Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 40,000
Wakati mwingine huwa ni busara sana kuongea na 'Mfuga Mmbwa' kuliko mtu mstaarabu kuanza kupigiana kelele ovyo na 'Mmbwa' mwenyewe anapokubwekea hovyo.
Mzee Mwanakijiji, asante kwa kulitambua hilo.
Mimi nahisi kuna kigogo yuko nyuma yao anawatumia UVCCM kuwatukana Sitta na Mwakyembe, vijana wanaongea maneno bila adabu, eti WANAKITAKA chama cha mapinduzi kutoilipa dowans, wanakitaka chama cha mapinduzi kuipundua bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu......
Nimeongea kule kwenye tamko kuwa kuna mwanaume nyuma ya hawa vijana, na wanatumika!...Tamko lao lingekuwa na nguvu kama wasingechanganya na matusi ya aibu kwa Dr.
Wanaanzisha moto hawa, ambao naamini hawataweza kuzima!
Kama mtu ambaye nimemuunga mkono Dr. Slaa na kuamini kuwa ni mtu aliyepaswa na anayestahili kupewa nafasi ya kuliongoza taifa nimeshtushwa na kusikitisha na tamko la UVCCM hususan mashambulizi yao ya mtu - ad hominem thidi ya Dr. Slaa. Ninawasihi viongozi wa CCM Taifa kukemea na kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya kundi hilo la viongozi wa vijana.
Kutokuchukua hatua mara moja na kukaa kimya binafsi naamini iwakuwa ni halali kuamini kuwa uongozi wa taifa wa CCM umetoa baraka zake. Which brings me to my observation: it won't be pretty! Yatakapoanza kuporomoshwa matusi na mambo mengine dhidi ya viongozi wa CCM wa kitaifa isije kuoneekana "ni kuvunja heshima, kuchochea, matumizi mabaya ya vyombo vya habari" na upuuzi wa kawaida tuliouzoea.
Maana naamini walichofanya UVCCM kimewapa watu wengine haki ya kuwatukana na kuwasema viongozi wa taifa wa CCM katika masuala yao binafsi. That will be a tragedy.
Ukiniuliza mimi CCM (T) hawana zaidi ya masaa ishirini na nne ya kutoa kauli ya kinidhamu dhidi ya vijana wao.