CCM ni ile ile, hakuna kimpya

CCM ni ile ile, hakuna kimpya

Nani aliweza kumpinga JPM na akabaki salama? Kina nani hao waliokuwa wanapinga uongozi wake na kwanini?
Mkuu mbona umejijibu mwenyewe, halafu ukaniuliza tena.? Sentensi yako ya kwanza hapo juu ni majibu ya swali lako kwenye hiyo paragraph yako, kwa hiyo hata wewe kumbe unafahamu kuongoza nchi sio kitu rahisi hasa ukiwa mzalendo.

NB:
Turudi kwenye mada ni ukweli usio pingika tuna changamoto ya uzalendo hasa kwenye nchi zetu za Afrika sio kwenye vyama tawala wala vyama vyama upinzani. Hata wapinzani nao ni walewale tu..
 
Hata mm nataman "Ncha" ifike.


Unajua siwapendi CCM kwa sababu tu ndogo wametawala toka 1961 lkn hamna kitu.


Nataman tuongozwe na chama kipya chenye Sera mpya .
Kipi? Funguka.
Hivi vingine pamoja na kupata mamilioni ya fedha za ruzuku waneshindwa sio tu kujenga ofisi ziendazo na hadhi ya chams,Bali hata kukarabati tu imeshindikana,wakikamata Dola wataweza kujenga nchi?
Waswahili tuna msemo dalili ya mvua ni mawingu.
 
Nyereere alifanikiwa sana 100% kuishikanisha Dola na CCM

Yaani CCM ndio Polis, Majesh, Usalama n.k

Kuiondoa CCM madarakan nisawa umeondoa Dola n.k. Kazi ambayo ni Ngumu mnooooo mnooooooo.
Huyu mzee licha ya sifa nyingi ila kuna sehemu alikosea sana na kupwaya vibaya sana hasa kwenye kuunda taasisi.
 
Sasa huo uzalendo wa kweli kwa upande wa upinzani bado nina mashaka nao. Kwangu mimi naona bado wana deni la kwa namna gani wafanye ili niridhike kua sasa wanaweza kuongoza nchi na kunisahaulishe yale waliyoyafanya mwaka 2015 kwenye uteuzi wa mgombea wao wa nafasi ya urais.

Binafsi nina imani nao tu kwenye nafasi za ubunge na nyingine za chini. Lakini kwenye kuongoza nchi bado hua nahisi wanaweza kurudisha nyuma hata haya maendeleo tuliyonayo.

NB: Kuongoza nchi kama Tanzania sio kitu rahisi, kumbuka hata Mh.Magu alipigwa sana mawe wakati wa uongozi wake na hii ilitokana na mapenzi pamoja n.a. uzalendo aliokua nao kwenye nchi yake..
Mbona unawahukumu wapinzan kwa kosa ambalo kwanza ni la kimkakat ivyo ivyo ni kosa ambalo litabak kuwa doa lkn ni funzo ,na pia kutoka sehem moja ukaenda upande wa pil ukapewa dhamana ata ccm wanafanya sana ,na kubwa zaid hawa wengne wanamakosa meng zaid ya walilofanya wapinzan na bado nchi inakua kama yao
 
Mbona unawahukumu wapinzan kwa kosa ambalo kwanza ni la kimkakat ivyo ivyo ni kosa ambalo litabak kuwa doa lkn ni funzo ,na pia kutoka sehem moja ukaenda upande wa pil ukapewa dhamana ata ccm wanafanya sana ,na kubwa zaid hawa wengne wanamakosa meng zaid ya walilofanya wapinzan na bado nchi inakua kama yao
Kosa ni kosa tu mkuu na ukifanya jua lazima watu watapoteza imani na wewe. Kwa upinzani lile lilikua kosa kubwa mno, haiwezekani mtu miaka yote mnamchafua halafu eti ndani ya wiki mbili mnamuita ni mtakatifu halafu wale walioongoza mapambano ndani ya chama kwa miaka zaidi ya kumi wanakuja kuonekana hawafai.

Mimi kama mtu ninaejielewa huwezi kunichezea akili kiasi hicho mkuu. Hata chama tawala sawa wanapokea mtu kutoka upinzani lkn haiwezi kukabidhiwa nafasi nyeti kama ile ndani ya muda mfupi sana.
 
Back
Top Bottom