi ya ufisadi na wizi wa rasilimali za nchi, iliwaaminisha waTanzania kuwa hii nchi haitakuwa masikini kama ufisadi ukikomeshwa muda huo huo ikiwatuhumu viongozi kadhaa kuwa ni mafisadi papa na namba moja akiwa Lowasa.

CHADEMA walipo mkubali Lowasa wakalazimika kuachana na ajenda iliyo wapa uungwaji mkono ya ufisadi wakabaki kumsafisha Lowasa.
Baada ya uchaguzi kuisha na Lowasa kurudi CCM wakakosa ujasiri wa kuendelea na hoja ya ufisadi.

Bahati mbaya Magufuli akawa dikteta akawapa hoja mpya ya demokrasia ambayo ndio wanaendelea nayo hadi hivi leo. Bahati mbaya kwao ni kuwa hoja ya demokrasia haina mvuto kwa asilimia kubwa ya watanzania isipokuwa wanasiasa na wanaharakati tu. Mtanzania ambaye hana hata mpango wa kupiga kula ukija na hoja ya NO REFORM NO ELECTION yani unamshawishije? Kwanza nakuona kama unawaza kushika madaraka tu.

CHADEMA ndio ilikuwa tumaini pekee la kuiondoa CCM ila kwa sasa watanzania wameshakata tamaa. Ili CHADEMA ifufuke basi irudi kwenye misingi yake ambayo ni vita dhidi ya ufisadi na ubadhilifu wa mali ya uma.
kwahiyo ndugu mchambuzi wa masuala ya kisiasa ndani ya vyama vya siasa,

unataka kusema kwamba chadema sasa imebaki ni skrepa tu?🐒
 
Uthibitisho wa kwanza kwamba CHADEMA ipo hai ni hili andiko lako, na pili ni mahangaiko ya dola dhidi ya CHADEMA.

Ukiona chama cha siasa Afrika hii viongozi wake hawasumbuliwi na vyombo vya dola, hawakamatwi na kufungwa kwa mashtaka ya kijinga ujue hicho chama ni MFU, kimejifia muda.

Wanaosema CHADEMA imekufa ni ama hawana akili timamu au wanajifariji kisaikolojia.
 
Polisi wanavyozidi kuwa makatili dhi ya Wananch ndivyo wanavyopandishwa vyeo HAKI iko wapi?
 
Hizo ulizoandika wala sio sababu.Ni ujinga tu,watanzania sio watu wakushikilia hoja za kisiasa za majukwaani.Ujio wa lowasa ulileta manufaa mengi chadema kuliko kipindi chochote kwenye historia ya uchaguzi wa vyama vingi labda kama wewe sio mfwatiliaji.Kufa kwa chama cha siasa ni process ndefu sana na kwa chadema bado hakijafika uko kwasababu bado kina wafuasi.Tatizo la chadema nikutokujua kua mshindani wao mkubwa hana nia yakushindana kihalani na wao wamekosa mbinu mbadala za kupambana naye au watumie njia gani kupata uungwaji mkono kutoka ndani ya wenye kuketi meza ya maamuzi.Wao wanafikiri kwa afrika hii unaweza ukapiga tu porojo za kiharakati mitandaoni na mikutano ya hadhara ukawa umemaliza.Kwahali hiyo wanakosa mbinu mbadala zakuitetemesha ccm ambayo imekita mizizi kila mahali.Kwahiyo ili warudi kwenye matumaini nilazima wajipange upya kwambinu mpya.
 
Back
Top Bottom