CCM yameguka

Mwiba

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2007
Posts
7,607
Reaction score
1,760
Hayawi hayawi yamekuwa habari za ndani kabisa zunadai CCM imeshameguka na kuna mivutano inayotokana na makundi na mitandao inayoelekea kutaka kuweka mtu wao kugombea Uraisi ,Kumbe ile mbinu ya Kinana na Nape kuzunguka nchi ni moja ya mbinu na mikakati ya kujijenga mmoja kati yao ni mgombea mtarajiwa ,tayari wameshasitukiwa na ziara zao zimeanza kupigwa mikwala na kutiliwa shaka kwa sababu za kufanya ubadhirifu wa hela za chama na pia kutumia baadhi ya mambo na vifaa vya serikali ikiwemo magari.

Na waliondani wamesema sasa hivi hali ni mbaya kifedha ,pia kumekuwa na kudharauliana na kubaguana ,pia kuna baadhi ya vigogo huenda wakatimkia vyama vingine vya siasa ,wakikiacha CCM kikiwa kwenye mtafaruku.
 
Acha kife kabisa, CCM ni pepo mfilisi wa nchi yetu. Naona mungu anataka kutuondolea hili pepo.
 

Kinana anawatoa makamasi,..mtaisoma,namba mwaka huuu
Kinana kanyaga twende Comrade
 
Huu muda mnaopoteza kuishambulia CCM.
Imarisheni UKAWA, waambieni na wananchi kwanini wawaamini, na waulizeni kwanini wanawaona ni matapeli. CCM sio saizi yenu.
 
Mzee wa Gombe hilo ndo kundi lake.

Ila tuwaache wafu wazikane.
 
Kumbe JF watu wana njaa kiasi hiki cha kuamini cheap propaganda?what's the different ya hii article na ma group ya facebook ya adolescents wa sekondari?
 
Huu muda mnaopoteza kuishambulia CCM.
Imarisheni UKAWA, waambieni na wananchi kwanini wawaamini, na waulizeni kwanini wanawaona ni matapeli. CCM sio saizi yenu.

Hivi wewe huwa huna Ajira nyingine?
 
Habari nusu hii kwa sababu CCM kuna makundi makuu matatu; kundi la Lowasa, la Membe Na la Sita.
sasa we unazungumzia kundi gani? Na lipi linataka kumeguka Au kuna labda kundi jipya?
Mkuu toa ufafanuzi
 
Jamaa atakua ameamka kutoka usingizini na hiyo ndio ndoto aliyoiota.
 
Ccm ni moja, wanachama na viongozi wake ni wamoja na watadumu katika umoja huo. Mleta mada pamoja na vibaraka wenzako Endeleeni kuishi kwa uzandiki,uongo na uzushi 2015 hiyooooo itawaumbua
 
Kumbe mtu anaweza kulala saa 6 mchana na akaota ee..hatari sana hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…