CCM tuone soni, huku ni kujiharibia

CCM tuone soni, huku ni kujiharibia

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Siwezi kuvumilia jambo hili. Nami nasema hata kama wasikilizaji hawatakuwepo. Nasema ukweli ili uniweke huru. CCM inafanya siasa za maigizo, ulaghai na usanii. Hii si CCM tuliyoizoea. Hii si CCM yetu ya miaka ya Nyerere, Mwinyi na hata Mkapa. CCM hii inategemea zaidi propaganda kuliko ukweli. Inategemea vihoja badala ya hoja za haja. Kutwakucha, CCM imetingwa na propaganda. Tunapotea na kupoteza.

Hakika hatutashinda uchaguzi huu na mwingine wowote kwa mipasho, kejeli, ulaghai na uzushi. Nianze na mgombea wetu wa Urais: Dr. John P. Magufuli. Ameahidi kuanzisha Mahakama ya Kupambana na rushwa na ufisadi. Kwakweli anashangaza na kudharau sheria zilizopo. Mahakama zipo. Sheria zipo. Majaji na mahakimu wapo. Tatizo utayari. Utayari wa kuwaburuza wahusika mahakamani. Ndani ya CCM na Serikali zake haupo. Afadhali angeahidi utayari tu. Si sheria wala mahakama.

Halafu, kunafanywa kila mbinu na nguvu kuwaaminisha watanzania kuwa UKAWA/CHADEMA ni mafisadi kwakuwa wanao akina Lowassa, Masha na Sumaye. Imesemwa kuwa kwa kuwapokea hao,CHADEMA imehamisha choo kukipeleka chumbani. Ni kweli kuwa Lowassa, Sumaye na Masha, hata kama kweli ni mafisadi, ndiyo pekee ndani ya CCM na hivyo kuhama kwao ni kuhamisha choo chote? Inang'ang'aniwa kashfa ya Richmond, vipi kuhusu kashfa nyingine kama EPA na Escrow?

Ifike mahali, CCM kama chama kinachopigania kutetea dola, kiache usanii na ulaghai. Siasa za sasa ni za kisasa na si kisasi. Kuendelea kujisafisha kisanii wakati huu wa uchaguzi ni usanii uliotukuka. Haufai wakati huu. Kama ni ufisadi, CCM ndiyo mama yake. Nasema hivi kwakuwa wala rushwa na mafisadi ni watu wenye mamlaka Serikalini. Nao ni makada wa CCM. Wao ndiyo waliozaliwa,kulelewa na kukua humo. Wapo wengi tu. Ni aibu kusingizia kuwa sasa wametoka na wamekwenda CHADEMA/UKAWA. Aibu sana.

Kama kampeni hizi za Urais,Ubunge na Udiwani zinalenga kupata ushindi kwa kusafisha chama kutoka rushwa na ufisadi,CCM itakwama na haitatoboza. Kama tunalenga kutetea dola kwa hoja na kuonesha mafanikio ya kichama kwa utawala uliopita,tutafanikiwa.

Tuache usanii!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Inabidi muwe makini maana cheap politics siku hizi hazipo.....Hakuna mtu yeyote chadema aliye na maamuzi binafsi isipokuwa baraza kuu tuu
 
umenena yote na yatupasa wasikilizaji kusikia.Na kweli itasimama daima
 
umeongea ukweli, lakini katika sehemu na wakati usiyo sahihi...
hawatakusikiliza mkuu...Rushwa kwao ni Richmond...baaasi...
 
Adui wa ccm sio chadema au ukawa adui wa ccm ni sisi wananchi
 
Hapa ni LOWASA tu...hata waigize maigizo ya kichina, kihindi, kijerumani au kimarekani....hapa ni Lowasa tuuuuuuuuuu
 
aluta continua no retreat no surrender no matter wat kaanan tuliohahidiwa tutafika japo Musa ataishia kuiona kwa mbali
 
VUTA-NKUVUTE,vp na mipango yenu inayofanywa na kina Masaburi na Mwigulu?! Si soon mtaleta Mungiki na boko kharam?! CCM bado mna uhalali wa kukaa madarakani?! Kwa maslahi ya nani??!!
 
