hapo ccp mbona kuna uoza mkubwa sana zaidi ya hao makuruta feki,IGP saidi mwema ana tenda ya kulisha mikate kila siku kutoka kwenye kiwanda chake pale mashenzini njoro, kwa wanoifahamu moshi vizuri njoro haina tofauti na mitaa ya kibera kule kenya.
Hivi sasa wanafunzi ambao hawana sifa bado wanaendelea kumiminika kwa wingi pale ccp kwa sababu ya askari waliojigeuza kuwa mawakala wanachukua fedha na kumpelekea mkuu wa chuo mbushi matanga ambaye ameunda mtandao mkubwa wa kuingiza wasio na sifa kila mtu aliyepo moshi anafahamu hilo.
Sasa nani atamfunga paka kengere?,kama IGP analisha mikate kila siku hapo na mbushi anapokea fedha za wanafunzi wasio kuwa na sifa,sasa hawa wote si wezi kama wezi wengine?,wataacha kulindana?
kwa anayebisha atafute askari wa jeshi la polisi pale moshi amwambie nina kijana wangu anataka kwenda CCP,vipi utaratibu ukoje?,atakujibu subiri kwanza nitakujulisha,baada ya muda mfupi atakuuliza unazo laki saba?,atakupa na mchanganuo wa hizo laki saba,ccp ya sasa ni bure tu hata ile ya kina changoja ni bure,maana hata wauza baada waliokuwa karibu na kija chagonja walikuwa wanaingia ccp kiulainiiiiiiii,na wapo mpaka leo wanazidi kupanda vyeo,