CCM yafanya umafia kumzima Dr Slaa Mbeya

CCM yafanya umafia kumzima Dr Slaa Mbeya

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Katika hali isiyotarajiwa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani hapa juzi, ilibuni mbinu za kuzuia kutangazwa kwa mkutano wa Dk. Slaa baada ya kuitisha kikao na waandishi wa habari wa vyombo vyote katika muda ambao katibu huyo wa CHADEMA alikuwa akihutubia.

Habari za uhakika kutoka ndani ya CCM, zilisema kuwa ingawa ilidaiwa kuwa mkutano huo na waandishi wa habari ulikuwa na lengo la kumtambulisha katibu mpya wa chama hicho wilaya ya Mbeya mjini ambaye amefika baada ya yule wa awali kuhamishwa, lakini nia kubwa ilikuwa kuukwamisha mkutano wa Dk. Slaa.

Habari zinadai kuwa CCM iliwaambia waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo kuwa walitaka pia kuzungumzia masuala yahusuyo mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya ambapo wamelenga kutuma makada wa chama hicho kuelimisha umma juu ya jambo hilo.

Katibu mpya wa CCM wilaya, Raimond Mwangwale, alisema uelimishaji huo utafanyika siku tatu mfululizo kuanzia Januari 12, katika kata 36 za jimbo la Mbeya mjini.

Mmoja wa makada maarufu wa CCM alilithibitishia Tanzania Daima ukweli wa mkutano huo na waandishi, ingawa alikiri kuwa mbinu yao haikufanikiwa sana. Alikiri kuwa hotuba za Dk. Slaa zimekuwa na madhara makubwa kwa CCM na imekuwa ni vigumu zaidi kuzifuta katika akili za wananchi ambao wameonyesha kuamini kila akisemacho

SOURCE:TANZANIA DAIMA
 
Katika hali isiyotarajiwa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani hapa juzi, ilibuni mbinu za kuzuia kutangazwa kwa mkutano wa Dk. Slaa baada ya kuitisha kikao na waandishi wa habari wa vyombo vyote katika muda ambao katibu huyo wa CHADEMA alikuwa akihutubia.
Habari za uhakika kutoka ndani ya CCM, zilisema kuwa ingawa ilidaiwa kuwa mkutano huo na waandishi wa habari ulikuwa na lengo la kumtambulisha katibu mpya wa chama hicho wilaya ya Mbeya mjini ambaye amefika baada ya yule wa awali kuhamishwa, lakini nia kubwa ilikuwa kuukwamisha mkutano wa Dk. Slaa.
Habari zinadai kuwa CCM iliwaambia waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo kuwa walitaka pia kuzungumzia masuala yahusuyo mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya ambapo wamelenga kutuma makada wa chama hicho kuelimisha umma juu ya jambo hilo.
Katibu mpya wa CCM wilaya, Raimond Mwangwale, alisema uelimishaji huo utafanyika siku tatu mfululizo kuanzia Januari 12, katika kata 36 za jimbo la Mbeya mjini.
Mmoja wa makada maarufu wa CCM alilithibitishia Tanzania Daima ukweli wa mkutano huo na waandishi, ingawa alikiri kuwa mbinu yao haikufanikiwa sana. Alikiri kuwa hotuba za Dk. Slaa zimekuwa na madhara makubwa kwa CCM na imekuwa ni vigumu zaidi kuzifuta katika akili za wananchi ambao wameonyesha kuamini kila akisemacho

SOURCE:TANZANIA DAIMA

Ni mteule wa MUNGU, Tanzania-Africa, kusini mwa jangwa sahara. tupme kura za ndio
 
Dr. Slaa ni zaidi ya mkutano mchovu kati ya waandishi na Magamba
 
Wanakiri pia kuwa wana mwenyekiti wa chama bomu ambaye ni jk, janga la kitaifa na rais bomu
 
CCM haina kitu imechoka jamani iacheni ikapumzike kwa amani. Hakuna kitu kisichokuwa na mwisho
 
Uongozi wa chadema mbeya umesambaratika,kutokana na mambo mbalimbali ya kijamii na kiuchumi yanayojitokeza kila kukicha.viongozi hao wameiona chadema kuwa ni chama kisicho na mwelekeo zaidi ya kuhamasisha vurugu na maandamano yasiyo na tija.
 
kwa hiyo wanahabari wamenunuliwa? Ngoja nimwambie DOTTO BULENDU.
 
hojatete au hojachafu? Utaendelea kuwa kiba
raka wa magamba mpaka lini?
 
Katika hali isiyotarajiwa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani hapa juzi, ilibuni mbinu za kuzuia kutangazwa kwa mkutano wa Dk. Slaa baada ya kuitisha kikao na waandishi wa habari wa vyombo vyote katika muda ambao katibu huyo wa CHADEMA alikuwa akihutubia.
Habari za uhakika kutoka ndani ya CCM, zilisema kuwa ingawa ilidaiwa kuwa mkutano huo na waandishi wa habari ulikuwa na lengo la kumtambulisha katibu mpya wa chama hicho wilaya ya Mbeya mjini ambaye amefika baada ya yule wa awali kuhamishwa, lakini nia kubwa ilikuwa kuukwamisha mkutano wa Dk. Slaa.
Habari zinadai kuwa CCM iliwaambia waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo kuwa walitaka pia kuzungumzia masuala yahusuyo mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya ambapo wamelenga kutuma makada wa chama hicho kuelimisha umma juu ya jambo hilo.
Katibu mpya wa CCM wilaya, Raimond Mwangwale, alisema uelimishaji huo utafanyika siku tatu mfululizo kuanzia Januari 12, katika kata 36 za jimbo la Mbeya mjini.
Mmoja wa makada maarufu wa CCM alilithibitishia Tanzania Daima ukweli wa mkutano huo na waandishi, ingawa alikiri kuwa mbinu yao haikufanikiwa sana. Alikiri kuwa hotuba za Dk. Slaa zimekuwa na madhara makubwa kwa CCM na imekuwa ni vigumu zaidi kuzifuta katika akili za wananchi ambao wameonyesha kuamini kila akisemacho

SOURCE:TANZANIA DAIMA

Ha ha ha.
Pelekeni utunzi wenu kwenye vitabu vya hadithi.
OTIS
 
Uongozi wa chadema mbeya umesambaratika,kutokana na mambo mbalimbali ya kijamii na kiuchumi yanayojitokeza kila kukicha.viongozi hao wameiona chadema kuwa ni chama kisicho na mwelekeo zaidi ya kuhamasisha vurugu na maandamano yasiyo na tija.
Wewe mbona ni mwongo uongozi wa ccm hapa mbeya ndio unasambaratika kutoka na maovu yanayofanywa na Meya wa jiji la mbeya bw. Kapunga anayekwamisha miradi ya jiji letu la mbeya hadi magamba wenzie wanataka kumng'oa kutokana na vitendo vyake vya kukwamisha miradi ya maendeleo na ufisadi uliotukuka.
 
kajifanyia umafia mwenyewe kutafuta mchawi ni kutaka umaarufu tu
 
source yenyewe tanzania daima ulitegemea nini. kama hakupata fursa hiyo maanake umaarufu wake mkoni mbeya unakwisha hakuna cha CCM wala CUF wala Mshirikina aliyetumwa kufanya fitna. Hivyo vyote ni visingizio
 
Back
Top Bottom