CHADEMA ije na Sera ya kufufua Vyuo vya Ufundi

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,180
85,338
Team,

Tunaishi kwenye ulimwengu ambao ukosefu wa ajira rasmi umekua tatizo kubwa sana, Tanzania haiwezi kujitenga na ukweli huu.

Sasa, kwakuwa Serikali sikivu ya CCM imeua vyuo vya Ufundi na vile vya jamii ni vyema CHADEMA ikaunda na kutamka wazi wazi kuvifufua vyuo hivi.

Vyuo hivi baadhi vilikuwa chini ya Wizara ya Afya na vingine vikawekwa chini ya Wizara ya Elimu.

Vyuo hivi vilikuwa vimetapakaa nchi nzima vikifundisha skills mbali mbali ambazo ziliwawezesha wanufaika kumudu maisha yao pasipo kupiga mfumo.
 
Mfumo mzima wa utoaji elimu inabidi urekebishwe kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu.

Elimu iwe ni bure, mitaala ipitiwe upya na maslahi ya walimu yaboreshwe.
Tuna kazi kubwa sana ya kufanya kuhusu elimu hapa nchini kwetu.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom