Wabogojo
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 354
- 87
Habari Wana JF!
Katika hali isiyo ya kawaida Spika wa Bunge leo tena ameahirisha kikao cha Bunge kwa mara nyingine baada ya kufanya hivyo jana. Sababu ya kufanya hivyo ni baada ya Wapiganaji na wawakilishi wa wananchi mle Bungeni kuomba Miongozo na Spika kutupilia mbali maombi ya miongozo ya Upinzani na hivyo kuanzisha sintofahamu kwa kuanza kupiga kelele na huku bila hata AIBU, Mh Simbachawene aliendelea tu kusoma mswaada huo as if yale makelele alikuwa hayasikii.
Kinachoonekana hapa ni kwamba kutakuwa na SIRI nzito inayo wasukuma hawa Wabumge wa CCM na serikali yao kutaka kutaka kupitisha huu mswaada kwa maslahi ya watu wachache badala ya wananchi wote. Na kwa kuwa Wabunge wa UKAWA wameonyesha kuugomea huo Mswaada wa maguta na gesi asilia na vema basi watueleze umma ni nini kilichopo nyuma ya pazia na kufanya mswaada huu pamoja na mingine mitatu kuingizwa Bungeni kwa hati za dharula huku kukiwa hakuna ulazima kihivyo.
Ingekuwa vema sana kama hoja ya Mh Mnyika ingekubaliwa kwa kuweka pembeni moswaada yote na badala yake Bunge lijadili kusuasua kwa zoezi la uandikishaji wapiga kura ikiwa ni pamoja na mapungufu yake kwa kutumia BVR, lakini pia kagusia suala la uwepo wa Tume huru ya Uchaguzi mboma jambo kama hili nyeti na kwa mstakabali kwa Uchaguzi ulio huru na haki hata halitengenewi mswaada na kuingizwa Bungeni kwa hati ya dharula huku ikizingatiwa kuwa wana siku chache sana za kuwepo bungeni na miezi michache sana kukaribia tarehe ya uchaguzi mkuu hapo Octoba 2015.
My Take:
Mosi, tunaomba UKAWA waueleze UMMA ni nini walicho kiona nyuma ya pazia la CCM juu ya miswaada yao hii ns kama kina harufu ya UFISADI basi ni bora tuelezwa tujue kuliko kuaminishwa kwamba Wabumge wa UKAWA ni watu wa fujo na dharau kwa BUNGE letu TUKUFU.
Pili nataka niwaulize Wabunge wa CCM ni kwa nini mara nyingi wanakuwa against na hoja nyingi zenye maslahi kwa wananchi na badala yake wanakuwa watetezi wa Serikali, hivi wanajua gharama yake? OK tutakutana nao baadaye Octoba 2015.
Katika hali isiyo ya kawaida Spika wa Bunge leo tena ameahirisha kikao cha Bunge kwa mara nyingine baada ya kufanya hivyo jana. Sababu ya kufanya hivyo ni baada ya Wapiganaji na wawakilishi wa wananchi mle Bungeni kuomba Miongozo na Spika kutupilia mbali maombi ya miongozo ya Upinzani na hivyo kuanzisha sintofahamu kwa kuanza kupiga kelele na huku bila hata AIBU, Mh Simbachawene aliendelea tu kusoma mswaada huo as if yale makelele alikuwa hayasikii.
Kinachoonekana hapa ni kwamba kutakuwa na SIRI nzito inayo wasukuma hawa Wabumge wa CCM na serikali yao kutaka kutaka kupitisha huu mswaada kwa maslahi ya watu wachache badala ya wananchi wote. Na kwa kuwa Wabunge wa UKAWA wameonyesha kuugomea huo Mswaada wa maguta na gesi asilia na vema basi watueleze umma ni nini kilichopo nyuma ya pazia na kufanya mswaada huu pamoja na mingine mitatu kuingizwa Bungeni kwa hati za dharula huku kukiwa hakuna ulazima kihivyo.
Ingekuwa vema sana kama hoja ya Mh Mnyika ingekubaliwa kwa kuweka pembeni moswaada yote na badala yake Bunge lijadili kusuasua kwa zoezi la uandikishaji wapiga kura ikiwa ni pamoja na mapungufu yake kwa kutumia BVR, lakini pia kagusia suala la uwepo wa Tume huru ya Uchaguzi mboma jambo kama hili nyeti na kwa mstakabali kwa Uchaguzi ulio huru na haki hata halitengenewi mswaada na kuingizwa Bungeni kwa hati ya dharula huku ikizingatiwa kuwa wana siku chache sana za kuwepo bungeni na miezi michache sana kukaribia tarehe ya uchaguzi mkuu hapo Octoba 2015.
My Take:
Mosi, tunaomba UKAWA waueleze UMMA ni nini walicho kiona nyuma ya pazia la CCM juu ya miswaada yao hii ns kama kina harufu ya UFISADI basi ni bora tuelezwa tujue kuliko kuaminishwa kwamba Wabumge wa UKAWA ni watu wa fujo na dharau kwa BUNGE letu TUKUFU.
Pili nataka niwaulize Wabunge wa CCM ni kwa nini mara nyingi wanakuwa against na hoja nyingi zenye maslahi kwa wananchi na badala yake wanakuwa watetezi wa Serikali, hivi wanajua gharama yake? OK tutakutana nao baadaye Octoba 2015.