KAMA KUNA MTU BADO ANAKUMBUKA OMAR MAHITA NA 'TOROLI YA VISU VYENYE TOMATO SAUCE', KILE KINACHOITWA 'UGAIDI' JIJINI ARUSHA UNA MALENGO YA KISIASA KUGAWA JIJI HILO KIDINI KUNAKOELEKEA UCHAGUZI WA MADIWA. WaTanzania wala tusipumbazwe kama mazezeta hivi; hakuna cha(1) Sheikh Ilunga, (2) Al-Shabaab, (3) Al-Qaeda wala nani anayewadhuru wananchi kwa malengo ya kuleta hofu na hali ya kutokuaminiana kati ya Wakristo kwa Waislamu nchini. Kwa kufuatilia matukio ya 'Ugaidi wa Kuchonga' na matukio ya hivi karibuni jijini Arusha lazima ujiulize kwamba kati ya watajwa watatu hapo juu na (4) Serikali ya CCM, ni yupi kati ya wote mwenye kuweza KUNUFAIKA kisiasa na ulipuaji ovyo wa mabomu A-Tauni??????? Na kwa mtindo huo ndio maana kati ya michango yote juu ya tukio hili la kusikitisha sana, hakika nimeweza kumtambua mwenzetu huyu, Mkuu Lyamunda, kuwa kweli ni great thinker mwenye uwezo mkubwa kuona ujumbe ilioko nyuma ya ujumbe unaoonekana wazi kwa kila mtu. Ni masikitiko yalioje kuona jinsi gani serikali ya CCM inavyotumia dhana ya 'Ugaidi' kwa maslahi kisiasa kwa mtindo ambao sio kabisa. Wakristo kwa Waislamu kote nchini, tafadhalini kaeni mbali sana na hizi mbinu chafu za CCM na serikali yake kutumia hizi mbinu za ki-Nazi kutafuta kutugawa kwa misingi ya kidini kwa kutumia silaha yao mpya ya 'Ugaidi unaosimamiwa na vijana wake'.