CCM tutakuja kulia machozi ya simba

CCM tutakuja kulia machozi ya simba

Suleomary

Member
Joined
Jul 4, 2015
Posts
12
Reaction score
12
Wana CCM wenzangu,

Ni muda sasa Nimekuwa naona Kauli za kuwabeza wapinzani..Lakini hawa watu kila siku wanazidi kuungwa Mkono..

Pia Wapinzani mwaka huu wamefanukiwa kuhamasisha wananchi kujiandikisha sana kupiga kura wakati sisi tuko busy na kushabikia Sinema ya kutangaza nia.

Nawaomba Tuungane kufanya kazi kwa pamoja la siyo mwaka huu tutapata kipigo cha mbwa mwizi kwenye Uchaguzi Mkuu..

Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
Yadumu mawazo ya Mkuu Wa Chama..
Ahsanteni
 
Huo ndio ukweli wenyewe. CCM wamejisahau kabisa. UKAWA wako busy na agenda za msingi na michakato ya uhakika, wao CCM kutwa wanavuana nguo, wanaimba ngonjera za TOT na kuwabeza makada wao wazoefu.
 
Ni wakati wa kila chama kusema mazuri yake na si kukisema chama kingine, CCM elezeni uzuri weni, UKAWA elezeni uzuri wenu,
 
" Hatujinyongi" "hatunywi sumu" ccm mbele kwa mbele hahahaha kalieni mipasho ndege ya ukawa isha anza kupaa hiyoooooo mpaka ikulu.
 
Huo ndio ukweli wenyewe. CCM wamejisahau kabisa. UKAWA wako busy na agenda za msingi na michakato ya uhakika, wao CCM kutwa wanavuana nguo, wanaimba ngonjera za TOT na kuwabeza makada wao wazoefu.

Mkuu naona mshauri wa ccm anawapotosha kwa makusudi
 
too late.
umemuona JK alivyotokwa povu bado hajaamini kuwa jamuhuri inaanguka.
kipigo kiko palepale.
 
Uuuuwwwiiiiii haya makitu tuyakimbize na nondo kabisaa
 
Wana CCM wenzangu,

Ni muda sasa Nimekuwa naona Kauli za kuwabeza wapinzani..Lakini hawa watu kila siku wanazidi kuungwa Mkono..

Pia Wapinzani mwaka huu wamefanukiwa kuhamasisha wananchi kujiandikisha sana kupiga kura wakati sisi tuko busy na kushabikia Sinema ya kutangaza nia.

Nawaomba Tuungane kufanya kazi kwa pamoja la siyo mwaka huu tutapata kipigo cha mbwa mwizi kwenye Uchaguzi Mkuu..

Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
Yadumu mawazo ya Mkuu Wa Chama..
Ahsanteni

Nawaonea huruma sana ccm kwani nyimbo zao zimekuwa ni kuwabeza na kuwakejeli wanao hama kutoka ccm kwa kuwaita mafisadi,leo kuna uzi hapa jamvini kuwa zimekamatwa pembe za ndovu huko uswis zente thamani ya sh 800millioni kutoka Tanzania,huo siyo ufisadi?huo mzigo ulipitia Air port watumishi wa hapo uwanjani hawakuwepo?watanzania tuikatae ccm kwa kuwachagua ukawa
 
Wajitahidi kusoma historia na kujiandaa kisaikolojia. Tatizo kila wanapotaka kujitetea na kuinuka tena, ndiyo wanaharibu kabisa. Mfano Katibu mkuu wa chama (CCM) kuwaita wanaoshindwa kwenye vinyang'anyiro vya kuomba ridhaa ya kugombania Urais, Ubunge na Udiwani kuwa ni makapi. Wapo walioshindwa kweli sababu kama wanaogombania ni wengi lazima apatikane mshindi. Na vilevile wapo wanaoshindwa kwa hila, mpano wanaokatwa majina kinyume cha kanuni, wanaoibiwa kura zao vituoni (tumeshuhidia mengi) na wapo wanaoshinda kwa kutoa rushwa. Sasa ni wazi msimamo huu wa chama utazidi kuwagawa na kuwafukuza wengi ndani ya chama. Na je wananchi tutawachukuliaje hao makapi, mara wanapokuja kukinadi chama chao?.
 
Watanzania wenyewe upeo wa fikra
wanataka mabidiliko. Matatizo ya maisha kama ukosefu wa Ajira, Umasikini, hofu ya maisha (uncertainty of life) asisingiziwe Mwenyezi MUNGU bali ni Man made, and is Made by CCM. ufisadi, uwizi na kukosekana uwajibishwaji ndio imetufikisha Hapo. UKAWA ndio Muarubaini, saa ya Ukombozi imefika. Chagua UKAWA Chagua CHADEMA.
 
Kikwete anajikaza tu lakini anajua ukweli wa kile kinachoenda kutokea octoba25.
 
Uongozi wa CCM uko imara, uliwaarifu wanachama kuwa tayari kisaikolojia kupokea serikali tatu, wahafidhina ndani ya chama badao wakafikiri kizamani wakauzima uongozi kwa kumtumia Sitta. Sasa uongozi unajua unakoelekea wanaofikiri kizamani wanataka mpaka goli la mkono. Uongozi umechoka na geresha na kupalilia umasikini
 
si bora yawe ya simba, mtalia ya samaki na hayatoonekana kwa furaha watakayopata watz
 
Nitafurahi sana ccm ikishindwa,kwa sababu tuna dhahabu,almasi,tanzanaiti,mlima kirimanjalo na vingine vingi tu.Lakini sijapata faida yake,kodi zetu za wanachi ndizozinazo lijenga taifa.Bora ccm ife sina uchungu.
 
Back
Top Bottom