Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,370
- 39,186
Tangia sakala la "orodha ya ufisadi" lianze, serikali ya CCM imekuwa ikitoa majibu ya kukanganyana na mengine hayaingii akili hata kidogo. Majibu mengine yamejaa kiburi na dharau na mengine inabidi mtu ajiulize "walikuwa wanafikiria nini". Kwa maoni yangu kabla ya viongozi wa serikali na wa CCM kuanza kutoa majibu kuhusu tuhuma kwa viongozi 11, la kwanza ambalo wangelifanya ni kukubali tatizo kwanza, hiki kiburi wanachokionesha kuwa wao hawawezi kukosea na wengine wanadai kuwa wamekuwa waadilifu kwa miaka zaidi ya 30 ni kutufanya sisi Watanzania "hamnazo". Nimeona nijitolee kuwaonesha njia CCM ili jambo hili liishe kwa amani. Tadhali sikiliza hoja yangu kuhusu kwanini CCM wakubali makosa kwanza.