Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,380
- 911,169
CCM Rukwa yataka Kanisa litubu
Imeandikwa na Peti Siyame, Sumbawanga; Tarehe: 28th December 2010 @ 23:53
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Rukwa, kimewataka baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga walioonesha kushabikia baadhi ya vyama vya siasa wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu, wasitumie nafasi ya Kanisa hilo kuwatenga na kuwawekea pingamizi waumini wao, hasa wanaCCM.
Rai hiyo ilitolewa juzi usiku mjini hapa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa, Hypolitus Matete katika hotuba yake kwenye hafla ya kuwapongeza Mbunge wa Jimbo la Sumbawanga Mjini kwa tiketi ya CCM, Aeshy Hilaly na Meya wa Manispaa hiyo, Samweli Kisabwite, kwa kuchaguliwa kushika nafasi hizo.
Kauli ya Mwenyekiti huyo inatokana na mgongano wa kiimani unaolihusisha Kanisa hilo na baadhi ya waumini wao ambao wengi wao ni wanaCCM, uliochochewa na kile Kanisa hilo kinachoeleza kauli za kufuru dhidi ya Utatu Mtakatifu wakati wa Uchaguzi Mkuu, likidai baadhi ya wagombea walikufuru imani ya Kanisa hilo kwa kujifananisha na Yesu Kristo mwana wa Mungu katika dhana ya mafiga matatu.
Kwa kuwa makanisani ni mchanganyiko wa waumini wenye itikadi za vyama mbalimbali vya siasa na wale ambao hawana itikadi hizo, bila shaka wapo baadhi ya viongozi wa kanisa wa ngazi mbalimbali ambao wana itikadi za vyama ambapo wengine walikuwa mawakala wa vyama vyao wakati wa Uchaguzi Mkuu uliopita.
Nashauri watu wa namna hiyo wasitumie nafasi zao za Kanisa kuwatenga na kuwawekea pingamizi zisizokuwa na msingi wa itikadi ya vyama vyao na hasa kwa wanaCCM wanaotaka kujipatanisha na kanisa lao, alifafanua Mwenyekiti Matete.
Alisisitiza kuwa kutengwa kwa baadhi ya waumini na kanisa hilo na wengine kuwekewa pingamizi, lisitafsiriwe kuwa ni fimbo ya kudhoofisha nyoyo za wanaCCM na mashabiki wao, kiasi wakashindwa kujiunga na CCM kwa hofu ya kutengwa au kuwekewa pingamizi, kwani chama kitaendelea kujengwa na kuwa imara.
Bahati mbaya Kanisa Katoliki liliingia kwenye mgogoro na baadhi ya waumini wake, ili tuendelee kuwa na amani, nawaomba kuliacha kanisa na waumini wake sisi ambao si waumini wa kanisa hilo ni vizuri tukanyamaza ili tusichochee uchochezi.
Wahenga walisema ya Ngoswe mwachie ngoswe mwenyewe, alisema.
Aidha, alitumia fursa hiyo kuwaonya baadhi ya watu wanaowanyanganya na kuwapora wanachama wa CCM wanapowakuta mitaani wakiwa wamevaa mavazi ya chama hicho, akisema vitendo hivyo vinaashiria uvunjifu wa amani na mshikamano uliokuwepo tangu zamani.
Naye Mbunge wa zamani wa Jimbo la Nkasi, Posian Nyami alitumia vifungu vya Biblia Takatifu juu ya msamaha na kuondoa makundi huku Mbunge Hilaly akitaka kutoangalia uzuri wa jalada la kitabu kabla ya kusoma.
Akizungumza hivi karibuni na vyombo mbalimbali vya habari mjini hapa, Wakili wa Kiaskofu; kwanza alikiri kutengwa na kuwekewa pingamizi baadhi ya waumini wa Kanisa Katoliki jimboni hapa, kwa kuwatenga wanaodaiwa kuisaliti imani yao kwa kufanya kwa kukufuru utatu mtakatifu na kukashifu msalaba.
Hata hivyo, Kasisi huyo alipinga shutuma zinazotolewa dhidi ya kanisa hilo kwa madai kuwa limewatenga na kuweka pingamizi sababu ya itikadi za siasa kwa kukipigia kura chama tawala au sababu za udini.