CDM na UTATU Mtakatifu katika Maandamano.

apolycaripto

JF-Expert Member
Feb 11, 2011
644
225
Shinyanga.jpg

Ni idadi nzuri kupagawisha katika Maandamano ya CHADEMA yaliyoishia kiwanja hiki katika Manispaa ya Shinyanga.Je! hawa ni utatu mtakatifu katika kukamilisha ibada (Wapiga kura wenye kuiunga mkono CHADEMA na wako tayari kutekeleza kauli ya CHAMA) ama UTATU huu KATIKA MAANDAMANO na MKUTANO una sura hii:

1.Wanachama (wanaojulikana)- Asilimia kubwa ni wapiga kura
2.Watoto (huwa ni wengi na idadi yao kutojulikana)-Hawapigi kura
3.Wasikilizaji (Wasio wanachama wa CDM) uvutwa na ushereheshaji,wengine kupenda kumuona ama kusikia anasema nini!(Kundi hili ni wengi na idadi yao kutojulikana)-Vigumu kutambua wamempigia nani kura mpaka baada ya Matokeo.

Naomba tupewe takwimu ili tujue kama kunafursa ya uungwaji mkono hapa ama ni usikilizaji tu.Manispaa ya Shinyanga inawakazi wasio zidi 200,000 na waliopiga kura ni 40,257 katika uchaguzi uliopita.Kwa kawaida kundi la watu 1000 huwa ni kubwa nalo pia la kupagawisha.Tunahitaji takwimu kuwa hawa wanakisiwa kuwa wangapi?Unaweza ukahesabu tu kwani upande huu uliopigwa picha ndio wenye wengi kisha uka-estimate kwa ambao hawako kwenye picha ama uhakika ni kupata takwimu halisi toka kwa Wenzetu waliokuwa katika Mkutano na wakweli pasipo ushabiki(mara nyingi upoteza taaluma za watu).

Tunahitaji kujua hili kundi kama ndilo lenye kuleta mabadiliko kwa maana ya " utatu mtakatifu" katika maeneo yote CDM iliyopita ama Wengi katika kundi la "utatu mtakatifu" mahudhurio yao ni kusikiliza DOWANS na skendo nyingine,kuafiki ama kutoafiki wengi ubakia siri yao!

Lengo la tathmini hii ndogo ni kuondoa ama kukuza kiwewe cha KIKWETE juu ya uungwaji mkono kwa CHADEMA vile vile kutopumbaza viongozi wa CDM kudhani wanaWafuasi wa kutekeleza AMRI siku 9 zitapo kwisha.

Tahadhari: Lugha chafu zenye kilevi kwa baadhi ya great thinkers zinaaibisha hiki kituo cha Intellectuals na kufanya kutokuwa tofauti na lugha za vilabuni (matusi).
 
Mkuu baada ya kuandika ujinga unategemea utakemewa ndo maana nusu ni mada nusu ni onyo kwa atakayesoma post yako. Mi nachukia kauli za uchochezi. Ikumbukwe Rukwa walioikashifu imani ya kikristo waliadhibiwa,juzi wachungaji wa Arusha waliodaiwa kukashifu uislam wameadhibiwa,na wewe unaleta kauli za kashfa,UTATU MTAKATIFU! Najiuliza asa kama una lengo jema iweje ulete utatu mtakatifu? Sichangii tena mada kama izi za kukashifu imani na kulinganisha utatu/ Holy Trinity,na viumbe alivoviumba Mungu mwenyewe. Nakushuku,safari njema ktk kuwagawa watz kwa imani zao,mi nashuka hapa mkuu!!!
 
juzi tulikuwa tuko kwenye kuanzisha tawi la chadema mtaa mmoja ambapo watoto waling'ang'ania kuwepo na kusikiliza kwanini chadema ni chama kinachofaa kupewa dola. kigezo cha watoto hava ni kwamba ndani ya miaka minne hadi mitano ijayo watakuwa na umri wa kupiga kura na hivyo kuichagua chadema!

chadema songa mbele!
 
Utatu mtakatifu ni nini na inahusiana nini ni huu upuuzi wako ulioandika? Acha kufuru!
 
Umetumwa wewe. Unaleta kufuru zenu za CCM kwa UKRISTO katika JF? MUNGU akulaani na mpango uliotaka kuutekeleza kwa kuichafua CHADEMA ufe.

AMINA.
 
Pesa walizopewa kwenye uchaguzi hawana jinsi ya kuhalalisha kushindwa kwao. Umamluki hatari.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom