kingadvisor
Senior Member
- Dec 21, 2011
- 109
- 30
Kumekuwa na matamshi mengi kutoka CHADEMA kuwa CCM ni chama cha mafisadi.Hivi kama wana ushahidi kwa nini hawakipeleki mahakamani? Wanabaki kusema kwenye bunge ,mikutano ya hadhara na vyombo vya habari wakati mahakama zipo.Ni kwa nini kama kweli wamepania kusaidia nchi hawakipeleki CCM mahakamani? ukweli ukathibitike huko? Siamini kwa chama kinachoamini utawala wa sheria kinaweza kuishia kusema mafisadi kwenye press conference,mikutano ya hadhara na bungeni kikaacha kwenda mahakamani kama kinao ushahidi wa kutosha.Vinginevyo kama hakina kitabaki kinabwabwaja maeneo ambayo hakuna hatua ya maana inayoweza chukuliwa na kuiacha nchi ikiendelea kuumia.
Nadhani ni wakati muafaka wananchi tushinikize vyama na viongozi wa upinnzani,wa Dini na wale wa ndani ya CCM wanaoimba wimbo wa kuweko mafisadi tuwaambie kuwa kama wako serious wanaona CCM ni mafisadi na kuna mafisadi wanaowajua na wanaowataja majukwaani bila aibu wala kumeza maneno wakawafungulie mashtaka mahakamani vinginevyo binafsi nawaomba wananchi tuwaone kama wanasiasa wasioheshimu utawala wa sheria na waendesha siasa za maji taka wawe CCM au nje ya CCM maana mwizi haongelewi barabarani hukimbizwa hupelekwa polisi na baadaye mahakamani.Kila chama na kila mtu ana haki ya kisheria. Si haki hata kidogo kupiga yowe kwenye mabarabara kuwa fulani fisadi au chama fulani fisadi bila ushahidi wa kutiwa hatiani wa kimahakama hata kama una vipande vya magazeti ulivyokata millioni vilivyoandika tuhuma za ufisadi wao.
Kuanzia leo sisikilizi tena mtu au chama kiwe Chadema au CCM au chama chochotete kitakochosema kuna mafisadi popote kama hakiwapeleki mahakamani nitakiona au kumwona mtu huyo anayesema hivyo tapeli wa kisiasa na mwendesha siasa za maji taka ambazo haziwezi kuikomboa nchi hii.Nimechoka siasa za maji taka.
kingadvisor@yahoo.com
Nadhani ni wakati muafaka wananchi tushinikize vyama na viongozi wa upinnzani,wa Dini na wale wa ndani ya CCM wanaoimba wimbo wa kuweko mafisadi tuwaambie kuwa kama wako serious wanaona CCM ni mafisadi na kuna mafisadi wanaowajua na wanaowataja majukwaani bila aibu wala kumeza maneno wakawafungulie mashtaka mahakamani vinginevyo binafsi nawaomba wananchi tuwaone kama wanasiasa wasioheshimu utawala wa sheria na waendesha siasa za maji taka wawe CCM au nje ya CCM maana mwizi haongelewi barabarani hukimbizwa hupelekwa polisi na baadaye mahakamani.Kila chama na kila mtu ana haki ya kisheria. Si haki hata kidogo kupiga yowe kwenye mabarabara kuwa fulani fisadi au chama fulani fisadi bila ushahidi wa kutiwa hatiani wa kimahakama hata kama una vipande vya magazeti ulivyokata millioni vilivyoandika tuhuma za ufisadi wao.
Kuanzia leo sisikilizi tena mtu au chama kiwe Chadema au CCM au chama chochotete kitakochosema kuna mafisadi popote kama hakiwapeleki mahakamani nitakiona au kumwona mtu huyo anayesema hivyo tapeli wa kisiasa na mwendesha siasa za maji taka ambazo haziwezi kuikomboa nchi hii.Nimechoka siasa za maji taka.
kingadvisor@yahoo.com