CCM ni wepesi kama unyoya

CCM ni wepesi kama unyoya

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Kuanzia vijana,washabiki na wengineo wa CCM,katika kujenga hoja ni wepesi sana. Inapotokea kuna mjadala wa ana kwa ana unaowajumuisha CCM na wapinzani,utajionea mwenyewe wepesi wa CCM. Mwana-CCM huishia kujitapa kuwa wanapendwa na kukubalika na wataendelea kuongoza. Alijisemea Mch. Msigwa Bungeni 'so what?'.

Ukiona kiongozi wa CCM au mwanachama anaongea 'points' ujue yuko kwenye mimbari ya mkutano wa hadhara iliyozungukwa na polisi na wanafunzi. Points zenyewe zitakuwa kusifu vyombo vya dola,kukejeli wapinzani na kutamba wanapendwa.

Kwenye midahalo au majadiliano yenye mchanganyiko wa wahusika,utauona wazi wepesi wa CCM. Hawachelewi kudai wahuni wamekodiwa kuwazomea. Hivi ukiongea vitu visivyo na tija kwa taifa ndiyo usizomewe.

Katibu Mkuu wa zamani wa CCM Yusuph Makamba alikuwa wa kwanza kuuona wepesi wa CCM. Aliwakataza viongozi kuhudhuria midahalo. Wa pili kuona wepesi ni Mwenyekiti wao wa sasa Rais Dr. Jakaya Mrisho Kikwete. Rais Kikwete aliwaasa wana-CCM kutotegemea vyombo vya dola. Alijua wazi,bila vyombo vya dola,CCM ni wepesi kama unyoya.

Kimsingi,hata mwaka huu mtaji wa CCM utakuwa ujinga,umaskini na maradhi waliyonayo watanzania na si hoja zao. Ngumu kwao kujenga hoja.
 
ccm bila vyombo vya dola ni wepesi zaidi ya karatasi .
 
Kuanzia vijana,washabiki na wengineo wa CCM,katika kujenga hoja ni wepesi sana. Inapotokea kuna mjadala wa ana kwa ana unaowajumuisha CCM na wapinzani,utajionea mwenyewe wepesi wa CCM. Mwana-CCM huishia kujitapa kuwa wanapendwa na kukubalika na wataendelea kuongoza. Alijisemea Mch. Msigwa Bungeni 'so what?'.

Ukiona kiongozi wa CCM au mwanachama anaongea 'points' ujue yuko kwenye mimbari ya mkutano wa hadhara iliyozungukwa na polisi na wanafunzi. Points zenyewe zitakuwa kusifu vyombo vya dola,kukejeli wapinzani na kutamba wanapendwa.

Kwenye midahalo au majadiliano yenye mchanganyiko wa wahusika,utauona wazi wepesi wa CCM. Hawachelewi kudai wahuni wamekodiwa kuwazomea. Hivi ukiongea vitu visivyo na tija kwa taifa ndiyo usizomewe.

Katibu Mkuu wa zamani wa CCM Yusuph Makamba alikuwa wa kwanza kuuona wepesi wa CCM. Aliwakataza viongozi kuhudhuria midahalo. Wa pili kuona wepesi ni Mwenyekiti wao wa sasa Rais Dr. Jakaya Mrisho Kikwete. Rais Kikwete aliwaasa wana-CCM kutotegemea vyombo vya dola. Alijua wazi,bila vyombo vya dola,CCM ni wepesi kama unyoya.

Kimsingi,hata mwaka huu mtaji wa CCM utakuwa ujinga,umaskini na maradhi waliyonayo watanzania na si hoja zao. Ngumu kwao kujenga hoja.

mwambie vuta...nkuvute huu upuuzi.
 
ccm bila vyombo vya dola ni wepesi zaidi ya karatasi .

jichanganye uone kivumbi chake unajaza tumbo unadhani ndiyo kazi imekwisha ila jua kazi bado mbichi kabisa.
 
Ukitaka kuwajua walivyo dhaifu waangalie hata hawa wanaolipwa kuitetea hapa Jamvini,uelewa wao ni mdogo sana.Mara wamtukane Nyerere huku wakiisifia CCM,mara waunge mkono Hoja ya Mahakama ya Kadhi huku Bunge la katiba walikuwa wenyewe na kupitisha yote waliyotaka kasoro Mahakama hiyo,Mara watetee akina Muhongo wakati Bunge lenye wabunge wengi wa CCM limemwona na hatia n.k,n.k. Kwa kweli hawa jamaa ni watupu sana kiujengaji wa hoja.
 
Ukitaka kuwajua walivyo dhaifu waangalie hata hawa wanaolipwa kuitetea hapa Jamvini,uelewa wao ni mdogo sana.Mara wamtukane Nyerere huku wakiisifia CCM,mara waunge mkono Hoja ya Mahakama ya Kadhi huku Bunge la katiba walikuwa wenyewe na kupitisha yote waliyotaka kasoro Mahakama hiyo,Mara watetee akina Muhongo wakati Bunge lenye wabunge wengi wa CCM limemwona na hatia n.k,n.k. Kwa kweli hawa jamaa ni watupu sana kiujengaji wa hoja.

Hakika Mkuu
 
CCM Imekataliwa Mbinguni na duniani.. Nakubaliana na wewe kabisa ni wepesi kama unyoya,, hawajiamini wanajishtukia kama wezi au wachawi.. Ukitaka kuona imechokwa hesabu fulana za CCM iwe posta au Kariakoo huoni wakivaa au la lazima avae shati jingine juu yake kuificha..

Hawa wasaka tonge ambao kazi yao kupiga kelele humu kama gsu ni njaa tu.. Utashangaa jitu kwao maskini kupindukia lakini bado linatetea mafisadi wanaotafuta fedha ambazo zilitakiwa kununulia dawa na vifaa tiba..

Tunaomba Jamii forum isifungwe ili baadae watoto na wajukuu wa hawa wakina gsu na wenzake waje wasome utumbo wao.. Hakika wajukuu watajuta kuzaliwa na kizazi chao maana wanafikiria kwa kutumia kiungo kinachotolea uchafu mwilini badala ya kutumia kichwa!!
 
jichanganye uone kivumbi chake unajaza tumbo unadhani ndiyo kazi imekwisha ila jua kazi ichi kabisa.

Ntashangaa sana mtanzania atayeipigia kura ccm mwaka huu
 
Kumbe analijua hilo!
basi awe na Sera nzuri inayo uzika
naye amiliki Dola
 
kweli aisee

sent from my iphone 7 nimeinunua SAPNA pale POSTA
 
Back
Top Bottom