CCM Yajenga Nchi!

Duduwasha

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
5,703
3,653
Nyimbo Hizi Nazikumbuka Tuliimba sabahu tulizikuta tukaimbishwa huku hatujui anayejenga nchi ni nani

Tokea Nchi imeanzwa kujengwa na sasa inatimiza Miaka hamsini bado haijaisha nadhani hata makao makuu ya Magereza Ohio Street yanaweza kuwa ni kati ya majengo machache yaliyojengwa kwa Muda mrefu sana i mean Miaka mingi sana hadi kukamilika nadhani walianza kujenga miaka ya 80s na 2011 ndio lipo ukingoni kuisha sijui kama hiyo finishing itamalizika lini Shukrani wahindi wanaomalizia... Jengo limejengwa hadi na Wafungwa..

Kuna mambo mengi yanayocheleweshwa kujenga nchi aidha kwa uzembe au watu wamekula pesa za bajeti so wanasubilia bajeti ya mwaka unaofuatia wale kidogo kisha wajenge kidogo, barabara zetu zimejaa mashomo yanasababisha magari yetu kuharibika hasara zinaenda kwa wananchi bora magari pikipiki ndizo zinaathirika zaidi na mashimo ya barabarani na kutishia maisha ya watumiaji.
hakuna fungu la ukarabati wa barabara zetu au ndio ufisadi na viongozi hawana uoga kwani ni wanachama wa magamba hawatawajibishwa sera kulindana na hakuna msafi wa kumnyooshea mwenzake kidole.

Airport yetu ni chafu imejaa vibada vya ovyo ovyo, haieleweki! office za ajabu zipo sehemu za abiria na wasindikizaji zimebana
katika siku za furaha enzi za Mwalimu, ilikuwa kwenda kutembelea airport DSM summit unatizama ndege za aina aina zikitua na kupaa kule juu hadi maharusi walikuwa wakienda kujifurahisha. yasikitisha hali ya sasa hatujui tunaenda mbele au nyuma. we need change before change changes us.

Kikwete turejeshee nchi yetu mapema kama uraisi ndio ulikuwa unautaka ushaupata najua au watu wanasema ni maamuzi magumu mi sioni ugumu wowote fanya uweke nchi irejee na heshima yake naomba japo tu hapo airport me huwa nasikia kinyaa jinsi palivyo.
Wajisikia vipi nchi ikiwa katika hali hii kila raia anahuzuni na nchi yake munung'uniko inazidi kuwa mingi hadi wakupendao hali zao za ushabiki zinawashinda sikuhizi muondoe ngeleja umeme unachukiza wengi kashindwa vitendo ila kwa maneno yupo mzuri Umeme Tanzania itakuwa historia damn! bul shait!

Maji salama umeshindwa, barabara umeshindwa kwa pesa zetu so zinajengwa kwa misaada ya nje ambayo itatugharimu baadae kudhibiti wezi wakubwa wanaosababisha hali duni no actions dah! me nimechoka nitakuja siku nyingine nimalizie
 
Nimeukumbuka ule wimbo tulikuwa tunaimbaga shuleni 'chama chetu cha mapinduzi chajenga nchi chama chetu cha mapinduzi cha jenga nchi' na sie tulikuwa tunaimba chai chapati marage mchuzi chajenga nchii ' wakati tunaimba nilikuwa nahamasika na kuamini kuwa ccm kweli inajenga nchi je wenzangu mlikuwa mna hisia gani wakati huo tukiwaimbia viongozi na walimu shuleni!!!
 
Zilikuwa hisia za matumaini lakini ndo mpaka leo hamna kitu kilichofanyika.
 
Nasema sitaki, narudia, sitaki kusikia CCM yajenga nchi hata kama ni kibwagizo cha miaka ya '47'. CCM ife kifo cha mende, inshallah!
 
Sitaki kusikia CCM inasagiwa, wote tumefika hapa kwasababu ya chama chetu, CCM. Ninataka niwakumbushe kuwa CCM ni chama cha kitaifa cha Watanzania, ni lazime tujikumbushe kujivunia kilicho chetu, mimi ninapata "goose bumbs" za furaha ninaposikia kuwa CCM inajenga nchi, CCM ilijenga nchi na inaendelea kujenga nchi. Wakati ilikuwa ni TANU ilituletea uhuru, ikatuunganisha na kuimarisha umoja wa kitaifa (nation state), baadaye kwa siasa za ujamaa na kijetegemea chama kilidhibiti misingi ya uchumi, na wakati ulipofika kikaruhusu uhuru wa kisiasa (liberalization). Hivi sasa chini ya kipenzi cha wananchi walio wengi, Baba Mlezi wa Taifa, Nuru yetu ya Maendeleo, Mhe Dr J. M. Kikwete tunaelekea kusherekea miaka 50 ya uhuru. Kweli kama siyo CCM tungekuwa wapi leo sisi Watanzania? KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI, ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA VIONGOZI WETU WA CCM.
 
