... Huu ni wakati wa CHADEMA kuwa wazi kabisa na sera zao. Wananchi waelewe chama kinasimamia nini.
... Sidhani kama wanaweka mkazo kwenye kuhakikisha wana sera mbadala zinazoeleweka kwa wananchi.
Tatizo lako nalijua kutokana na maandiko yako humu.Kimeozaje mkuu. Kujidanganya kwako ndo kosa kubwa sana. Unaongea as if CHadema imejaaa kila kitu safi na haki. Hapo ndo unaonekana mjinga. Kuwa mkweli hata kama inauma ndo dawa ya kweli. Kosa kubwa sana. MlifanyA kwa Dr slaa. Kama mbunge alifanya kazi kubwa jimboni kwake. Hivyo watu walimwamini. Sio maneno maneno ambayo ukiuliza kafanya Nini ohhhh anajua kutukana.
Kalamu1
nimeshiliki kwa ukamilifu uchaguzi wa 2021
Nimeshiriki vyema mchakato mzima wa kampeni mwanzo mwisho itoshe kusema, wanachokosa CHADEMA ni jeshi la kulinda kura zao na vyombo vya kutangaza huo ushindi wao!
hiki chama kipo zaidi ya 80% maeneo ya nchi hii!
Sera zao mbona zinaeleweka vizuri tu!
elimu bure(jpm) akaikwapua 2015, serikali za majimbo ili kupunguza centralization ya uchumi na upendeleo katika maendeleo ya nchi, katiba mpya na ushirikishwaji wa wananchi katika maamuzi ya nchi kidemokrasia!
Cha kuwashauri CHADEMA ni kupunguza tu zile siasa za kihanarakati zisizo na tija yoyote.
Ule uporaji wa kura wa mwaka jana ndyo taswira ya uimara wa CHADEMA!
Mosi, naamini kwamba CHADEMA waliingia uchaguzi wa 2020 sababu hawakuamini kwamba CCM wangeendesha uporaji wa kiwango hicho katika uchaguzi mkuu. Walitarajia uwepo wa waangalizi wengi wa kimataifa. Magufuli alikwepa hili la waangalizi kwa kukataa fedha za UN, ambazo ndio huambatana na waangalizi hao. Kwa hiyo akadai kwa wananchi kwamba uchaguzi huu haitumiki fedha ya nje bali ya ndani tuuu!!! Kumbe kazima taa ili akwibe kwa amani na utulivu.Mwaka jana hapakuwepo na uchaguzi mkuu 'guwe_la_manga', huo ulikuwa ni uchafuzi.
Lakini swali ambalo bado ninajiuliza ni hili, labda nawe utasaidia kulijibu:
Hivi kweli CHADEMA waliingia kwenye uchaguzi huo wakitegemea kwamba utakuwa huru na wa haki? Zingatia hapa kilichofanyika na ule uchaguzi wa serikali za mitaa uliokuwa umetangulia!
Ni nini hasa kilichowaaminisha CHADEMA kwamba wangeweza kushiriki na kupata ushindi katika hali iliyokuwa bayana kabla ya kupiga kura!
Siwezi kamwe kukubishia juu ya utayari wa ushindi walioutegemea kutoka kwa wananchi kama ulivyoeleza kuwa hali uliyoishuhudia wewe mwenyewe. Sasa jiulize, wananchi wakawapigia kura CHADEMA, CCM wakazipora, na kukwa kimya kana kwamba hakuna kilichotokea! Huoni hitilafu katika hali hiyo?
Maoni yangu ni kwamba, hata kama CHADEMA walipewa kura nyingi na wananchi, wananchi hao hawakuwa na msisimuko wa kuiunga mkono CHADEMA. Hata kama waliwapa kura zao, hiyo ilikuwa ni kwa sababu hapakuwa na mwingine wa kumpa; zilipoporwa, wananchi hawakuwa na mori wa kukataa uharamia huo.
Kazi waliyokuwa waifanye CHADEMA kabla ya kura kupigwa, ni kuwaandaa wananchi wasikubali kunyang'anywa haki yao ya msingi, haki ya kuwachagua viongozi wanaowataka.
