PreGE2025 CCM tujipange naona vijana wameamua agenda yao ni 'No Reforms, No Election'

PreGE2025 CCM tujipange naona vijana wameamua agenda yao ni 'No Reforms, No Election'

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

koryo1952

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2023
Posts
1,289
Reaction score
2,190
Jana katika kipindi cha MALUMBANO YA HOJA iliyohusu NINI NAFASI YA VIJANA KWENYE UCHAGUZI 2025. Kwa kweli vijana walisema mengi kuhusu mustakabali wa nchi yetu kuelekea uchaguzi wa 2025.

Kwanza waligusia Tume Huru ya Uchaguzi na wakasema kwa uwazi kuwa Tume hii si huru. Pili walisema kuwa ili kuwe na uchaguzi ulio huru basi marekebisho kwanza yafanyike kwenye Tume huru. Tatu waliunga dhana ya No reform No election na dhana hii kwa kweli imekwishaenea kwa vijana wengi nchini na hivyo kama Wana CCM inatubidi tujipange kuwaelemisha wananchi juu ya dhana hii.

Kama inavyoonekana mwaka huu wapiga kura wengi watakuwa vijana. Vijana safari hii wamepata mwamko mkubwa sana. CCM tujipange.
 
Jana katika kipindi cha MALUMBANO YA HOJA iliyohusu NINI NAFASI YA VIJANA KWENYE UCHAGUZI 2025. Kwa kweli vijana walisema mengi kuhusu mustakabali wa nchi yetu kuelekea uchaguzi wa 2025.

Kwanza waligusia Tume Huru ya Uchaguzi na wakasema kwa uwazi kuwa Tume hii si huru. Pili walisema kuwa ili kuwe na uchaguzi ulio huru basi marekebisho kwanza yafanyike kwenye Tume huru. Tatu waliunga dhana ya No reform No election na dhana hii kwa kweli imekwishaenea kwa vijana wengi nchini na hivyo kama Wana CCM inatubidi tujipange kuwaelemisha wananchi juu ya dhana hii.

Kama inavyoonekana mwaka huu wapiga kura wengi watakuwa vijana. Vijana safari hii wamepata mwamko mkubwa sana. CCM tujipange.
ccm ilishakufa hili somo likieleweka kwa tume na polisi baaass
 
Msifananishe Gen Z wa Kenya na wabongo. Kwanza VIJANA wetu wana uelewa tofauti sana juu ya Haki na wajibu wao kwa nchi yao. Wapo wapo na shughuli zao zinazowaingizia kipato. Fursa ni nyingi ktk nchi hii kwa vijana kuweza kujipatia vipato vyao japo vidogo ukilinganisha na wale wa Kenya ambao hata siha zao tu zinaonyesha dhahiri ni mafukara waliopoteza matumaini.
VIJANA wa kitanzania hawalii njaa kwa sababu wanaweza kupata riziki zao ndogo ndogo bila kupigana.
Ninakuhakikishia hata kama CDM wataitisha maandamano, VIJANA hawatashoboka nayo kwa sababu wameshaona wapinzani wa nchi hii hawana tofauti na watawala. They look like the same.
 
Lisu mwenyewe kaikataa tayari iyo agenda ya chama chake.ndio maana kaamua kutangaza nia ya kugombea urais.sasa sijui hao vijana unaowasema ni kina nani na wanamuunga mkono nani!
 
CCM hawana wasiwasi wana machawa redio zote Tanzania.
 
Njia nzuri ya ccm kuonesha kwamba bado anastahili kuongoza na bado yupo imara ni kutoa go ahead kwa serikali kufanya reform ya katiba ya uchaguzi na mwisho kuunda tume huru kisha tushindane kwa kura.

Kujisifia wewe ni imara na bora halafu tume ipo chini yako unaipangilia wewe na kupokea order kutoka kwako huko ni kujitekenya na ukacheka.
 
