CCM Wameonyesha Demokrasia

Wacha1

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2009
Posts
16,676
Reaction score
8,246

Uchaguzi ndani ya CCM leo hii umeonyesha jinsi chama hicho kikongwe kilivyo bora katika kufanya shughuli zake pale walipomchagua mgombea wa Urais wa Zanzibar Dodoma leo hii.

Mwniyi ndiye atakiwakilisha chama chake mwaka huu. Je, vyama vya upinzani wanaweza kujifunza lolote? Je, CCM walipanga mbinu hii ili kuwahadaa upinzani?
 
Naunga mkono hoja.
 
Naona tu hata Shein amewachoka kabisa.
 
Demokrasia kwa nchi nyingine? Hapa kwao aameshindwaje kuweka viongozi wengine akina Membe akajipima mabavu
 
Yeah nimependa Mwenyekiti Mgombea kusimamia process nzima yeye mwenyewe

Sijui kisheria hili limekaaje, lakini nanusa conflict of interest. Ingawaje ccm ipo pande mbili, kitakiba, Zanzibar na Tanganyika ni nchi mbili tofauti..inawakuwaje Raisi wa Tanganyika (ingawaje pia ni wa muungano) kusimamia mambo ya Nchi ya zanzibar ili hali Raisi wa Zanzibar amejikalia tu kama kibogoyo... mambo gani haya? Tanganyika ni kweli wanathamini muungano, lakini hili la kusimamia uchaguzi wa ccm ya zanzibar, nchi ya zanzibar, serikali ya wazanzibar na uraisi wa zanzibar, tafadhari waacheni wapumue kwa kweli.. mumewakalia sana kooni sana..
 
Demokrasia au udikteta kamili?
Hakuna kumpingaagufuli na aliyejaribu amekiona cha mtema kuni....

Mzee mwinyi alisema anatamani magufuli atawale milele kwa hiyo huo uteuzi wa mgombea wa Zanzibar ni kiini macho tu bali uhalisia ni kua magufuli alifurahia sn kauli ile ya mzee so hiyo ni hisani na mkakati wa kudumu kwa ajili ya nia ovu
 
Magufuli alishindanishwa na nani ?
 
Wazanzibar miaka yote huwa wanachaguliwa Rais na sisi watanganyika
 
Mbona tulijua tangu 2016, tofautisha kuchaguliwa na kupitishwa
 

Point yako ni nini hapa we dogo?
 
Mzee ni mnufaika akiwa na tegemeo hili la fadhila familia isife njaa.
 

Mkuu kama wazanzibari bado wamelala, unategemea wataacha kuchaguliwa viongozi? Unapoishi kwa kutegemea vyombo vya dola, yule anayetoa amri ya vyombo vya kukubeba anakuchagulia tu kiongozi, na hakuna utakalofanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…