CHADEMA hali si shwari

CHADEMA hali si shwari

Viongozi wa chama hicho wanajitahidi sana kulipamba sanduku la marehemu/Jeneza kwa nje lakini ukweli wa mambo ni kuwa ndani kuna maiti, ambayo imepigwa dawa na ganzi ili isitoe harufu. baada ya muda mfupi mwili huu usipozikwa harufu itawaumbua kwa waombolezaji endapo hawatafanyia kazi ukweli huu mchungu.

Hivi karibuni wanachama waandamizi wa CHADEMA akiwemo mwenyekiti wa BAVICHA wamehamia CCM, wanachama waandamizi wa vyama vingine ikiwemo wabunge wanahamia CCM kwa kasi ya kutisha. ni wakati muafaka sasa kwa vyama vya upinzani hasa CHADEMA ambacho ni cha kikuu cha upinzani kujitafuta/kujisachi/kujipangusapangusa....hali ya mambo sio nzuri sana huko chumbani. amkeni haraka..........hizi taarifa za Mnyika kukihama CHADEMA SIO ZA KUPUUZWA. ZIFANYIENI KAZI. ATASAJILIWA NA TIMU PINZANI SIO MUDA MREFU.
Hivi ganzi inazuia harufu ......................!!?
 
imepigwa ganzi inataka kufanyiwa post mortem.
Hawa watu Chadema hawaambiliki hakuna anaetaka upinzani ufe ila chadema Kama haina strategy jitafakarini fanyeni research muachane na Sababu moja mbio kuwa na uhakika nayo kuna kitu zaidi ya mnachoimba na nyingi ni wabishi hata ccm ilifika hapo ila haijawa na approach na ubishi Kama wenu
 
Wananuliwa ipo cku watarudi nyumbani
Huu ni Udhaifu mwingine wa kuona kuwa baadhi ya viongozi wa Chadema wananunulika kirahisi namna hiyo.
Sasa chama ambacho baadhi ya viongozi wake wananunulika tunafanyaje ili kuinusuru hali hii.
Inamaana tumwamini Mboe peke yake sasa, au na yeye ana bei yake ?
Vitendo vinavyofanywa na baadhi ya viongozi wa Chadema vya kununuliwa ni vya aibu kwa Chadema kwani licha ya kuwakatisha tamaa wanachama na wadau wengine wa Chadema lakini pia kinaleta hisia ya kutoaminika kwa wananchi wa Tanzania.
Wanachama na wapenzi wa Chadema wanatumia nguvu nyingi kuwasimamia na kuwaunga mkono wagombea wao wa Uongozi hadi wanapata Ushindi, halafu kirahisirahisi tu wanajiuzuru na kujiunga na chama kingine. Kisa ati wananunuliwa, huu ni ufisadi na hujuma kwa Watanzania na wapenda mageuzi kwa ujumla wake.
Haieleweki hii ni njaa au kutojitambua kwa hao wanaonunuliwa.
Kweli hii inasikitisha na kuvunja moyo juhudi za kuimarisha upinzani nchini kwetu.
Mimi nawalaumu sana hao wanaonunuliwa kuliko mnunuaji.
Acheni njaa imarisheni Chama
Mungu ibariki Chadema Mungu ibariki Tanzania
 
CCM inajipambanua kuwa chama kisichopenda rushwa, wakati ni tofauti kabisa na matendo yake. Kinanunua, kina warubuni na mara nyingine kuwatisha kuwafilisi mali zao wapinzanu wasipohama upinzani. Ahadi za kupewa madaraka nje ya upinzani ndo ngao yao kubwa (nafikiri hii ina baraka ya mkubwa wao).
Anayerudi CCM kwa kisingizio cha kwamba hicho chama sasa kinafanya makubwa ni zezeta, ni makubwa yapi? Mfano wa haraka ni kile kitendo cha rais kuzuia private contarctors kujenga hostel za UDSM na badala yake wakajenga TBA - ni nini kimetokea? Ni ujenzi usiokidhi engineering specifications ambao umeleteleza crack kubwa kabla hata mwaka kwisha. Sasa kitachofuata ni gharama mara dufu, either tubomoe ukuta ujengwe upya au tuwe wa kuziba mara kwa mara.
Mifano ni mingi. Ugua au uguliwa ukazwe Muhimbili, kama unapaswa kupelekwa chumba cha upasuaji uatkuta hata machela hayapo na kama yapo hakuna nesi wa kuyasukuma hadi huko - upuuzi mtupu. MOI hukomndo usiseme.
Nenda mahakamani uone jinsi haki inavyonunuliwa kwa pesa......
Tukija maisha ya kawaida leo ni afadhai ya jana. Wanaokula mara tatu kwa siku namba yao inapungua kila siku na hii ni hatari sana.
Ndugu yangu fikiri kabla ya kuandika nadhani hujazunguka na hata CHADEMA yenyewe hujaijua kabisa unaongea bila kuifanyia kazi.
 
