CCM yapendekeza Samia urais hadi 2035

CCM yapendekeza Samia urais hadi 2035

Lakini katiba inasema kama ameupata urais mtangulizi wake akiwa hajafikisha nusu ya muhula basi ataruhusiwa kugombea kipindi kimoja tu, maana yake kama Magufuli angekuwa amefikisha miaka miwili na nusu katika ile mitano ndiyo angeruhusiwa kugombea awamu mbili. So kwa mujibu wa katiba haruhusiwi.
 
Ila kuna watu wanataka tu kuiua Tanzania. Hata hawana huruma na hii nchi. Tanzania is getting worse everyday because of Samia, ila bado CCM mnataka aongoze hadi 2035

Lengo ni nini, tuendelee kutukanana mitandaoni, au tuendelee kuishi na manung'uniko au utekaji uendelee, au udini ukue, au ufisadi uongezeke yani mnataka Tanzania ife au?
 
Nyerere alitawala miaka 23 na ktk miaka yote hiyo serikali zake zote ziliitwa awamu ya kwanza unajua ni kwa sababu gani?
Wewe katika kuhalalisha Jambo lenu umesema alikuwa anamalizia awamu ya Magufuli. Hiyo ilikuwa awamu ya tano raisi wa tano.
Kabla uchaguzi 2025 mlikataa hiyo hoja mkamuita raisi wa sita na awamu yake ya sita. Hamkutaka iitwe awamu ya tano raisi wa sita, kwamba uraisi awamu ya tano umemaliza awamu zote mbili.
Lengo apate nafasi ya kugombea
Mlisahau kuna kesho atataka apate mihula yake miwili ya uraisi wake pekee?
 
Kwa kazi ngumu aliyofanya kupambana na wahalifu waliochoma na kuiba mali za watu Oct 29 ni kweli kabisa anastahili kugombea hadi 2035.

Kwanza ile awamu iliyopita ilikua ameshikia tu haikua yake , awamu yake ya kwanza ndo hii.

Kama kuna nyumbu anabisha atoke barabarani kuandamana sahivi tumpokee vizuri.
 
Lakini katiba inasema kama ameupata urais mtangulizi wake akiwa hajafikisha nusu ya muhula basi ataruhusiwa kugombea kipindi kimoja tu, maana yake kama Magufuli angekuwa amefikisha miaka miwili na nusu katika ile mitano ndiyo angeruhusiwa kugombea awamu mbili. So kwa mujibu wa katiba hafuhusiwi.
Ila Kipindi hiki ni kama hakugombea 🐼
 
Ukweli ni kwamba siioni future ya kizazi Cha Tanzania kwa miaka mingine ijayo....

Just imagine, hii nchi imefika hatua ya kudeal na vitu rahisi rahisi, uchawa uchawa tu daily, unafiki unafiki, kujipendekeza jipendekeza...

Sishangai kinachoendelea, haina shida msiogope msiseme atagombea mpaka 2035 semeni... Huyo ndio kiongozi wa Maisha hata akiondoka tutaweka jiwe liendelee kuwa madarakani...
 
Back
Top Bottom