"CCM " Ndio Chanzo cha Maendeleo, Umaskini umesababishwa na Mwananchi mwenyewe

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,100
Moja ya dhana katika ulimwengu wa Vihatarishi wanasema" It is easy to manage Risk than Crisis, Management of crisis ni gharama kubwa sana, kwa lugha ya isiyo rasmi wanasema si rahisi kulizuia janga kwani Janga tayari limetokea lakini ni rahisi kutatua au kuzuia vitu ambavyo vinaweza pelekea kwenye janga

Wananchi wengi wa Tanzania tayari ni Janga au crisis wanalala na kuamka wanafikiri umaskini wao au utajiri wa wengine umesababishwa na ccm Kama chama hilo sio kweli kabisa, Wananchi wenyewe wamejisababishia umaskini wa fikra tangu uhuru

Watanzania wengi Baada ya uhuru walijenga fikra Sasa mkoloni alitutumikisha sana ni muda wa kupumzika, na kweli walipumzika wakisubiri serikali mpya ilete maendeleo kwenye familia zao, Nani asiyejua jinsi Nyerere Rais alipopita maeneo ya Njombe na Ruvuma akitishia watu lazima walime sana mahindi baada ya kugundua wanabweteka tu ,kuna kipindi watu walifanaya kazi za shamba kuogopa ma DC na wakuu wa mikoa ,Je hili ni kosa la ccm ?

Nani asiyejua hulka ya watanzania kuchangia ngoma na harusi badala ya kushikamana kuchangia baadhi ya watoto wapate elimu ,Ni jambo la kawaida kusikia sherehe imegharimu milioni 20 Huku Bi harusi na Bwana harusi wanatoka koo zenye umaskini uliotopea na koo yenye watoto wengi wasiosoma, Hili ni kosa la ccm ?

Leo hii miaka mingi imepita tangu uhuru, kimezaliwa kizazi kipya kabisa cha 1990's ambacho Ndio kimemaliza shule na vyuo kwenye ulimwengu wa technology, kizazi hiki kimesoma kwenye ulimwengu wa You tube, Facebook na WhatsApp, Nani asiyejua jinsi hawa vijana wanatumia kuanika maungo yao na kujadili mambo ya betting tu, Je umaskini wa hawa watoto na watoto wao baadae ni kosa la ccm ?

Miaka hii ya kuanzia 2005 to 2010.enzi za Kikwete nani asiyejua mzunguko wa pesa ulivyokuwa mkubwa na watu wengi waliamua kuacha kazi na kufanya biashara wakiamini kazi ni utumwa ,Wakati wazungu mtu hufanaya kazi zaidi ya tano au kumi bila kudharau kazi mojawapo, Fikra kuwa kazi moja ni zuri kuliko nyingine imewafanya vijana kutokuwa na msimamo na msingi imara leo anafunga hiki kesho anaanza kile, Nani asiyejua vijana hufuata upepo wakisikia matikiti yamezaa sana mwaka huu basi wote mwakani watalima matikiti na kuacha kazi moja, Hili kosa la kufuata upepo ni kosa la ccm ?

Kuendekeza siasa za majitaka na uchama ,kujadili Viongozi masaa 24 siku saba kwa week badala ya kufanya kazi Ndio agenda ya kuelekea 2020.Nani asiyejua wanaojadiliwa wana miradi na maendeleo ya kutupwa, Makosa kama haya yaliletwa na ccm ?

Wananchi lazima watambue maendeleo yao yanaletwa na wao wenyewe kwa kubadili fikra zao binafsi, Hata siku moja ccm haikuwahi msababishia mtu umaskini tangu kuanzishwa kwake

Sisi wananchi ndio tumeisababishia ccm umaskini Jaribu kuangalia wanaojiuzulu ubunge ili ccm iingie gharama, Jaribu kuangalia sauti za Komu na kubenea wakipanga uhuni ili serikali na chama viingie gharama

Tutatoa povu lakini maisha yako yapo mikononi mwako mwenyewe binafsi, Chama kipo pale Kama holistic structure tu

Maswali ya kujiuliza :
Je, Taratibu na kanuni tulizonazo Kuna siku zitabadilika au ni wananchi wenyewe wabadili fikra zao ili wakifanye chama kilete maendeleo, na sio kukisubiri kiwaletee maendeleo

Ni nani anayeeneza sera na Itikadi kwa miaka hii karibuni, Je si ni vijana wenzenu mliowaunga mkono leo mnawaona mwiba na wasaliti, Hata siku moja maendeleo hayaletwi na chama bali watu hufanya chama kilete maendeleo

Hitimisho :

Kusubiri chama kilete maendeleo hakuna tofauti na kumchukua mbuzi beberu kumuweka angalie UEFA champions league ataona mnampotezea muda wa kula nyasi
 
Mimi nakwambia pamoja na uzembe wa wananchi pia chama chetu kinailea serikali inayomkandamiza mwananchi kwenye kodi, kwenye kupunguza mzunguko wa hela mtaani, kiwatisha wawekezaji ambao wangeleta ajira kwa watu,
Haiwapi ulinzi wananchi na wawekezaji na wanapotea kwa kutekwa,

Mimi ni CCM huru, siyo parasite ambaye anaongea kushabikia tu kutafta ulaji,

Mimi ni CCM huru nisiyetetea upuuzi
 
Mimi nakwambia pamoja na uzembe wa wananchi pia chama chetu kinailea serikali inayomkandamiza mwananchi kwenye kodi, kwenye kupunguza mzunguko wa hela mtaani, kiwatisha wawekezaji ambao wangeleta ajira kwa watu,
Haiwapi ulinzi wananchi na wawekezaji na wanapotea kwa kutekwa,

Mimi ni CCM huru, siyo parasite ambaye anaongea kushabikia tu kutafta ulaji,

Mimi ni CCM huru nisiyetetea upuuzi
Nimekuelewa mkuu, Lakini mambo mengi yamekuwa ya kusikia sikia yaani "hear say na Rumours " Mimi binafsi sijawahi ona watu wakitoa suluhisho ya matatizo ya nchi hii bali wanasubiri Viongozi wateleze halafu wanaanza kupiga siasa mitandaoni

Mfano ukisema Rais amekosea kununua ndege ilibidi waseme kingenunuliwa kitu gani ?