Nasema sitaki, narudia, sitaki kusikia CCM yajenga nchi hata kama ni kibwagizo cha miaka ya '47'. CCM ife kifo cha mende, inshallah!
INABIDI TUWAFUNDISHE WANETU MASHULENI NYIMBO ZENYE MAANA. Hiki sio kizazi cha NDIO MZEE TENA au kidumu chama cha majambazi! Baadae kidogo tu watoto wataanza kututia bakora kwa kushabikia chama cha majambazi.
 
Sitaki kusikia CCM inasagiwa, wote tumefika hapa kwasababu ya chama chetu, CCM. Ninataka niwakumbushe kuwa CCM ni chama cha kitaifa cha Watanzania, ni lazime tujikumbushe kujivunia kilicho chetu, mimi ninapata "goose bumbs" za furaha ninaposikia kuwa CCM inajenga nchi, CCM ilijenga nchi na inaendelea kujenga nchi. Wakati ilikuwa ni TANU ilituletea uhuru, ikatuunganisha na kuimarisha umoja wa kitaifa (nation state), baadaye kwa siasa za ujamaa na kijetegemea chama kilidhibiti misingi ya uchumi, na wakati ulipofika kikaruhusu uhuru wa kisiasa (liberalization). Hivi sasa chini ya kipenzi cha wananchi walio wengi, Baba Mlezi wa Taifa, Nuru yetu ya Maendeleo, Mhe Dr J. M. Kikwete tunaelekea kusherekea miaka 50 ya uhuru. Kweli kama siyo CCM tungekuwa wapi leo sisi Watanzania? KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI, ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA VIONGOZI WETU WA CCM.
UNAHITAJI MAOMBI HUYO PEPO MCHAFU AKUTOKE!! Hana tofauti na yule anaefanya watu wale mavi!! Kweli mjinga atashabikia ujinga na matokeo yake ni ya kijinga kama tunavyoona Tanzania
 
Nasema sitaki, narudia, sitaki kusikia CCM yajenga nchi hata kama ni kibwagizo cha miaka ya '47'. CCM ife kifo cha mende, inshallah!
INABIDI TUWAFUNDISHE WANETU MASHULENI NYIMBO ZENYE MAANA. Hiki sio kizazi cha NDIO MZEE TENA au kidumu chama cha majambazi! Baadae kidogo tu watoto wataanza kututia bakora kwa kushabikia chama cha majambazi.
 
Ni muada wa wale waliokuwa wakitamba kuwa CCM yajenga nchi kipindi caha uchaguzi,wajitokeze na kuimba wimbo huo tena ili wajione walivyo wasindikizaji wa wenye CCM ambao sasa wapo nje wanakunywa wine na waliobaki wakitoa majibu ambayo leo yanasababisha waliokuwa wanaimba CCM ina wenyewe.

Mnaonaje wana JF KWA HILI?
 
thubutu! Sasa hivi kila mtu anajidai hakuipigia ccm kura, ila mpaka ifike 2015 wengi wao watakua wamekufa kwa presha na magonjwa ya moyo kutokana na maumivu ya majuto ya kuichagua ccm
 
Wanaoimba ivo hawajasoma uzi wako. Hawana umeme, hawajui tivii wala redio, sembuse intaneti!!!
soo tangazo au ujumbe wako haujawafikia.
 
Kumchagua JK ni janga la kitaifa:maneno yaho yalisemwa na Dr W Slaa kipindi cha uchaguzi wa 2010 kaulihii ina macho na ililenga mbali lakini watuhawakumwelewa sasa watanzania wanavuna ubishi wao zaidi ya kukosa dawa hata huyo Daktari tu hawamuoni wakirudi nyumbani kumpikia uji mgonjwa sukari tsh 3000 patamu kwelikweli mgonjwa atapona?
 
Wanaoimba ivo hawajasoma uzi wako. Hawana umeme, hawajui tivii wala redio, sembuse intaneti!!!
soo tangazo au ujumbe wako haujawafikia.

Hii nimeipenda, absolutely valid statement and like all valid statements in logics is capable of verification. Ahsante mkuu.
 
Hadi 2015 vijana wengi sana watapiga kura. Wale mateja wa ccm siku hizi wamejanjaruka. Mwaka juzi nilisimamia upigaji kura huko kijijini, mtu analetwa hajui anaenda kumchagua nani anaye jua ni yule anayempeleka akapige kura.
 
Ndugu wana jf.. ingawa kuna baadhi ya watu wanajitahidi kukichafua chama cha mapinduzi na kukifanya kana kwamba hakijafanya chochote tangu kishike dola. Lakini embu angalia data hizi..Kimefanikiwa kuilinda mipaka ya nchi na kudumisha amani ndani ya nchi..Kimefanikiwa kujenga shule mpya za sekondari takribani 1000 pamoja na kuzifanyia ukarabati zile kuukuu. kimeunganisha huduma za barabara kwa mikoa na mkoa wa DSM ambako ndiko lango kuu la uchumi lilipo..huduma za umeme na nishati mpaka kule vijijini pamoja na mitandao ya kimawasiliano na mengine kemkem..
 
Back
Top Bottom