Last edited by a moderator:
Usanii wao waendelee nao wanadhani wapiga kura ni walewale kama wa 2005 walioahidiwa maisha bora kwa kila mtu...usanii wa kufananisha mabadiliko yaliyotokea Libya na tunayotaka watanzania ni usanii, kuvalisha vijana wa mtaani t-shirt za chadema , kujenga hospital ya rufaa kila mkoa ni usanii,
 
Hamna soni sikiliza tena maana umeshasikia siamini kama ni unaweza kuwa mshiriki wa ujinga huu
 
Nakupa big up kubwa sana Mzee Tupatupa kwa kuwapa vidonge vyao na ukweli mtupu makada 'wenzio' wa Lumumba.
 
kwa upande wangu, naunga mkono kauli yako mkuu.

Ikiwa CCM ina uchungu wa kutaka kuendeleza taifa hili, hatua kali za kisheria zingechukuliwa dhidi ya wahusika wote wa kashfa mbalimbali zinazodhohofisha nchi yetu.

Viongozi wanapoyaacha matukio mabaya ya ubadhirifu wa mali za umma hususan fedha za serikali na rasilimali zake, Wananchi wanaumia sana. Kinachowaumiza wananchi ni kukosekana kwa huduma bora za jamii au upungufu wa huduma hizo. Hivyo neno 'UZALENDO' linakosa thamani katika jamii.

Kukosekana kwa Uzalendo ni tatizo ambalo linaweza kupelekea maendeleo duni ya Taifa letu. Watu katika taifa hili hawatajitolea katika ujenzi wa Taifa kwa sababu wataamini kuwa kuna wachache wanaonufaika na rasilimali za taifa. Hivyo wananchi watahitaji pesa kufanya kazi ambazo zamani walikuwa wakizifanya bure.

Hivyo Ikiwa CCM itapata nafasi tena au chama chochote kitachopata nafasi ya kuiongoza nchi hii, kiwe tayari kutoa adhabu kali bila kumfumbia macho mhujumu uchumi yeyote kwa kumshitaki, kumfilisi na hata kumpeleka jela mtu yeyote aliyesababisha hasara kubwa kwa nchi.

TUMECHOKA KUBEBANA

Sasa ona tena visa vya Mwakyembe kwa Lowassa kuhusu Richmond. Mtu ambaye alipewa dhamana ya kuwatetea Watanzania dhidi ya kupe hewahuyu (Richmond). Ni yeye ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge iliyochunguza kashfa ya hiyo. Amesahau kuwa ni yeye ndo alimwona Lowassa hana hatia na kuutangazia umma kuwa Lowassa hakuhusika. Inakuwaje anataka kugeuza Kiswahili ambacho hakitaweza kutusaidia tena Watanzania kwamba Lowassa alihusika.

Tuwe wakweli, tulijenge taifa letu.
:wink::wink:😎😎😎😎
 
mkuu VUTA-NKUVUTE nimesema mwanzo kitengo cha propaganda hakifai wanajua kuomba pesa tu lakini hamna outcome!
 
Last edited by a moderator:
...
Halafu, kunafanywa kila mbinu na nguvu kuwaaminisha watanzania kuwa UKAWA/CHADEMA ni mafisadi kwakuwa wanao akina Lowassa, Masha na Sumaye. Imesemwa kuwa kwa kuwapokea hao,CHADEMA imehamisha choo kukipeleka chumbani. Ni kweli kuwa Lowassa, Sumaye na Masha, hata kama kweli ni mafisadi, ndiyo pekee ndani ya CCM na hivyo kuhama kwao ni kuhamisha choo chote? Inang'ang'aniwa kashfa ya Richmond, vipi kuhusu kashfa nyingine kama EPA na Escrow?
...

Hii mbinu ya choo kuhamishiwa chumban ni mbinu mfu ya ssm kujaribu kuwaogopesha Team Lowassa ambao bado wapo ssm ili wasihame sasa.

Bakhat mbaya sana kwa ssm, na kama ilivo ada ya siku ya kufa nyani ambapo miti yote huteleza, mbinu hiyo haisaidii kitu sababu, hata kama Team Lowassa wasipohama kwa sasa, bado mikakati yote ya ndani ya ssm wanaipekleka kwa legwanan na kura watampa el
 
Back
Top Bottom