CHADEMA "achaneni" na Dr.Slaa (Ushauri)

CHADEMA "achaneni" na Dr.Slaa (Ushauri)

Ukisoma katikati ya mistari mleta mada ana hoja, pro CDM punguzeni mihemuko mf. hilo suala la nyumba kwa nyumba ni mkakati mzuri ni kuona namna ya kuratibu jambo zuri kama hilo.
 
KAMA CCM inamhofu SLAA na wewe unashauri CHADEMA IACHANE naye ,kaangalie notes CCM walikuambia uandike nini HASA maana inaonesha kuna desa umepoteza!
 
Tukubali kutofautiana.Si kala mtu anayekushauri,ushauri ambao hukubaliani nao ni adui yako.Mimi sina matatizo na Chadema.Mimi sio mnafiki,na siogopi kusema kitu ninacho kiona kina ukweli.NAWAPENDA CHADEMA NDIO MAANA NAWASHAURI.Tunataka ukombozi wa nchi yetu,hatutaki kubadilisha sura tu.Chadema lazima ijipange vema ili kuongoza ukombozi tunaoutaka ambao ni mgumu zaidi kuliko enzi za ukoloni.Chadema kubalini kushaurika.Nchi hii ni yetu sote
Mkuu Mwankuga nimependa hiyo mstari wenye red hiyo imesimama sana nakubaliana na wewe.Lakini penye blue hapo nilitaka kukumbusha tu kwamba sifa kuu mbili za ushauri ni kukubalika ama kukataliwa,chadema haijakataa kushaurika,Ben katoa maoni yake naye kama mtu binafsi naye atakuambia kwa mapenzi aliyonayo kwa chadema,sasa ukilazimisha kama hapo kwenye blue manake wewe unajiona yadumu mashauri yako,hii ni hatari sana kwako kwani mashauri yanayodumu na kusimama ni ya Mungu tu,sasa labda uniambie wewe na Mungu mpo sawa,uwe na wakati mwema.
 
Aisee mleta uzi pole sana kwa mashambulizi kutoka kwa wabakaji wa demokrasia wa chadema. Wao hawaoni jema hata moja katika ushauri wako na hili linadhihirisha ujinga uliowajaa kumkichwani kwao. Kwa staili hii huo ukombozi mnaoudai mtaungoja sana labda mpaka Yesu arudi.
 
Umekosea ndugu ktk title yako, CDM ni taacc,kuna kina Silaa wengi ambao ni majembe kuliko unavyodhani,ila kidogo nimekuelewa hunania mbaya,wewe ni mtu mzuri tu.
:yell:
 
Tujadili hoja si mtu hembu tujadili mustakabali wa nchi yetu si jina la mtu au la chama fulani Je rasilimali zetu zinatumika ipasavyo kwa maendeleo ya Taifa?tujiepushe kumjadili mtu fulani binafsi naona haitasaidia tutaendelea na kasumba yetu ya kuwa watu wa kulalamika na kunungunika bila suluhisho la matatizo lukuki yanayoikabili nchi yetu,tujielekeze kujadili tutatoka vipi kwenye tawala hii dhalimu ya CCM na kuweka utawala mwingine safi utakaotuvusha kutoka hapa shimoni.
 
Una balaa ww, yaani unapendekeza mungu wa chadema atoswe?
 
Ulichotaka kusema hapa ni kwamba CHADEMA waachane na RAIS wetu DR SLAA, wewe utakuwa unasumbuliwa ule ugonjwa ambao anasumbuliwa chris lukosi, hatuhitaji ushauri dhaifu kama huu....
 
Back
Top Bottom