CCM sasa ina 'Lissuphobia'

CCM sasa ina 'Lissuphobia'

ccm kwa lissu ni sawa na tembo na sisimizi,lissu anawakimbiza mno
 
T.l ni jembe kwelikweli lukuvi anamtambua akitaka kupambana nae lazima amwandae mwanasheria na bi kidude .
 
lisu ni sawa na serikali ya maccm na makada wake
 
Tatizo ni ufinyu wa hoja na mashtaka ya uongo. Lissu kw akweli ni mwanasheria anayezijua sheria za nchi ipasavyo, ndio maana hata bungeni siku hizi wale wakalia kiti wakiona tu lissu anaomba muongozo hukaa vizuri na ikibidi humzuia hata asiseme neno au huo mwongozo. Chezea lissu wewe. Dah kweli hii ni lissuphobia........................Peoples.............................Power.....................
Jamaa zetu walikuwa wanapenda sana kukimbilia mahakamani na kutengeneza vijikesi vya kipuuzi tu siku hizi thubutu, wengine Dr. Slaa aliwataja kwenye list of shame wakasema wataenda mahakamani wako wapi mpaka leo Kimyaaaaaaaaaaaaaaa.
 
Wakili Msomi Tundu Antipas Mughway Lissu sasa ni 'ugonjwa' kwa CCM yetu. Makada hutetema,hukosa raha na kunyong'onyea linapotajwa jina la Lissu. Ni katika mashauri mbalimbali yanayopelekwa Mahakamani yakiwahusisha makada wa CCM au CCM ikitajwa 'kuanzisha na kubariki' mashauri hayo.Yaweza kuwa ya jinai au madai. CCM yetu sasa ina 'Lissuphobia'.

Kwenye kesi ya ugaidi iliyomhusisha Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA Winfred Muganyizi Lwakatare na kusemwa kuwa 'ilianzishwa' na CCM, mara baada ya kujitokeza kwa Tundu Lissu kama Wakili wa Utetezi, makada wa CCM walitimua mbio.Kila mmoja na njia yake. Wakapoteana. Mahakama kuu ikafutilia mbali mashtaka ya ugaidi dhidi ya Lwakatare. Lissuphobia.

Katika kesi kupinga ushindi wake wa uchaguzi wa 2010 katika Mahakama ya Rufani ya Tanzania iliyoketi Dodoma, Lissu alijiwakilisha mwenyewe. Si kama Wakili.Ni kama Mjibu Rufani. Makada wa chama chetu cha CCM walisambaratika na kupotelea kusikojulikana. Wakamuacha Wakili wao solemba.Lissu akashinda. Lissuphobia.

Ni jana tu, ilitolewa taarifa kuwa Wakili Msomi Lissu ataongoza timu ya Mawakili wa Utetezi katika kesi ya 'kutukana' iliyokuwa ikimkabili Mbunge wa Arusha Mjini Ndugu Godbless Lema. Kimsingi,kesi hii imeanzishwa na kada wa CCM na Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Ndugu Magesa Mulongo.Kusikia uwepo wa Lissu,makada wote wa CCM wakiongozwa na CCM waliachana njia.Wakaweka mpira kwapani na kukimbia Mahakama na kesi husika. Lema akafutiwa mashtaka yake leo Arusha. Lissuphobia.

Mifano hii, pamoja na kesi ya rufaa ya Ubunge wa Lema iliyosikilizwa Mahakama ya Rufani ya Tanzania iliyoketi Dar es Salaam,itoshe kuonesha jinsi Wakili Msomi Tundu A.M. Lissu anavyoogofya. CHADEMA sasa wana silaha imara.Ni dhidi ya unaoonwa kama ukandamizwaji wa demokrasia nchini na uonevu wa kisiasa kupitia Mahakama. Katabia kanakojengeka na kushamiri.Wana Lissu.CCM tuna nani? Dawa ya Lissuphobia ni nini?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Tuna watoa kucha na macho!! Soon tutamu-ulimboka Lissu!! subiri uone!!
 
Halafu Mkuu, Lissu kama Wakili wa Kujitemea,ukiacha kuwa ni Mbunge wa CHADEMA, CCM bado mna Fursa ya Kumtumia kwenye Kesi zenu Kama Murji wa Mtwara alivyomtumia Peter Kibatala, nanyi Mtumieni Lissu basi kama wakili wenu
Hebu jaribuni option hii basi, Mzee, Peleka huu ushauri Lumumba

watamshushia hadhi lissu wetu, acha magamba waendelee kuwatumia mawakili uchwara kwa maana kesi zao ni za kijinga na hawajifunzi kila kunapokicha wao wanatanguliza ujinga tu.
 
lissu pekee ni, serikali nzima ya jk na jk akiwemo ndani+ wabunge wa sisiemu.
Hakuna anayeweza kusimama na lissu mbele ya mahakama toka sisiemu.
Mkuu nakubaliana na wewe kabisa, Ila tatizo la Mkuu wa Kaya anawasikiliza sana maccm wakati anajua Lisu ni kifaa kuliko mwanasheria mkuu wa Sereka;li ila amemweka benchi kisa usisiemu.
 
Mtu mmoja alisema ili kukabiliana na Tundu Lissu ni lazima CCM itumie mabingwa wa matusi watu kama Lusinde,Komba,Mwigulu,Nkamia,Kigwangwala na wengine ambao hawajaiva vizuri(katika matusi) ili watukane weee mpaka hoja ya Lissu ipoteze maana.
Hao niliowataja ni HAZINA kubwa sana ndani ya CCM.
 
Kawaida ukishakubaliwa kuwa katika safu ya uongozi CHADEMA, wewe ni mkali wa kujenga hoja na kuchambua mambo.

C.v ya mtu ni tosha kabisa kwa maadui kugubikwa na woga. Ni chama chenye watu wanaothubutu bila shuruti wala woga.
 
Upinzani si uadui, bali ni kuwapa fursa wananchi wamchague kiongozi aliye bora, vilevile upinzani unaisaidia serikali iliyoko madarakani kutobweteka na kufanya yaliyo mema kama ilivyo ahidi.Na kiongozi mzuri ni yule anaye heshimu maamuzi ya wananchi na maamuzi ya wananchi yana anzia kwenye kupiga kura.
 
Ina maana upo ndani lakini Haujui kwamba ccm ina wenyewe?


Dawa yake ni utawala wa haki na sheria;



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Mchambuzi swali sio CCM ni ya nani, Ila CCM ina nani wakupambana na LISSU MAHAKAMANI, BUNGENI, MDAHALO nk.

Tehtehh! au Unajitolea Kupambana naye wewe, wakuandalie Mdahalo?

CC: #TeamBk7 ,#Makamanda
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom