mzalendokweli
JF-Expert Member
- Apr 21, 2012
- 579
- 137
Kwamba alikua hana hata nauli yakwenda dodoma!!?? huo uongo sasa. Huyu ni mume wa jaji mfawidh mahakama kuu kanda ya Arusha atakosa nauli kuja dom kweli?
Mbunge mteule wa A.Mashariki Makongoro Nyerere amesema kura za wabunge wa CDM ndizo zilimfanya kushinda ubunge huo.Makongoro amesema wagombea wenzake kupitia CCM walitishia ushindi wake kutokana na jinsi walivyokuwa wanatembeza rushwa.
Makongoro amesema alikuwa hana hata nauli ya kwenda Dodoma lakini alimtegemea Mungu.Amesema CDM walipotaka kususia uchaguzi ule aliamini mwisho wake ulikuwa umefika kwani kura zote za wabunge wa CDM zilikwenda kwake.Amesema ni ngumu sana kugombea nafasi yoyote kupitia CCM kama huna hela za kugawa.Makongoro ameendelea kusema kwamba chuki ya rushwa waliyo nayo wabunge wa CDM ndiyo iliyomuokoa kwani anaamini ni vigumu wabunge wa CDM kuchagua mtoa rushwa.Amemalizia kwa kusema shukrani yake kwa CDM ni kwa yeye kuwatumikia wananchi wote bila ubaguzi wowote.
SOURCE:TANZANIA DAIMA
Waziri anashiriki kugawa rushwa, bwana mkubwa anaona ni upepo tu ambao utapita. Makubwa haya!