Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Kwa kweli inasikitisha sana hasa kwa sisi wapenda mabadiliko na wafuasi wa CHADEMA kuona haya mapungufu ya wazi katika kampeni za CHADEMA.
Ukizunguka maeneo mengi Tanzania, mijini na vijijini, hakuna mabango ya mgombea uraisi wa CHADEMA!!!!. Sijui sababu ni nini lakini nadhani CHADEMA kama chama makini walitakiwa wajiandae mapema angalau katika hili suala la mabango. Najua kampeni inahusisha mambo mengi lakini hili la mabango ni muhimu na lilitakiwa kupewa kipaumbele.
CHADEMA wasibweteke kwa kudhani kuwa mgombea wao anajulikana na kila mtu... mbona KIKWETE anajulikana lakini kila unakopita mabango yake yamejaa! Na ukweli ni kwamba bado ni asilimia kubwa tu ya watanzania ukiwauliza mgombea uraisi mwingine zaidi ya Kikwete anashindwa kutaja au inamchukua muda fulani kufikiria (na hii ni mijini na zaidi vijijini). Kwa hiyo kama kuna watu wanahusika hili suala naomba wajitahidi, NI AIBU...
Ukizunguka maeneo mengi Tanzania, mijini na vijijini, hakuna mabango ya mgombea uraisi wa CHADEMA!!!!. Sijui sababu ni nini lakini nadhani CHADEMA kama chama makini walitakiwa wajiandae mapema angalau katika hili suala la mabango. Najua kampeni inahusisha mambo mengi lakini hili la mabango ni muhimu na lilitakiwa kupewa kipaumbele.
CHADEMA wasibweteke kwa kudhani kuwa mgombea wao anajulikana na kila mtu... mbona KIKWETE anajulikana lakini kila unakopita mabango yake yamejaa! Na ukweli ni kwamba bado ni asilimia kubwa tu ya watanzania ukiwauliza mgombea uraisi mwingine zaidi ya Kikwete anashindwa kutaja au inamchukua muda fulani kufikiria (na hii ni mijini na zaidi vijijini). Kwa hiyo kama kuna watu wanahusika hili suala naomba wajitahidi, NI AIBU...