GE2025 CCM walikosea kukata jina la Luhaga Mpina Ubunge kisesa

GE2025 CCM walikosea kukata jina la Luhaga Mpina Ubunge kisesa

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

koryo1952

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2023
Posts
1,289
Reaction score
2,190
Mhe. Luhaga Mpina anapendwa sana na wananchi wa Jimbo la Kisesa kule Wilaya ya Meatu. Alipotia nia ya kuomba uteuzi wa kuwa tena mgombea ubunge wa Jimbo la Kisesa CCM wakamkata jina.

Amejiunga na ACT - Wazalendo kama mgombea Urais. Mhe. Luhaga ameanza kuomba saini za udhamini kutoka mikoa mbalimbali. sijaamini macho yangu Mpina anapendwa. sana na wananchi.

Namtabiria Mhe. Mpina kuchukua uongozi wa nchi hii kwa jinsi wananchi wanavyompenda. Alipofika Chato na Katoro usipime ule umati uliojaa pale inaashiria kuwa huko mbeleni mambo ni mazuri kwa Mhe. Mpina.

Ataisumbua sana CCM. CCM mlifanya kosa kubwa kukata Jina la Mhe. Mpina. "Majuto ni mjukuu".
 
Wewe Mpina , mtu wa Kazi maalumu ya kuwapumbaza wapinzani, mfano umeahinda,Nani atakutangza mshindi wakati tume isiyo huru ni ya bi🐸
 
Kupendwa sio issue nchi hii walipendwa akina Mrema, Lowasa, Slaa na Lissu ila walidhulumiwa kura zao na tume ya uchaguzi.

Mpina yupo vizuri ila kuingia kwenye uchaguzi ambao utakuwa na makandokando naona amepoteza muelekeo.
 
Law number 1 of Power: Never outshine your master - Robert Green
 
Hivi kwa nini hakugombea ubunge kwa tiketi ya ACT-WAZALENDO? Ingawa ni wazi anakubalika sana jimboni kwake, sidhani kama anakubaliaka kiasi hicho nchini kote.

Amandla...
 
Mhe. Luhaga Mpina anapendwa sana na wananchi wa Jimbo la Kisesa kule Wilaya ya Meatu. Alipotia nia ya kuomba uteuzi wa kuwa tena mgombea ubunge wa Jimbo la Kisesa CCM wakamkata jina. Amejiunga na ACT - Wazalendo kama mgombea Urais. Mhe. Luhaga ameanza kuomba saini za udhamini kutoka mikoa mbalimbali. sijaamini macho yangu Mpina anapendwa. sana na wananchi.

Namtabiria Mhe. Mpina kuchukua uongozi wa nchi hii kwa jinsi wananchi wanavyompenda. Alipofika Chato na Katoro usipime ule umati uliojaa pale inaashiria kuwa huko mbeleni mambo ni mazuri kwa Mhe. Mpina. Ataisumbua sana CCM. CCM mlifanya kosa kubwa kukata Jina la Mhe. Mpina. "Majuto ni mjukuu".
Huwa kuna msemo wao maarufu wakiutumia wanasema; "Mkia hauwezi kumtikisa ng'ombe, bali ni ng'ombe ndiye mwenye uwezo wa kuutikisa mkia vile apendavyo".
Nadhani wataalamu wa tamathali za semi wanaweza kutusaidia maana ya huu msemo
 
Trash, angekuwa Genuine kwa kugombea ubunge na angepata, kitendo cha kugombea u Rais anakuwa kazi maalum
 
Back
Top Bottom