CCM Yajenga Nchi!

CCM Yajenga Nchi!

Ndugu wana jf.. ingawa kuna baadhi ya watu wanajitahidi kukichafua chama cha mapinduzi na kukifanya kana kwamba hakijafanya chochote tangu kishike dola. Lakini embu angalia data hizi..Kimefanikiwa kuilinda mipaka ya nchi na kudumisha amani ndani ya nchi..Kimefanikiwa kujenga shule mpya za sekondari takribani 1000 pamoja na kuzifanyia ukarabati zile kuukuu. kimeunganisha huduma za barabara kwa mikoa na mkoa wa DSM ambako ndiko lango kuu la uchumi lilipo..huduma za umeme na nishati mpaka kule vijijini pamoja na mitandao ya kimawasiliano na mengine kemkem.. kama vile upatikanaji wa maji kwa kiasi kikubwa.. CCM yajenga nchi bwanaa
 
Yajenga nchi kwa kuuza tembo? Yajenga nchi kwa urichmond? Yajenga nchi kwa wanafunzi kufeli? Yajenga nchi kwa maisha magumu?
YOU MUST BE CRAZY
 
wanabodi piteni hapa hakuna cha kujadili wameishiwa sasa wanatapatapa
 
kitajendaje nchi wakati rais anaishi angani na airport
 
Risala fupi ya marehem CCM: Marehem CCM alizaliwa 05/02/1977.Enzi za uhai wake marehem alijishughulisha na kuua mazao ya biashara km pamba,tumbaku,kahawa,korosho na katan. Marehem pia atakumbukwa kwa kaz kubwa aliyoifanya kwa bidii ya kuua viwanda km Mwatex,Mutex,Kiltex,Ufi,Bora Tanelec, Mgololo,Tanganyika packers,viwanda vya maziwa.Pia aliwaleta na kuwapa wagen mali za waTZ.Ameacha wachina kariakoo,waarabu loliondo,makaburu mererani na wazungu wa kila aina kwny migodi yote ya madini na gesi.Marehemu ameacha mke m1 aitwaye (CUF) na watoto wawili.UDP na TLP.Shetani amuweke pabaya moton milele Amen.
 
Tangu miaka ya 80 nilipojiunga na CCM,kauli mbiu yetu ilikuwa 'CCM yajenga nchi'. Kauli hii tuliambiana,tuliimbiana,tuliandikiana na kukumbushana.Tena kimatendo. Lakini sasa ni tofauti.CCM haijengi tena nchi. Kujenga nchi, kwa uelewa wangu, ni kusikiliza wananchi,kuwahudumia na kuwafanya wawe wamoja.Kufanya mambo ya kimaendeleo pamoja.

Kujenga nchi ni kuheshimu maoni ya wengine,changamoto mpya na kuzikabili kiutatuzi ili mambo ya nchi yaende mbele. CCM sasa haijengi nchi.Haisikilizi wananchi wake. Haiwaheshimu wananchi wake na kuwafanya wamoja. Inawatawanya makusudi ili kuendelea kubaki madarakani. Mbinu hii ni chakavu na itashindwa hima. CCM ile ilikuwa ikijirudi haraka na kusonga mbele.Hii ni tofauti. Haiambiwi;haisikii.

Hebu tutupe macho kwenye uandikaji wa Katiba mpya. CCM,yenye asilimia 99 ya Wajumbe wa Tume ya Katiba,imefikia kuibishia Tume na watanzania kwa ujumla. Inataka mawazo yake tu yaheshimiwe.Kwamba,kuwe na Serikali mbili na Mawaziri wawe Wabunge. Imeandaa nyaraka yake na kuwalazimisha Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya waiseme nyaraka kama ilivyo.Huku ni kuvuruga nchi.

Leo,CCM imekiuka hadi Sheria za kimataifa.Imemtumia Balozi wa China nchini kukinadi chama. Kidiplomasia,hata Waziri Bernad Camilius Membe anaweza kushuhudia, Balozi huiwakilisha nchi yake katika nchi nyingine.Balozi ni wa kitaifa na wala si wa kichama. Kumtumia kwa namna yoyote Balozi yeyote katika mikutano ya kichama,ni ukiukwaji wa sheria husika na ni kuwagawa wananchi katika minajiri ya kichama. Ni kuvuruga nchi.

Kwa leo naishia hapa. Nikihitajika kwa mjadala zaidi nitakuwa 'around'.Ijulikane kuwa sasa CCM haijengi nchi;inavuruga nchi. Ni dalili mbaya kisiasa.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.
 
Na uvurugaji huu utaliingiza taifa vitani mda si mrefu,

Napata shaka nakuanza kuamini maneno ya mitaani kuwa shughuli za tindikali nchini zina ratibiwa na ccm kwa madhumuni hayo hayo
 
Back
Top Bottom