Chadema hili mmelitazama vipi?

Mr.Busta

JF-Expert Member
Mar 24, 2011
672
99
WanaJF ambao ni wapenzi na wakereketwa wa CDM,pia kwa wanachama na viongozi kwa ujumla naomba kutoa angalizo mapema ili liwezekufanyiwa kazi mapema zaidi hasa katika katiba mpya pamoja na tume ya uchaguzi kwa ujumla

HOJA yangu ni kuhusu tatizo la form za kugombea hasa ubunge na udiwani.Nakumbuka kuna majimbo yaliyopita bila CDM kuwa na mwakilish,na baadhi yalitokana na sababu ya wagombea kuchukua form bila kurudisha.

Kuna wangine ambao walienda kuchukuwa form tume na kuambiwa kuwa tayari kuna mwanachama wenu amechukuwa hvyo kama unahitaji form inabidi atafutwe aliyechua hiyo form ndipo upewe nyingine na hii ilisemekana kwamba ni njama zilifanywa na CCM kushirikiana na viongozi wa tume.

Hivyo CDM mmejipanga vipi 2015 ILI lisitokee tena kama ni kweli ilikuwa ni hujuma?nafikiri kwa wanaolifahamu hili vizuri watalitolea ufafanuzi zaidi.naomba kuwasilisha.
 
Tutavuka daraja tukilifikia

tunatakatujue kama linamapungufu ambayo yatatakiwa yawekwenye katiba ili tusije chelewa au kurekebishwa kwa sheria mapema zaidi ili mda ukifika tusiwe na mambo mengi ya kuyafanyia kazi kisheria.
 
Tutaliongelea kwenye katiba mpya

Hili liongelewe mapema kwani wao wamezidi kuwekea mapandikizi kwa vijisenti vyao ambayo huja kujitoa dakika za mwisho, jambo hili linaudhi sana na ni wakati muafaka hivi sasa kuweka mechanism ambayo itakuwa ina check na kutoa ripoti moja kwa moja makao makuu kuhusu uadilifu wa waombaji uongozi ndani ya CDM, PIA kosa lililofanyika kwa wahamiaji wa fasta kama wasomali eg Shibuda hao ndio kabisaaaa mlango ufungwe isipokuwa kwa wale wanaotoa ushirikiano na chama hivi sasa lakini bado wako CCM na si ghafla
 
Back
Top Bottom