Mwisho, kutokana na niliyoandika hapo juu, sina hakika sana kwamba wananchi hata kama waliwapa kura zao nyingi CHADEMA, sababu ya kufanya hivyo ilikuwa ni kwa sababu walielewa na kuzikubali sera, kama zile ulizozitaja wewe.
Kunawezekana sana kama waliwapigia CHADEMA kura, sababu inaweza kuwa ni kwa sababu ya kuwakataa CCM, na hasa kutokana na aliyokuwa ameyafanya mwenyekiti wa chama hicho kama rais.
Sitapenda unielewe kwamba wananchi hawazipendi sera za CHADEMA, lakini ningependa kupata ushahidi unaojitegemea zaidi.
Nimekusoma vyema.Kwa uzoefu wangu mdogo nilioupata kuhusu siasa za Bongo, sehemu kubwa ya wananchi hawana muda hata wa kupima kitu kinachoitwa sera. Ni mihemko tu, ukiwaudhi wanakutosa kwa mihemko, ukiwateka kwa hoja nyepesi nyepesi tu, wanakupigia makofi na kukuchagua kwa mihemko pia. Sera zipo kwenye documents za vyama, ila wananchi wengi wala huwa hawana muda wa kuzitathmini. Pengine hata wewe ukiulizwa sera gani kumi zilikuvutia ukakichagua chama ulichokipigia kura, huenda ukajitahidi kukumbuka tatu tu, tena si kwa sababu umezitathmini, ila kwa sababu zimeimbwaimbwa ukazikariri
Chadema imewekeza sana kwenye mitaa na vijiji,ushahidi kamili ni uchaguzi wa uliopita. Bila figisu CCM ingeng'okaKazi kubwa iliyo mbele yao (CHADEMA), ni kuwaendea wananchi walipo,huko mitaani. Wasitegemee sana hizi siasa za majukwaani.
CCM imetumia udhaifu wao huo kwa vile wao CCM wako kila sehemu mitaani.
CHADEMA inabidi warekebishe muundo wao wa chama ili ngazi za mashina ziwe na sehemu muhimu zaidi ndani ya chama hicho.
Niseme tu mkuu wangu 'Mindi'; mada hii ni kuwahimiza CHADEMA "Wagange yajayo", yaliyopita liwe fundisho.Mosi, naamini kwamba CHADEMA waliingia uchaguzi wa 2020 sababu hawakuamini kwamba CCM wangeendesha uporaji wa kiwango hicho katika uchaguzi mkuu. Walitarajia uwepo wa waangalizi wengi wa kimataifa. Magufuli alikwepa hili la waangalizi kwa kukataa fedha za UN, ambazo ndio huambatana na waangalizi hao. Kwa hiyo akadai kwa wananchi kwamba uchaguzi huu haitumiki fedha ya nje bali ya ndani tuuu!!! Kumbe kazima taa ili akwibe kwa amani na utulivu.
Pili CHADEMA wali-underestimate kiwango cha kukosa aibu cha Magufuli, hawakuamini angeweza kuendesha kiwango hicho cha ujambazi.
Kuhusu wananchi kulinda kura zao, ni vile tu kwamba hawajafikia kiwango hicho, ipo siku watafikia. Lakini pengine matokeo ya wizi huo ni kutengwa kimataifa kiasi kwamba kuendesha nchi sasa ni ngumu zaidi. Serikali inazidi kuwapora wananchi wake. Angalia package za bima ya afya za Magufuli. Ni wizi mtupu. Ni mradi wa kukusanya fedha ya miradi yake na siyo huduma ya Afya kwa wote.
Sidhani, kama ulivyosema pia, kwamba serikali itathubutu kuiba kura tena kwa viwango vya serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020. Inahitaji 'kichaa' na sidhani kama hao waliopo CCM sasa ivi kuna mwenye kiwango hicho cha ukichaa.
Ni kweli CHADEMA wanaendelea kuenjoy kura za chuki na pia sympathy. Wanateseka mno na pia maisha kwa wote ni magumu sana. Wakiboresha meseji yao itakuwa vema zaidi
Umeandika mengi mkuu why unazungukazunguka?waambie chama dola wa LEVEL playing field na itisha mechi even today uone makali ya CDM,inasikitisha mno middle class wetu kuingiza vichwa vyao mchangani,walete tume huru ya uchaguzi ,kampeni huru(cdm wanahitaji mikutano 10 tu nchi nzima.Hakuna shaka yeyote, na sidhani kwamba kuna mtu anayeweza kuhoji uwepo wa CHADEMA kama chama cha kisiasa kilicho na ushindani mkubwa hapa nchini licha ya misukosuko mingi iliyoelekezwa kwao ili kuwamaliza kabisa katika miaka mitano na zaidi sasa iliyopita.
