CCM yatafuta kick Moshi


Mimi huwa nakemea wote. Nakumbuka wako wana-CCM waliokuwa (wakati wa kampeni) wanamtukana Lowassa kwa matusi makubwa, kwa mfano, kuwa 'anaji....' mimi nilikuwa nawakemea humu JF. Kimsingi naichukulia JF kuwa ni sehemu ya kupashana habari na kuelimishana na siyo sehemu ya kuonyesha ujuzi wa matusi. Binafsi sipendi matusi. Kwa bahati mbaya wapo vijana wengi nchini mwetu wasiojua kabisa historia ya nchi hii. Wengi wamekulia katika Enzi hizi za mfumo wa vyama vingi vya siasa na wanadhani kuwa matusi ni sehemu ya demokrasia. Inasikitisha kweli kweli kuona kuwa wako ambao wanajaribu hata kumtukana 'Head of State'. Tena bahati mbaya ilioje kuona kuwa wanaoendesha matusi wamo wanasiasa wa pande zote mbili, CCM na upinzani, na wasijue kuwa tunajenga misingi mibovu ya kukosa uzalendo, heshima na busara kwa kizazi hiki na kwingineko. Yaani uhuru wa kutoa mawazo tulio nao nchini mwetu unachukuliwa kuwa ni tiketi ya kuwadhalilisha viongozi wetu na jamii yetu kwa ujumla. It is a shame... Ndiyo maana mimi nasema aje mtu afanye kosa na kuniambia uso kwa uso kuwa mimi ni shoga, nadhani huo ndio utakuwa ni mwisho wa chapter...
 
teh teh teh

pale stendi ya Moshi kuna vinywaji kinaitwa Ndizi kuku ..... yaani banana na kiroba jogoo
 

1954;
Mkuu naona umeandika kwa uchungu kweli kumwonya huyu mtoto. Sawa kabisa, ila najua weye ni ccm dam dam, si mbaya nia haki yako. Ila ulipokosea ni kule kusema ati, huyu kijana (mtoto) hajui walio ijenga hii nchi.
Ama kweli, nyani haoni kundule. Inakuwaje mtu kama weye kuweza kutamka neno hilo? Weye ulizaliwa ccm?? CCM ndo babako na mamako?? Hakuna mwenye haki ya kusema ati ndo aliijenga nchi hii. Hayupo. Uliijenga nchi, ilikuwa imebomoka??
Kila mtu anahusika na Tanzania. Waliouomba uhuru hawapo tena, hata weye hukuijenga nchi. Waache watu wajisemee watakavyo kwani HAKUNA NAMNA TENA. iLIPOTUFIKISHA CCM TUNAPAJUA. Miye sina chama, ila naumia ninapoona watu wakijihesabia haki. Watu wenye mawazo ka yako wanajiona kuwa ndo wanajua hata saa ambayo mimi natakiwa kulala.
Nilidhani ungejikita kwenye mada. CCM wakiratibu maandamano hata kama ni ya kwenda Ikulu, intelijensia inaona usalama. Chama kingine chochote kikiratibu maandamano, hata kama ni kwenda Pugu mnada wa ng'ombe, intelijensia inaona kuwa ng'ombe wataanguka kifafa.
Haya, waacheni waandamane mpaka Stand kuu ya mabasi, kando tu ya kituo kikuu cha Polisi, ila polisi siku hiyo hawatakuwa na hofu yeyote bali watawapa hata brass band.
Mku hilo lichama lishajifilia lenyewe. JPM hana haja ya kuombewa Stand kuu ya mabasi. Kwanza pale ni usumbufu hata malaika anayepokea maombi hatasikia. Pale kuna dini sijui 7 zimeizunguka ile stend kama jografia yangu ya Moshi haijapotea sana. Sasa ni kiongozi wa dini gani mtakaye mlipa kitu kidogo. Kwaheri, ila usiache kutuletea mrejesho
 
Uhuru huu ukipotea...
Uhuru huo ni haki ya kikatiba au unatolewa kwa hisani? Waliomwita Lema shoga walikuwa kina nani kama si wana CCM? Huo mshikamano wa taifa unapotea kwa CCM kuitwa chama cha Mashoga ila CHADEMA wakiitwa chama cha Wakatoliki na wachaga ni sawa, au CUF wakiitwa chama cha Wapemba na waislam ndiyo amani inadumishwa?
 
kwani Magembe na mathayo was chama gani
 
Nijuavo ndugu zangu wa kaskazini hawana muda wa mikutano au maombi yasiyo na tija.wako bussy kutafuta pesa
 
Ujue kumbe mtu kumlk smartphone sio kua na akil timamu sasa lowasa washukuru nn watu wakat hajashnda au kwasababu n darasa huru bas kila mtu anaandka tu afu et ccm nchi nzima bas mngekua na wabunge weng ukawa achen utoto kuen na mawazo endelevuuuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…