Lisu mwenyewe kaikataa tayari iyo agenda ya chama chake.ndio maana kaamua kutangaza nia ya kugombea urais.sasa sijui hao vijana unaowasema ni kina nani na wanamuunga mkono nani!
ulisoma mpaka darsa la ngapi huko ulikofundishwa ujinga huu
 
Jana katika kipindi cha MALUMBANO YA HOJA iliyohusu NINI NAFASI YA VIJANA KWENYE UCHAGUZI 2025. Kwa kweli vijana walisema mengi kuhusu mustakabali wa nchi yetu kuelekea uchaguzi wa 2025.

Kwanza waligusia Tume Huru ya Uchaguzi na wakasema kwa uwazi kuwa Tume hii si huru. Pili walisema kuwa ili kuwe na uchaguzi ulio huru basi marekebisho kwanza yafanyike kwenye Tume huru. Tatu waliunga dhana ya No reform No election na dhana hii kwa kweli imekwishaenea kwa vijana wengi nchini na hivyo kama Wana CCM inatubidi tujipange kuwaelemisha wananchi juu ya dhana hii.

Kama inavyoonekana mwaka huu wapiga kura wengi watakuwa vijana. Vijana safari hii wamepata mwamko mkubwa sana. CCM tujipange.
Kweli umewapa mwanga kwa sababau wamebanwa mpaka kooni. Vijana wa leo sio wanavyowafikiria wameamka. Kuna kijiwe cha vijana CCM nakionaga mahali anzia Lissu alivyoingia mtaani na kupaza sauti kwa ajili ya wanyonge kimesambaratika. Tena kila mmoja anamkwepa mwenzie.

Vijana CCM badilikeni acheni kuwa toilet paper. Familia za matajiri wanapeana vyeo mtoto akiwa tumboni.

Watoto wa masikini mnakwenda kukatia ng'ombe majani na kfagia mbolea ili wakirudi waje wanywe maziwa.
 
Jana katika kipindi cha MALUMBANO YA HOJA iliyohusu NINI NAFASI YA VIJANA KWENYE UCHAGUZI 2025. Kwa kweli vijana walisema mengi kuhusu mustakabali wa nchi yetu kuelekea uchaguzi wa 2025.

Kwanza waligusia Tume Huru ya Uchaguzi na wakasema kwa uwazi kuwa Tume hii si huru. Pili walisema kuwa ili kuwe na uchaguzi ulio huru basi marekebisho kwanza yafanyike kwenye Tume huru. Tatu waliunga dhana ya No reform No election na dhana hii kwa kweli imekwishaenea kwa vijana wengi nchini na hivyo kama Wana CCM inatubidi tujipange kuwaelemisha wananchi juu ya dhana hii.

Kama inavyoonekana mwaka huu wapiga kura wengi watakuwa vijana. Vijana safari hii wamepata mwamko mkubwa sana. CCM tujipange.
WEWE SIO CCM.
 
vijana hawatapiga kura. Nimekaa pale naangalia
Vijana ninaokutana na kuongea nao wanasema watapiga kura.
Ila nimeshangaa kitu kimoja. Bibi flani, ni jirani yangu, nilimsikia kabisa akisema "safari hii siendi kupiga kura, tangu nipige kura nimepata nini?. Hao tunaowapigia kira siwanaenda kujilia tu". Maeneo tunayoishi na huyo jirani bibi, tangu uhuru ndio tumepata barabara ya lami mwaka jana. Maji unayapata mtoni.
 
Vijana ninaokutana na kuongea nao wanasema watapiga kura.
Ila nimeshangaa kitu kimoja. Bibi flani, ni jirani yangu, nilimsikia kabisa akisema "safari hii siendi kupiga kura, tangu nipige kura nimepata nini?. Hao tunaowapigia kira siwanaenda kujilia tu". Maeneo tunayoishi na huyo jirani bibi, tangu uhuru ndio tumepata barabara ya lami mwaka jana. Maji unayapata mtoni.
Chai
 
Back
Top Bottom