Ni sawa kabisa kusema kwamba CHADEMA wamepitia kwenye tanuru la moto mkali, na wamepikika sawasawa kuweza kuendelea na pilkapilka zao za kisiasa na kutafuta njia ya kuliongoza taifa hili.
Sioni mbele yao, kupata hujuma tena, kama walizozipata miaka hii ya karibuni chini ya utawala wa Marehemu Magufuli. Tanzania itakuwa na bahati mbaya sana, kama patatokea hivi karibuni misukosuko iliyolitingisha taifa kama ilivyotokea wakati wa serikali ya Magufuli.
Watu wanaweza kuhoji kwamba kuendelea kuwepo kwa CCM madarakani hiyo ndiyo hatari kubwa kwa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani.
Mimi hilo silioni hivyo kwa sasa, na hata katika CCM ya enzi za Kikwete. Hatari iliongezeka zaidi alipoingia madarakani Magufuli na kutangaza waziwazi kutopenda uwepo wa vyama vya upinzani.
CCM wenyewe kama chama, hila zao zilikuwa ni za kawaida, mradi tu wanapata ushindi, hawakuwa na lengo maalum la kuua upinzani.
CHADEMA wafanye nini (samahani kwa kuwasema CHADEMA, badala ya vyama vya upinzani, kwa sababu vingine ndio hivyo tena vimetekwa).
Huu ni wakati wa CHADEMA kuwa wazi kabisa na sera zao. Wananchi waelewe chama kinasimamia nini.
Kati ya sifa chache, lakini muhimu alizojijengea Magufuli (sio CCM) ni kuonekana kuwa mtetezi wa mali na utajiri wa nchi hii na maendeleo ya wananchi wake.
Amejitambulisha bila shaka yoyote, kwamba yeye alikuwa ni mtetezi mkubwa wa maslahi ya Tanzania na wananchi wake. Amejenga hata ukuta, kulinda Tanzanite yetu iliyokuwa inatoroshwa kwenda nchi za nje na kuwanufaisha hao zaidi ya sisi tulivyokuwa tunanufaika kwayo.
Swala la madini aliliwekea mkazo sana; hata kama ilionekana kama kulikuwa na makosa katika juhudi hizo, lakini wananchi walielewa madhumuni yake. Kuna mifano mingi kuhusu msimamo wake juu ya mali za Tanzania.
Hatujui kuhusu mikataba mbalimbali nchi yetu iliyoiingia na nchi na mashirika mbalimbali ya kimataifa, lakini bado inaelekea wananchi waliamini kwamba mikataba hiyo ilikuwa ni kwa maslahi yao.
Jambo ambalo inawezekana hakulifanya vizuri ni kuhusu mashirikiano yetu na nchi mbalimbali duniani kwa vile alikazia zaidi "ubeberu" na mambo mengine kama masimango yao.
Nimeyaandika haya, ili CHADEMA watambue kwamba kama sera zao hazieleweki kwa wananchi, kazi yao itaendelea kuwa ngumu zaidi kuwashawishi wananchi hao kuwapa madaraka. Ni lazima wajieleze waziwazi kwa wananchi, wao ni nini hasa wanakisimamia kama chama cha siasa, na nchi yetu itafaidika vipi na misimamo yao hiyo kama watapewa ridhaa ya kuongoza serikali.
Kwa hiyo, nadhani ni halali sasa kusema kwamba adui mkubwa aliye mbele ya CHADEMA ni CHADEMA yenyewe. CCM wataendelea na hadaa zao kwa wananchi, hadaa za "Hawa ni Wenzetu" kama ilivyowahi kuwa huko nyuma, na wananchi kama hawaoni mbadala wa kuwapa madaraka, watarudi huko huko kwenye chama kilichooza ndani kwa ndani.
Niseme hapa, sijui kama Samia atakuwa na nguvu za kukibadilisha hiki chama kiwe chama cha wananchi wenyewe kwelikweli. Sijui.
