Elections 2010 Ccm yaanza kampeni ya uchaguzi 2010 kwa changa la macho

Jan 16, 2007
721
176
Ndugu zangu wanajamii katika siku za karibuni tumeshuhudia kauli mbali mbali ya viongozi kuhusu kukemea ufisadi!Kauli ya Mh.John Malecela,Dr.Makongoro,SpIka wa Bunge Samweli Sitta n.k .Hivi hawa watu ambao wengi wao wamo katika uongozi karibu nusu karne!Walikua wapi mpaka nchi inafika hapa ilipo leo?Jamani tunapashwa kua makini kwa kauli za watu hawa kwani ni hao hao waliokua wanaimba nyimbo ya kua hakuna ufisadi CCM!Ni nini kimewafanya wabadirike ghafla??!Naona hapa tunaandaliwa mazingaombwe mengine au changa la macho.Sitashangaa kila wakati wa uchaguzi utakavyokua unakaribia tutakua tunasikia kauli za viongozi wa CCM wakikemea ufisadi na mwisho wake Rais JK atachua hatua kali kwa baadhi ya viongozi wa CCM (Ambao watatolewa kafara) Na kuibuka mshindi shujaa na jasiri wa kupambana na RUSHWA NA UFISADI!!!Maandamano nchi nzima na kuwasahaulisha walalahoi kwa UFISADI MKUBWA WALIOUTENDA KATIKA KIPINDI CHAO CHA UTAWALA.WANANCHI TUKAE CHONJO NA KUA MAKINI TUNAPASHWA KUWAULIZA WALIKUA WAPI WAKATI HAYA YOTE YANATOKEA? TUWE MAKINI MAZINGAOMBWE YAMETOSHAA MUNGU IBARIKI TANZANIA.nAWAKILISHA HOJA
 
mimi nakuunga mkono katika swala la maandamano. Lazima tupigania haki yetu 2010...hatuwezi kuendeshwa kama kondoo
 
Back
Top Bottom