Viongozi wa chama hicho wanajitahidi sana kulipamba sanduku la marehemu/Jeneza kwa nje lakini ukweli wa mambo ni kuwa ndani kuna maiti, ambayo imepigwa dawa na ganzi ili isitoe harufu. baada ya muda mfupi mwili huu usipozikwa harufu itawaumbua kwa waombolezaji endapo hawatafanyia kazi ukweli huu mchungu.

Hivi karibuni wanachama waandamizi wa CHADEMA akiwemo mwenyekiti wa BAVICHA wamehamia CCM, wanachama waandamizi wa vyama vingine ikiwemo wabunge wanahamia CCM kwa kasi ya kutisha. ni wakati muafaka sasa kwa vyama vya upinzani hasa CHADEMA ambacho ni cha kikuu cha upinzani kujitafuta/kujisachi/kujipangusapangusa....hali ya mambo sio nzuri sana huko chumbani. amkeni haraka..........hizi taarifa za Mnyika kukihama CHADEMA SIO ZA KUPUUZWA. ZIFANYIENI KAZI. ATASAJILIWA NA TIMU PINZANI SIO MUDA MREFU.
Mi naiona tatizo la vyama vya upinzania Tanzania ni kupata mafanikio makubwa katika uchaguzi wa 2015 wakajua wameshamaliza mchezo bila kujua CCM wanajitafakari na kujitathmini ili kuja na mikakati madhubuti ya kutatua changamoto ambazo wananchi walikuwa wanaziona kero kwa taifa. Magufuli kipindi cha uchaguzi alizunguka kupata maoni kwa wananchi na alikuwa msikivu; hivyo alivyopata urais akaanza kutekeleza alichoambiwa na wananchi kama kero. Kipindi mabadiliko hayo yanatokea, wapinzani hawakusoma alama za nyakati wakaendelea na porojo zilezile walizozizoea. Badala ya kubadilika kwa kufuata mwenendo wa madabiliko wao kabaki na zile habibu rejea za kukosoa vitu vidogo ambavyo serikali inakosea. Wananchi wanaona matatizo yao yanaanza kufanyiwa kazi na serikali inajidhatiti kulinda raisili mali iliziwanufaishe taifa; wao wakabaki na kebei bila kuja na mkakati madhubuti. Vyama vya upinzani, badilikeni muendane na matakwa ya wananchi na sio kuleta porojo zisizo na tija.
 
Wale wanaoendesha manunuzi ndo wajisachi na kujipangusapangusa. I believe chadema siyo ya mtu mmoja au wawili kwahiyo hata huyo anayesemwa kuondoka akiondoka, itapendeza coz struggle itakuwa imemshinda.
 
Viongozi wa chama hicho wanajitahidi sana kulipamba sanduku la marehemu/Jeneza kwa nje lakini ukweli wa mambo ni kuwa ndani kuna maiti, ambayo imepigwa dawa na ganzi ili isitoe harufu. baada ya muda mfupi mwili huu usipozikwa harufu itawaumbua kwa waombolezaji endapo hawatafanyia kazi ukweli huu mchungu.

Hivi karibuni wanachama waandamizi wa CHADEMA akiwemo mwenyekiti wa BAVICHA wamehamia CCM, wanachama waandamizi wa vyama vingine ikiwemo wabunge wanahamia CCM kwa kasi ya kutisha. ni wakati muafaka sasa kwa vyama vya upinzani hasa CHADEMA ambacho ni cha kikuu cha upinzani kujitafuta/kujisachi/kujipangusapangusa....hali ya mambo sio nzuri sana huko chumbani. amkeni haraka..........hizi taarifa za Mnyika kukihama CHADEMA SIO ZA KUPUUZWA. ZIFANYIENI KAZI. ATASAJILIWA NA TIMU PINZANI SIO MUDA MREFU.
Ni lini ulishasema chadema hali shwari??
 
Mbowe apumzike sasa ili CHADEMA ianze upya.Ukweli mchungu!
 
upinzani haupo kwenye vyama na wanachama wa vyama
upinzani upo vichwani mwa wananchi
who is mnyika? ni mtu mmoja tu
 
Tundu Lissu( King Jumong) aliisha sema, waoga wote lazima watalaza mishale. Watakaobaki upinzani, ni wale wasioogopa. Kwani unashangaa Mnyika kwenda ccm,?. Uoga humwingia Mtu yeyote wakati wowote. Chadema haiwezi kufa kama mnavyojidanganya. Chadema IMO ndani ya mioyo ya wapenda mabadiliko.
 
wapotee tu ili waje wapinzanzani wenye nia ya kweli na taifa hili.
[HASHTAG]#Maziko[/HASHTAG] ya kitaifa ya mbwa.
 
bac sawa. ngoja upinzani ufe ndyo mtajua unuhimu wa chama cha upinzani.
 
Back
Top Bottom