Hatujui
Huko unakotaka twende tulishafika na kumaliza kazi , hii ndio sababu ya Mahera kupokea maagizo ya ccm ( Bashiru , Polepole na Magufuli ) ya kuondoa wagombea wa Chadema nchi nzima na kwingine kupeleka kura za mabegi , labda nikutoe shaka , Chadema imo mpaka ndani ya ccm na atakayejaribu kuihujumu atakiona cha mtemakuni , nimemalizaKazi kubwa iliyo mbele yao (CHADEMA), ni kuwaendea wananchi walipo,huko mitaani. Wasitegemee sana hizi siasa za majukwaani.
CCM imetumia udhaifu wao huo kwa vile wao CCM wako kila sehemu mitaani.
CHADEMA inabidi warekebishe muundo wao wa chama ili ngazi za mashina ziwe na sehemu muhimu zaidi ndani ya chama hicho.
Wizi kistaarabu ndio nini? Hivi huwa una akili timamu?Niseme tu mkuu wangu 'Mindi'; mada hii ni kuwahimiza CHADEMA "Wagange yajayo", yaliyopita liwe fundisho.
Wizi wa kura hautakoma, utaendelea kuwepo, hata kama utakuwa ni wizi wa kistaarabu chini ya utawala mpya.
CHADEMA walijue hili, na wawe tayari kufanya kazi nzito zaidi kuwavuta wananchi upande wao ili kufidia kura zinazoingia upande mwingine kwa wizi.
Ni kazi ngumu sana, lakini ni kazi inayowezekana kwa viongozi waliojizatiti kuifanya kwa ufanisi.
Hakuna mbadala wa kuwaendea wananchi kila kona ya nchi walipo na kuwaelimisha chama chao kinasimamia nini. Wananchi wakielimika, sina shaka watachagua kwa utashi wao wanachokitaka.
ngoja utandikwe ban nyingine akili ikukae sawaWizi kistaarabu ndio nini? Hivi huwa una akili timamu?
Mimi siamini kama wapiga kura wa nchi hii wanachagua viongozi baada ya kusoma,kuchambua na kuelewa Sera za vyama vyao.Sidhani kama tumefikia umakini wa kiwango hicho kama taifa.Hakuna shaka yeyote, na sidhani kwamba kuna mtu anayeweza kuhoji uwepo wa CHADEMA kama chama cha kisiasa kilicho na ushindani mkubwa hapa nchini licha ya misukosuko mingi iliyoelekezwa kwao ili kuwamaliza kabisa katika miaka mitano na zaidi sasa iliyopita.
Ni sawa kabisa kusema kwamba CHADEMA wamepitia kwenye tanuru la moto mkali, na wamepikika sawasawa kuweza kuendelea na pilkapilka zao za kisiasa na kutafuta njia ya kuliongoza taifa hili.
Sioni mbele yao, kupata hujuma tena, kama walizozipata miaka hii ya karibuni chini ya utawala wa Marehemu Magufuli. Tanzania itakuwa na bahati mbaya sana, kama patatokea hivi karibuni misukosuko iliyolitingisha taifa kama ilivyotokea wakati wa serikali ya Magufuli.
Watu wanaweza kuhoji kwamba kuendelea kuwepo kwa CCM madarakani hiyo ndiyo hatari kubwa kwa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani.
Mimi hilo silioni hivyo kwa sasa, na hata katika CCM ya enzi za Kikwete. Hatari iliongezeka zaidi alipoingia madarakani Magufuli na kutangaza waziwazi kutopenda uwepo wa vyama vya upinzani.
CCM wenyewe kama chama, hila zao zilikuwa ni za kawaida, mradi tu wanapata ushindi, hawakuwa na lengo maalum la kuua upinzani.
CHADEMA wafanye nini (samahani kwa kuwasema CHADEMA, badala ya vyama vya upinzani, kwa sababu vingine ndio hivyo tena vimetekwa).
Huu ni wakati wa CHADEMA kuwa wazi kabisa na sera zao. Wananchi waelewe chama kinasimamia nini.
Kati ya sifa chache, lakini muhimu alizojijengea Magufuli (sio CCM) ni kuonekana kuwa mtetezi wa mali na utajiri wa nchi hii na maendeleo ya wananchi wake.
