Mallaba
JF-Expert Member
- Jan 30, 2008
- 2,554
- 47
VIONGOZI wa juu na wabunge wa Chadema jana walitawanyika katika wilaya mbalimbali za mkoa wa Mwanza na kufanya mikutano ya hadhara kuendelea kupinga kupanda kwa gharama za maisha, malipo kwa Kampuni ya Dowans na kupanda kwa gharama za umeme.
Viongozi na wabunge hao wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe na Katibu wake mkuu Dk Willbrod Slaa aliyekuwa mgombea urais katika uchaguzi mkuu uliopita Oktoba 31 mwaka 2010 walichagiza katika mikutano hiyo ya mtawanyiko.
Mikutano hiyo ya hadhara ilikusanya maelfu ya wakazi wa mkoa wa Mwanza, huku mwenyekiti Mbowe akifanya mkutano wa hadhara wilayani Geita akiwa ameongozana na wabunge wanne wa chama hicho na Katibu wake Dk Slaa akiwa Kisiwani Ukerewe ambako naye aliambatana na mbunge wa Ukerewe, Salvatory Machemli na wabunge wa viti maalum, Rebecca Mngodo na Grace Kiwelu.
Viongozi na wabunge hao wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe na Katibu wake mkuu Dk Willbrod Slaa aliyekuwa mgombea urais katika uchaguzi mkuu uliopita Oktoba 31 mwaka 2010 walichagiza katika mikutano hiyo ya mtawanyiko.
Mikutano hiyo ya hadhara ilikusanya maelfu ya wakazi wa mkoa wa Mwanza, huku mwenyekiti Mbowe akifanya mkutano wa hadhara wilayani Geita akiwa ameongozana na wabunge wanne wa chama hicho na Katibu wake Dk Slaa akiwa Kisiwani Ukerewe ambako naye aliambatana na mbunge wa Ukerewe, Salvatory Machemli na wabunge wa viti maalum, Rebecca Mngodo na Grace Kiwelu.