Au Mbowe aache uenyekiti wangesema nani anafaa kuwa mwenyekiti ?

Kiuhalisia umaskini wa watanzania ni fikra zao ,Serikali imeongeza kodi ? nini kifanyike kufidia kodi hiyo ?

Hatuwezi kuendelea kwa fikra zenye kujaa mawazo yanayofanana kusubiri Viongozi wakosee tuwacheke
 
Maana ya kuwepo shule za Serikali na kutoa Elimu bora ni nini na nini madhara yake zisipokuwepo au zikawa hazitoi elimu bora.
Kwa nini Serikali inasimamia na kuweka mifumo ya Elimu, nini madhara yake kusipokuwepo misingi bora ya elimu? na nini madhara kwa wananchi kusipokuwepo na misingi bora ya elimu?
 
mkuu kutegemea maendeleo kupitia magenge yaitwayo vyama vya siasa ni kujichelewesha. hayo ni makundi yaliyohalalishwa kisheria kupora raslimali za wavuja jasho wa nchi hii. tuna miaka karibu 60 tangu uhuru lakini mambo yaliyofanyika hayaendani na umri wetu tangu uhuru....
 
Hongera mkuu mawazo yako ni mazuri, ipo siku wananchi watajitambua ili lawama hii juu yao iondoke (wapate maendeleo).

Ila tambua kua kwenye hilo "badiliko" la kujitambua si ( CCM) wala si( Chadema) itakua madarakani bali ni "kiongozi" kutoka chama chochote hapo juu mwenye uchungu na atakayefuata misingi ya sheria.
 
Kwanini serikali inamiliki hospitali zake na kusimamia huduma za Afya? Nini kitatokea huduma za Afya zikiwa mbovu?, ipi athari kwa mwananchi huduma za afya zikiwa mbovu?
 
mkuu kutegemea maendeleo kupitia magenge yaitwayo vyama vya siasa ni kujichelewesha. hayo ni makundi yaliyohalalishwa kisheria kupora raslimali za wavuja jasho wa nchi hii. tuna miaka karibu 60 tangu uhuru lakini mambo yaliyofanyika hayaendani na umri wetu tangu uhuru....

Tufanyeje sasa mkuu maana hayo magenge ndio yanatoa mgombea uraisi na huyo mgombea ndiye huwa raisi.
 
Moja ya dhana katika ulimwengu wa Vihatarishi wanasema" It is easy to manage Risk than Crisis, Management of crisis ni gharama kubwa sana, kwa lugha ya isiyo rasmi wanasema si rahisi kulizuia janga kwani Janga tayari limetokea lakini ni rahisi kutatua au kuzuia vitu ambavyo vinaweza pelekea kwenye janga
Kwa kusoma andiko lako kwenye kichwa cha habari na hii aya ya kwanza umeshindwa kujua uandike kitu gani. Ukitaka kuchambua mada kwanza jaribu kuelewa unachotaka kuandika. Lengo sio kukutafitia mJibu ila ni vema ukajua unataka kufafania nini. Inashangaza hujui hata maana ya neno Risk. Pili hujui maana ya neno Crisis. Katika haya mawili hakuna lolote linalomaanisha janga. Kwa vile umeanza kupoteza uelekeo wa ulichotaka kuandika imekuwia rahisi kupata jibu kuwa maendeleo ya Tanzania yanaletwa na ccm ila umaskini wa Tanzania ya leo umesababishwai wananchi . Hapa unahitajika kuwa smart vinginevyo utaleta majibu kama ngonjera ulizoandika.
 
Tufanyeje sasa mkuu maana hayo magenge ndio yanatoa mgombea uraisi na huyo mgombea ndiye huwa raisi.
mkuu tafuta kitabu kimeandikwa kwaheri uhuru, kwa heri mkoloni utajifunza mengi. kiufupi pambana na hali yako. tulichokipigania ili kupata uhuru sich tukifanyacho.
 
Maswali bado magumu kichwani kwangu, Kama wananchi wanafanya kazi kwa bidii na kodi wanalipa kubwa na kodi yao haijengi miundombinu bora na rahisi kwa wao kufanya kazi kwa bidii hapo napo wasiilaumu Serikali kwa kuwaletea umasikini?
 
Samurai, Mawazo ya watu sasa hasa vijana ni uvyama tu kichwani, Mtu hana mawazo zaidi ya kufikiri ccm ndio tumeisababishia umaskini

Hiyo ccm imemsababishia umaskini Babu na Bibi, Baba na Mama, Sasa wewe na Mkeo, Unasubiri isababishe umaskini kwa wajukuu zako ?
 
Haya unayoleta ingepaswa yaletwe na polepole baada ya miaka 50+ ya uhuru.
Unataka kutuambia kazi ya serikali ni kuleta au kuhalalisha umasikini?
 
mkuu tafuta kitabu kimeandikwa kwaheri uhuru, kwa heri mkoloni utajifunza mengi. kiufupi pambana na hali yako. tulichokipigania ili kupata uhuru sich tukifanyacho.

Nani alaumiwe sasa mkuu, na nini kifanyike maana tuko kwenye mjadala huru hapa. Kitabu nitakitafuta nikisome.
 
Back
Top Bottom