Amejitambulisha bila shaka yoyote, kwamba yeye alikuwa ni mtetezi mkubwa wa maslahi ya Tanzania na wananchi wake. Amejenga hata ukuta, kulinda Tanzanite yetu iliyokuwa inatoroshwa kwenda nchi za nje na kuwanufaisha hao zaidi ya sisi tulivyokuwa tunanufaika kwayo.
Swala la madini aliliwekea mkazo sana; hata kama ilionekana kama kulikuwa na makosa katika juhudi hizo, lakini wananchi walielewa madhumuni yake. Kuna mifano mingi kuhusu msimamo wake juu ya mali za Tanzania.
Hatujui kuhusu mikataba mbalimbali nchi yetu iliyoiingia na nchi na mashirika mbalimbali ya kimataifa, lakini bado inaelekea wananchi waliamini kwamba mikataba hiyo ilikuwa ni kwa maslahi yao.
Jambo ambalo inawezekana hakulifanya vizuri ni kuhusu mashirikiano yetu na nchi mbalimbali duniani kwa vile alikazia zaidi "ubeberu" na mambo mengine kama masimango yao.
Nimeyaandika haya, ili CHADEMA watambue kwamba kama sera zao hazieleweki kwa wananchi, kazi yao itaendelea kuwa ngumu zaidi kuwashawishi wananchi hao kuwapa madaraka. Ni lazima wajieleze waziwazi kwa wananchi, wao ni nini hasa wanakisimamia kama chama cha siasa, na nchi yetu itafaidika vipi na misimamo yao hiyo kama watapewa ridhaa ya kuongoza serikali.
Kwa hiyo, nadhani ni halali sasa kusema kwamba adui mkubwa aliye mbele ya CHADEMA ni CHADEMA yenyewe. CCM wataendelea na hadaa zao kwa wananchi, hadaa za "Hawa ni Wenzetu" kama ilivyowahi kuwa huko nyuma, na wananchi kama hawaoni mbadala wa kuwapa madaraka, watarudi huko huko kwenye chama kilichooza ndani kwa ndani.
Niseme hapa, sijui kama Samia atakuwa na nguvu za kukibadilisha hiki chama kiwe chama cha wananchi wenyewe kwelikweli. Sijui.
Hatujui
Sidhani, na wala sitegemei kuona uhujumu kiasi ya tuliouona chini ya Magufuli, sidhani.Huko unakotaka twende tulishafika na kumaliza kazi , hii ndio sababu ya Mahera kupokea maagizo ya ccm ( Bashiru , Polepole na Magufuli ) ya kuondoa wagombea wa Chadema nchi nzima na kwingine kupeleka kura za mabegi , labda nikutoe shaka , Chadema imo mpaka ndani ya ccm na atakayejaribu kuihujumu atakiona cha mtemakuni , nimemaliza
Sina tatizo na wewe tena mkuu!Wizi kistaarabu ndio nini? Hivi huwa una akili timamu?
Ninakubaliana na wewe kwa kiasi; lakini haitakuwa hivyo milele.Mimi siamini kama wapiga kura wa nchi hii wanachagua viongozi baada ya kusoma,kuchambua na kuelewa Sera za vyama vyao.Sidhani kama tumefikia umakini wa kiwango hicho kama taifa.
Tulionya mapema sana kwamba shetani hajawahi kumshinda Mungu , nadhani sasa somo linaanza kuelewekaSidhani, na wala sitegemei kuona uhujumu kiasi ya tuliouona chini ya Magufuli, sidhani.
Ndiyo maana sasa CHADEMA wajizatiti zaidi kuvuna walichopanda, kama kweli mbegu ilishapandwa kama unavyoeleza.
Wakati huo huo, usisahau kwamba CCM ni chama kikongwe sana na wana miundo mbinu kila mahala.
Wao pia wanayo nafasi ya kuji-'re-invent'; kama kuvua gamba hivi kwa kutumia miundo mbinu nyingi walizonazo kujisafisha kwa wananchi.
Hizi ndizo tahadhari tunazowaeleza mzijue
CCM wanatumia dola kubaki madarakani. CHADEMA wana nguvu ya wananchi yakuwaweka madarakani. Muda utaongea.CCM itaendelea kutawala kwa muda mrefu sana.