MKEHA
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 714
- 1,137
Kwa mwenendo wa siasa za sasa za Tanzania, kuna uwezekano mkubwa sana bunge lijalo likawa halina wabunge kabisa wa upinzani au wakawemo wachache sana.
Ni kweli awamu hii ya JPM imefanya makubwa sana, lakini kuna baadhi ya wana CCM wangependa kuona bungeni kukiwa na wabunge wa CCM pekee.
Hii itakuwa hasara kubwa sana kwa taifa,.pamoja na maendeleo tunayoyaona kuna mkono kidogo wa wapinzani kwani wakati wanainanga serikali ya CCM kushindwa kununua ngege, ufisadi katika miradi ya umeme wa dharura, wafanyakazi hewa hoja nyingi zilikuwa zikitolewa na wapinzani.
Lakini pia kuna wabunge wengi wa CCM kazi yao ni kusofia tu bila kutoa maoni na mwongozo wa nini kifanyike. Wabunge wengi wa CCM wanaogopa kuikosoa serikali wakiogopa chama kuwashughulikia.
Na wengine wanaogopa kuikosoa serikali wakitarajia kuteuliwa kuwa mawaziri na manaibu mawaziri.
Ni kutokana na hilo bado tunawahitaji sana baadhi ya wapinzani wenye mwelekeo wa kuipa changamoto serikali na kuyafanyia maboresho maisha ya Watanzania.
Kuna baadhi ya wabunge wa CCM ni mzigo kwa chama na serikali. CCM tukiwa peke yetu bunge lijalo itakuwa ni majanga na tutashindwa kuisaidia Tanzania yetu.
Ni kweli awamu hii ya JPM imefanya makubwa sana, lakini kuna baadhi ya wana CCM wangependa kuona bungeni kukiwa na wabunge wa CCM pekee.
Hii itakuwa hasara kubwa sana kwa taifa,.pamoja na maendeleo tunayoyaona kuna mkono kidogo wa wapinzani kwani wakati wanainanga serikali ya CCM kushindwa kununua ngege, ufisadi katika miradi ya umeme wa dharura, wafanyakazi hewa hoja nyingi zilikuwa zikitolewa na wapinzani.
Lakini pia kuna wabunge wengi wa CCM kazi yao ni kusofia tu bila kutoa maoni na mwongozo wa nini kifanyike. Wabunge wengi wa CCM wanaogopa kuikosoa serikali wakiogopa chama kuwashughulikia.
Na wengine wanaogopa kuikosoa serikali wakitarajia kuteuliwa kuwa mawaziri na manaibu mawaziri.
Ni kutokana na hilo bado tunawahitaji sana baadhi ya wapinzani wenye mwelekeo wa kuipa changamoto serikali na kuyafanyia maboresho maisha ya Watanzania.
Kuna baadhi ya wabunge wa CCM ni mzigo kwa chama na serikali. CCM tukiwa peke yetu bunge lijalo itakuwa ni majanga na tutashindwa kuisaidia Tanzania yetu.