CCM walalamikia ratiba ya Kampeni ya NEC

CCM walalamikia ratiba ya Kampeni ya NEC

Mwaka huu ccm wako taabani wanatafuta visingizio kibao ili ikubalike lakin wamechelewa Kura zote UKAWAAA
 
Maji shingoni hawa watu kwani kama wamefanya mengi kama wanavyosema wawe wapole watapata kura ila kama ni maigizo tuliyoyazoea basi wakapumzike kwa amani!
 
Kwa hiyo alipopita wasanii hawakumsaidia?

Wana kazi kwani kuandaa mkutano mmoja wa ccm ni mil 118
 
Kwa hiyo alipopita wasanii hawakumsaidia?

Wana kazi kwani kuandaa mkutano mmoja wa ccm ni mil 118

yaani ccm hofu tupu coz wanajua watu walifuata fiesta na sio sera so Lowasa akija anawabadili kwa kuwapa sera na sio fiesta
 
saa 10 jioni: wananchi wako 1000

saa 11 jioni: wananchi ni 1200
saa 11:30 jioni: wananchi ni 2000 wakati Mana FA akitumbuiza...
 
CCM bwana , UKAWA walipochelewa kuanza Kampeni walizusha kua UKAWA imeshindwa kuanza Kampeni mapema kwa sababu Pesa zimewaishia, mara UKAWA wamevurugana nk nk. Sasa leo tena wanageuka wanasema UKAWA walichelewa Kampeni ili waisome kwanza Ratiba ya CCM.

Sasa nyinyi CCM mbona mnalalamikalalamika. Kwani Ratiba kitu gani?
UKAWA vichwa sio kama CCM vilaza.
UKAWA wanajichukulia Point 3 kila wanapolitenga na bado hawajalitenga kwenye Base (Ngome) zao, CCM lazima Mkae.
 
ccm wamekua walalamikaji mwaka huu teh teh teh kifo cha nyani......m
 
Ukiona baba analalamika kwa maumivu makali.Mshaurini aandike wosia,kwani mwisho unakaribia
 
CCM waache utoto... wenyewe walianza kampeni wiki moja mbele ya UKAWA...

Sasa kuna mgongano hapo...? Mgongano ni kama ingekuwa CCM na UKAWA wanafanya mkutano UWANJA MMOJA, SIKU MOJA.... au RATIBA KUINGILIANA....hiyo ndio ingekuwa ni MGONGANO..... waache uongo...!!!

UKAWA wana DELETE CCM kabisaaaa
 
tehe tehe...goli la mkono limeanza kugoma...mie sipo...mtajiju...nanyi mmeanza kuisoma namba...UKAWA MSIKUBALI KUBADILI RATIBA...mimi nimeshaanza kuikariri...pliiizi pipooooz...wapuuzeni...kila kitu kimewashinda hata ratiba yao ya kampeni? wamebaki kutukana na ngonjera kila mahali....muda wa kuongozwa na waswahili umeshapita tunahitaji watu siriazi..
 
Hahahhah hadi wao wanalalamikia NEC, mwaka huu NEC imekuwa upinzani tena
 
Haina haja ya kuhangaika nao hawa jamaa.
Sana sana tunawasaidia kuwaepushia aibu ya kuzomewa. Manake watu kwenye mikutano ya Magufuli wakiulizwa rais nani wanajibu Lowassa mbele ya Magufuli.
Sasa wacha wapange upya ratiba halafu tuone kama na wao watabadilisha style.
Labda wasitumie ile style ya kuwauliza wananchi, "Rais naniiiiiii...."
manake jibu wanalijua
 
Inavyoonekana tayari CCM wameingiwa na woga baada ya kuona Nguvu na Mvuto wa UKAWA ukizidi kuongezeka kila siku. Hii sio dalili njema sana kwa CCM, ni kiashiria cha kukata tamaa.
 
Inavyoonekana tayari CCM wameingiwa na woga baada ya kuona Nguvu na Mvuto wa UKAWA ukizidi kuongezeka kila siku. Hii sio dalili njema sana kwa CCM, ni kiashiria cha kukata tamaa.

Ila Ukawa wamewakwaza sana wana morogoro wamewatangazia watu mwezi mzima kuwa kutakuwa na mkutano uwanja wa shujaa Leo. watu wametoka sehemu za mbali ya mjini wamefika uwanjani kuna tetesi tu kuwa mkutano umeahirishwa na haijulikani utakuwa lini inakatisha tamaa kupotezeana muda Namba hivi.
 
Ila Ukawa wamewakwaza sana wana morogoro wamewatangazia watu mwezi mzima kuwa kutakuwa na mkutano uwanja wa shujaa Leo. watu wametoka sehemu za mbali ya mjini wamefika uwanjani kuna tetesi tu kuwa mkutano umeahirishwa na haijulikani utakuwa lini inakatisha tamaa kupotezeana muda Namba hivi.

Mkuu, nasikia umehairishwa sababu ya mitihani ya darasa la saba Leo na kesho. Watoto wetu wafanye mitihani kwa utulivu. Hii ndo serikali makini ya awamu ya tano ijayo! Inajali mambo ya msingi.
 
Sasa jamani kama CCM mmejiandaa vizuri na mna Sera zenye mishiko kwanini mpate hofu. Hii ndio ile inaitwa kutojiamini na niaibu cha chama tawala ambacho kimekuwa madarakani kwa zaidi ya miaka 50 kuanza kulia lia wakati huu mkihitaji kuonewa huruma na NEC. Ukicheza mpira wa miguu wakati mvua inanyesha ukapigwa bao usilete visingizio vya mvua kwani timu pinzani haikucheza na mianvuli kichwani bali ubora wa kulisakata dimba. CCM hata mrudie kule mlikopita mara tatu hamtawabadirisha watanzania walio kwisha kuamua kwamba sasa imetosha CCM HAPANA..!!! ""UKAWA ULIPO NA WATANZANIA WAPO""
 
Bado na mimi watanisingizia nahubiri udini Jamiiforums😀😀:😉😎
 
Back
Top Bottom