Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,615
Habari za Uhakika zinasema kuwa, viongozi wooote waandamizi wa CCM hivi sasa wapo kwenye mkakati madhubuti kuhakikishisha kuwa Dk Slaa hafui dafu kwa JK.
CCM imeshtushwa kwa kiwango cha juu kukubalika kwa kiasi kikubwa kwa Dokta Slaa na Chama chake.
Moja kati ya Mikakati iliyowekwa ni kuhakikisha pesa inamwagwa kama njigu kwenye "maeneo korofi" kisiasa
Pia vyombo vya habari vyote isipokuwa Tanzania Daima vitatumika kueneza propaganda ya uwongo dhidi ya Mgombea huyo wa CHADEMA.
Imeelezwa kuwa katika mkakati huo wa kummaliza Dokta Slaa ambaye hadi sasa Mkutano Mkuu wa Chama chake hauja mpitisha kugombea Urais, watapenyezwa Mamluki wengi kutoka CCM na miongoni mwao ni wale walioshindwa ubunge kupitia kura za maoni.
Mtoa habari muhimu na anayeaminika alisema, yapo maeneo maalum ambayo wagombea ubunge wameonekana "kushindwa" lakini kiuhalisia hawakushindwa bali ni mbinu chafu ya kuwahadaa watanzania kwa kutaka watu hao wahamie CHADEMA ili wavuruge.
Ujio wa ghafla wa Mabere Marando CHADEMA pia unahusishwa na mkono wa CCM.
Ukimya wa CCM hivi sasa si wa kupuuza.
Katika hatua nyingine, moja kati ya propaganda zitakazoenezwa ni maisha binafsi ya Dokta Slaa, ya Kifamilia na ya Kiimani pia.
Wito wangu: Wanachadema wawe tayari kujibu mapigo.
CCM imeshtushwa kwa kiwango cha juu kukubalika kwa kiasi kikubwa kwa Dokta Slaa na Chama chake.
Moja kati ya Mikakati iliyowekwa ni kuhakikisha pesa inamwagwa kama njigu kwenye "maeneo korofi" kisiasa
Pia vyombo vya habari vyote isipokuwa Tanzania Daima vitatumika kueneza propaganda ya uwongo dhidi ya Mgombea huyo wa CHADEMA.
Imeelezwa kuwa katika mkakati huo wa kummaliza Dokta Slaa ambaye hadi sasa Mkutano Mkuu wa Chama chake hauja mpitisha kugombea Urais, watapenyezwa Mamluki wengi kutoka CCM na miongoni mwao ni wale walioshindwa ubunge kupitia kura za maoni.
Mtoa habari muhimu na anayeaminika alisema, yapo maeneo maalum ambayo wagombea ubunge wameonekana "kushindwa" lakini kiuhalisia hawakushindwa bali ni mbinu chafu ya kuwahadaa watanzania kwa kutaka watu hao wahamie CHADEMA ili wavuruge.
Ujio wa ghafla wa Mabere Marando CHADEMA pia unahusishwa na mkono wa CCM.
Ukimya wa CCM hivi sasa si wa kupuuza.
Katika hatua nyingine, moja kati ya propaganda zitakazoenezwa ni maisha binafsi ya Dokta Slaa, ya Kifamilia na ya Kiimani pia.
Wito wangu: Wanachadema wawe tayari kujibu mapigo.