Kinkunti El Perdedo
JF-Expert Member
- Nov 28, 2020
- 5,595
- 14,054
CCM imekuwa madarakani kwa takribani miaka 50 shida ambazo watanzania wanazo ni zilezile chini ya utawala wa CCM.
Imefika wakati viongozi ambao ndio dira ya taifa kutoa majina ya ajabu kwa wananchi wake kuona kwamba ndo sifa kuu ya wao kupata ushawishi wa kisiasa nacha ajabu ni kuwa wananchi wenyewe wamekubali kuitwa majina hayo hayo uku wakijihisi ni ufahari kuitwa hivyo "Wanyonge" Na wanyonge hawa ndo wamekuwa wakitapeliwa pesa zao na utawala wa CCM mfano ni wakulima wa korosho.
Na sifa za hawa wanyonge ambao ni mazao ya utawala wa CCM ndo umefanya wawepo wamekuwa na mawazo ya kimaskini ya kutaka kuona kila aliye nacho apoteze ili awe kama wao ila sio wao kufanya juhudi kupata ili wawe kama kundi la walio nacho.
Ndio maana kuna kiongozi alikuwa anawaambia wananchi wake kuwa nchi yao ni tajiri hivyo watembee kifua mbele na wakati huo huo anajiita Rais wa Wanyonge na mpaka anapoteza maisha kawaacha wanyonge bado wakiwa katika hali ile ile uku wakilia badala ya kutumia akili zao kutoka kwenye unyonge.
Unyonge ni ishara ya kujidharau, ujinga, kuwaza kimasikini, uvivu, majungu, fitina, uoga nk na hawa wanyonge ndo mtaji wa CCM kubaki kuendelea kutawala maana ni "wapupaze na uwatawale"
CCM imekuwa ikitembea na matumaini hewa kwa watanzania ndio maana maadui watatu ambao Baba wa taifa aliwataja wako pale pale miaka kenda rudi ni wimbo ule ule Umaskini,ujinga na Maradhi.
CCM ni chama chenye mfumo wa kulindana ndio maana wezi wakubwa wa mali za umma wako bado mitaani wakila kuku kwa mrija kabisa bila wasiwasi na bado pesa za Watanzania wavuja jasho zikiendelea kuwatunza kama viongozi wastaafu.
Watanzania sasa wameonekana kuwa na matumaini makubwa baada ya kuingia kwa awamu ya 6, uku wakisahau kuwa Chama ni kile kile mifumo ni ile ile hakuna kipya ni suala la muda tu.
CCM ni sawa na ukoo wa Panya.
Imefika wakati viongozi ambao ndio dira ya taifa kutoa majina ya ajabu kwa wananchi wake kuona kwamba ndo sifa kuu ya wao kupata ushawishi wa kisiasa nacha ajabu ni kuwa wananchi wenyewe wamekubali kuitwa majina hayo hayo uku wakijihisi ni ufahari kuitwa hivyo "Wanyonge" Na wanyonge hawa ndo wamekuwa wakitapeliwa pesa zao na utawala wa CCM mfano ni wakulima wa korosho.
Na sifa za hawa wanyonge ambao ni mazao ya utawala wa CCM ndo umefanya wawepo wamekuwa na mawazo ya kimaskini ya kutaka kuona kila aliye nacho apoteze ili awe kama wao ila sio wao kufanya juhudi kupata ili wawe kama kundi la walio nacho.
Ndio maana kuna kiongozi alikuwa anawaambia wananchi wake kuwa nchi yao ni tajiri hivyo watembee kifua mbele na wakati huo huo anajiita Rais wa Wanyonge na mpaka anapoteza maisha kawaacha wanyonge bado wakiwa katika hali ile ile uku wakilia badala ya kutumia akili zao kutoka kwenye unyonge.
Unyonge ni ishara ya kujidharau, ujinga, kuwaza kimasikini, uvivu, majungu, fitina, uoga nk na hawa wanyonge ndo mtaji wa CCM kubaki kuendelea kutawala maana ni "wapupaze na uwatawale"
CCM imekuwa ikitembea na matumaini hewa kwa watanzania ndio maana maadui watatu ambao Baba wa taifa aliwataja wako pale pale miaka kenda rudi ni wimbo ule ule Umaskini,ujinga na Maradhi.
CCM ni chama chenye mfumo wa kulindana ndio maana wezi wakubwa wa mali za umma wako bado mitaani wakila kuku kwa mrija kabisa bila wasiwasi na bado pesa za Watanzania wavuja jasho zikiendelea kuwatunza kama viongozi wastaafu.
Watanzania sasa wameonekana kuwa na matumaini makubwa baada ya kuingia kwa awamu ya 6, uku wakisahau kuwa Chama ni kile kile mifumo ni ile ile hakuna kipya ni suala la muda tu.
CCM ni sawa na ukoo wa Panya.